Ibara ya 24:3 ya Sheria ya Utumishi wa Umma ina maana gani? Rais anaweza kumlazimsha jaji kustaafu?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Nilikuwa katika kujisomeasomea na kutafiti kitu fulani lakini nimekutana na hiki kipengele sijakielewa hasa. Ibara ya 24 ya sheria hiyo ya 2002 inazungumza kuondolewa kwa watumishi wa umma na inaanza kwa kusema kuwa

24:1 The president may remove any public servant from the service of the Republic if the President it in the public interest to do so. Except in the case of removal of a judge or other judicial officers, the procedure for the exercise of these powers shall be provided for in the Regulations.


Na sehemu ya 3 inasema kuwa:

A justice of appeal or a judge of the High Court may only be removed from office in exercise of power in pursuit of the procedure set out in the constitution; save that where the President removes a justice of appeal or a judge from office, the judge shall be deemed to have retired from the public service from the date of such removal from office.

Sasa najiuliza; ina maana kuwa Rais anaweza kumlazimisha Jaji wa Mahakama Kuu au wa Rufaa kustaafu? Inaposema "save that where" maana yake ni "isipokuwa pale ambapo" .. naomba mwanga kidogo itanisaidia katika kajiutafiti kangu fulani. Au kipengele hicho hakipo tena na kuwa majaji hawawezi kuondolewa na Rais isipokuwa kwa kanuni iliyowekwa kwenye Katiba?
 
Many lawyers prefer to read only few like to write. Let the only few share with us the clarification of those sections from their proffesional eyes.

Back to topic, that concluded Mahakama si huru. Kama watoto wanamtegemea baba kwa uongozi na baba ni mtumwa kisheria, ni upuuzi kwa watoto kusema wako huru.
 
Kwanza naomba kufanya marekebisho kidogo, neno 'Ibara' linatumika tupapozumzia KATIBA, kwenye SHERIA tuna 'Kifungu' hivyo unachozungumzia ni Kifungu cha 24 kwenye Sheria Namba 8 ya 2002 Sheria ya Utumishi wa Umma.
Nadhani umepata point nzuri tu kwamba utaratibu wa kuwaondoa Majaji na Mahakimu wa High Court ni tofauti, kuna procedure za kufuata kama zilivyoelekezwa kwenye Katiba, taratibu hizo zikikamilika Judge/Hakimu huyo anatangazwa amestaafu kwa manufaa ya umma. Kwa hiyo ni kweli Rais anaweza kumstaafisha kazi mtumishi yeyote wa Umma, kwa madaraka aliyopewa na Sheria ya Utumishi wa Umma isipokuwa kwa watumishi hao wa mahakama, anachofanya yeye ni kuanzisha hiyo hoja then taratibu zilizotajwa kwenye katiba zinafuata na zikikamilika na ikathibitika hoja ya Rais in ushahidi na faida kwa Umma, Judge/Hakimu huyo atastaafishwa.
Nadhani kilichokuchanganya ni hiyo tafsiri ya google ya 'save that where' katika 'content' hiyo isipokuwa pale si tafsiri iliyokusudiwa. Ni kukosekana tu kwa neno zuri la muendelezo ndio kumepelekea ugumu wa kupata tafsiri iliyokusudiwa.
 
Kwanza naomba kufanya marekebisho kidogo, neno 'Ibara' linatumika tupapozumzia KATIBA, kwenye SHERIA tuna 'Kifungu' hivyo unachozungumzia ni Kifungu cha 24 kwenye Sheria Namba 8 ya 2002 Sheria ya Utumishi wa Umma.
Nadhani umepata point nzuri tu kwamba utaratibu wa kuwaondoa Majaji na Mahakimu wa High Court ni tofauti, kuna procedure za kufuata kama zilivyoelekezwa kwenye Katiba, taratibu hizo zikikamilika Judge/Hakimu huyo anatangazwa amestaafu kwa manufaa ya umma. Kwa hiyo ni kweli Rais anaweza kumstaafisha kazi mtumishi yeyote wa Umma, kwa madaraka aliyopewa na Sheria ya Utumishi wa Umma isipokuwa kwa watumishi hao wa mahakama, anachofanya yeye ni kuanzisha hiyo hoja then taratibu zilizotajwa kwenye katiba zinafuata na zikikamilika na ikathibitika hoja ya Rais in ushahidi na faida kwa Umma, Judge/Hakimu huyo atastaafishwa.

Nashukuru sana kwa usahihisho; kwenye katiba inasemwa ni tume ndio kimsingi inafanya uchunguzi na ikiwa na ushahidi wa kutosha inapendekeza kwa Rais jaji au hakimu kuondolewa kwa manufaa ya umma. Kwa hiyo, ni salama kusema kuwa Rais hawezi kumstaafisha jaji wa mahakama kuu au rufani au mtumishi wa mahakama bibila kuhusisha tume. Hawezi tu kutangaza kuwa ameamua kumstaafisha jaji au mtumishi wa mahakama bila kuundwa kwa tume kama article 110 ya katiba inavyotaka?
 
Kwanza naomba kufanya marekebisho kidogo, neno 'Ibara' linatumika tupapozumzia KATIBA, kwenye SHERIA tuna 'Kifungu' hivyo unachozungumzia ni Kifungu cha 24 kwenye Sheria Namba 8 ya 2002 Sheria ya Utumishi wa Umma.
Nadhani umepata point nzuri tu kwamba utaratibu wa kuwaondoa Majaji na Mahakimu wa High Court ni tofauti, kuna procedure za kufuata kama zilivyoelekezwa kwenye Katiba, taratibu hizo zikikamilika Judge/Hakimu huyo anatangazwa amestaafu kwa manufaa ya umma. Kwa hiyo ni kweli Rais anaweza kumstaafisha kazi mtumishi yeyote wa Umma, kwa madaraka aliyopewa na Sheria ya Utumishi wa Umma isipokuwa kwa watumishi hao wa mahakama, anachofanya yeye ni kuanzisha hiyo hoja then taratibu zilizotajwa kwenye katiba zinafuata na zikikamilika na ikathibitika hoja ya Rais in ushahidi na faida kwa Umma, Judge/Hakimu huyo atastaafishwa.
Nadhani kilichokuchanganya ni hiyo tafsiri ya google ya 'save that where' katika 'content' hiyo isipokuwa pale si tafsiri iliyokusudiwa. Ni kukosekana tu kwa neno zuri la muendelezo ndio kumepelekea ugumu wa kupata tafsiri iliyokusudiwa.

Kuongezea ni kwamba judge au magistrate ataondolewa kwenye utumishi sio rais anaposema tu bali yeye ataondolewa baada ya judicial commission kukaa na kuamua kama kweli kuna haja ya kufanya hivyo, kwa maana hiyo haki zake zote za malipo na mengineyo hufuata. Hicho ndo kinachoongelewa hapo. Ni kawaida kabisa kwani kumbuka hakuna total independence ya organ of the state bila check and balance. Na ili kupunguza tyranny na unscrupulous behaviour katika kumuondoa judge ndipo commission hukaa kuangalia umuhimu wa kufanya hivyo hapo swali hubakia kama kweli hiyo tume ya maadili ya mahakama itatenda haki kwa mhusika.
 
Hivi Jaji anapotoa maamuzi ya kipuuzi kama alivyofanya kwenye kesi ya Lema Arusha anawajibishwa kivipi na hiyo Commission? au ndio mpaka Rais alianzishe? huku tukiwa tumesahau kuwa huyo huyo Rais ndie alimpendekeza, Akamu interview, akamchagua, akamwajiri, akamthibitisha kazini etc..

Kweni wenzetu wa Kenya wanafanyaje katika hoja hii?
 
Hivi Jaji anapotoa maamuzi ya kipuuzi kama alivyofanya kwenye kesi ya Lema Arusha anawajibishwa kivipi na hiyo Commission? au ndio mpaka Rais alianzishe? huku tukiwa tumesahau kuwa huyo huyo Rais ndie alimpendekeza, Akamu interview, akamchagua, akamwajiri, akamthibitisha kazini etc..

Kweni wenzetu wa Kenya wanafanyaje katika hoja hii?

Mambo ya kenya ni yao mkuu, cha muhimu unatakiwa kufahamu judge anapotoa maamuzi ya kesi anakuwa 'functus officio' na kuna kinga anayopata kwa maamuzi hayo. Kuna njia mbalimbali za kuweza kupata suluhisho kama kukata rufaa nk. Ila kumbuka jaji au hakimu sio watu wa kudhaniwa kuwa na uhuni wa namna hiyo lakini pindi itakapofahamika mahakama ya juu yaweza kutengua hukumu hiyo either by its own motion au kwa kupelekewa.
 
Back
Top Bottom