Ibara ya 102 ya Katiba ya Muungano: Seif na Balozi Idi vyeo vyao havimo

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
Katiba ya Muungano inaweka utaratibu wa vyeo vikuu vya Serikali ya Zanzibar na inaelezea juu ya vyeo vingine au taratibu nyingine kwa mujibu wa "katiba hii (ya MUungano) na Katiba ya Zanzibar". Je Makamu wa Rais wa Zanzibar Seif na Idi wana nafasi yoyote wanapokuja kwenye Muungano. Kwa mfano, wakisimama mawaziri wa Tanzania na Waziri Mkuu wa Tanzania hawa wanasimama kama viongozi wa kitaifa?
 
Katiba ya Muungano inaweka utaratibu wa vyeo vikuu vya Serikali ya Zanzibar na inaelezea juu ya vyeo vingine au taratibu nyingine kwa mujibu wa "katiba hii (ya MUungano) na Katiba ya Zanzibar". Je Makamu wa Rais wa Zanzibar Seif na Idi wana nafasi yoyote wanapokuja kwenye Muungano. Kwa mfano, wakisimama mawaziri wa Tanzania na Waziri Mkuu wa Tanzania hawa wanasimama kama viongozi wa kitaifa?
Hapo nilipobold ndiyo taratibu iliyofuata.
 
unajua kilichotokea hapo ni kuirekebisha kidogo katiba ya Zanzibar kwa ajili ya kipindi cha mpito kwani Serikali ya Umoja wa Kitaifa si yakudumu ni ya mpito tu,sasa hapo sijui itakuwa accomodated vipi kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,any way ngoja tuwasikie Great thinkers wengine wa JF watatujuza vipi.
 
Katiba ya Muungano inaweka utaratibu wa vyeo vikuu vya Serikali ya Zanzibar na inaelezea juu ya vyeo vingine au taratibu nyingine kwa mujibu wa "katiba hii (ya MUungano) na Katiba ya Zanzibar". Je Makamu wa Rais wa Zanzibar Seif na Idi wana nafasi yoyote wanapokuja kwenye Muungano. Kwa mfano, wakisimama mawaziri wa Tanzania na Waziri Mkuu wa Tanzania hawa wanasimama kama viongozi wa kitaifa?

:help:
mkuu hii mada nzito.. wataalamu wa mambo ya kikatiba watusaidie katika hili
 
another point for the need of massive overhaul (or, say; retyping) of our constitution
 
Asante kwa kulitambua tatizo hilo.
Maalim na Balozi wanatambulika na Katiba ya Zanzibar kama viongozi wa taifa lao. Katiba ya JMT haikurekebishwa kupokea mabadiliko hayo ya karibuni. Tatizo linaonekana hata pale walipoketi Bungeni pembeni mwa spika hivi karibuni.
Ikumbukwe kuwa wazanzibar walipendekeza Rais wa SMZ arudishiwe cheo chake cha Makamu wa kwanza wa Rais. Kwa hio kuna mambo kibao yanatakiwa kurekebishwa ili kuendana na marekebisho yaliyo fanywa hivi karibuni.
Suluhu ya tatizo hilo na mengine mengi ya muungano yanatakiwa kuwekwa kwa wadau wote na katiba ya JMT iandikwe upya. Ila ndio hivyo..........ni mvutano tu.
 
Jamani hamjajua kuwa zanzibar ni nchi nyingine bada mnajipendekeza tu?waje huku ili iweje?watu 1m=25ministers = over 70 MP kwenye bunge letu = kikwete atakaoteua kuwa mawaziri halafu bado unataka wengine ni hivi TUMELIWA KWA UJINGA WA VIONGOZI WETU-TUPIGANIE KATIBA MPYA
 
Kwenye protokali ya Jamhuri ya Muungano tuna:

Rais
Makamu wa Rais
Waziri Mkuu wa Muungano
Rais wa Zanzibar??
Mawaziri wa Muungano au Makamu wawili wa Zanzibar
Makamu wa Wawili wa Zanzibar au Mawaziri wa Muungano
Mawaziri wa Zanzibar
Wakuu wa Mikoa

Naomba mnisaidie ikoje?
 
Kwenye protokali ya Jamhuri ya Muungano tuna:

Rais
Makamu wa Rais
Waziri Mkuu wa Muungano
Rais wa Zanzibar??
Mawaziri wa Muungano au Makamu wawili wa Zanzibar
Makamu wa Wawili wa Zanzibar au Mawaziri wa Muungano
Mawaziri wa Zanzibar
Wakuu wa Mikoa

Naomba mnisaidie ikoje?

Mwanakijiji, pole sana uko mbali.

Siku ile Wanatoka Kuzindua Bunge, ilifurahisha kuona Itifaki waliyoitumia kutoka ndani ya Bunge. From that one can judge, nani ni nani katika mpangilio wa vyeo.
 
Kwenye protokali ya Jamhuri ya Muungano tuna:

Rais
Makamu wa Rais
Waziri Mkuu wa Muungano
Rais wa Zanzibar??
Mawaziri wa Muungano au Makamu wawili wa Zanzibar
Makamu wa Wawili wa Zanzibar au Mawaziri wa Muungano
Mawaziri wa Zanzibar
Wakuu wa Mikoa

Naomba mnisaidie ikoje?

Kiprotokali rais wa Zanzibar anatajwa kabla ya Waziri Mkuu wa Muungano, lakini kikatiba serikali mbili zina operate parallely bila kuingiliana.
 


Toka kushoto mbele;Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein,Makamu wa Rais Serikali ya Muungano Dk. Mohamed Ghalib Bilali,Waziri Mkuu Mizengo Kayanda Peter Pinda,na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar,Mh. Seif Shariff Hamad.Kushoto nyuma;Jaji Mkuu Mh. Augustino Ramadhani,Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Mh Anne Makinda,Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Iddi Seif,Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano,Jaji Frederick Werema na Katibu Mkuu Kiongozi,Mh. Philemon Luhanjo.

You can now connect the dots . . . . .
 
Mwanakijiji naona sasa umeelekeza nguvu zako kwenye katiba....:teeth:

Safi sana lakini....
 
Kiranga, vyeo vya Serikali ya Zanzibar vya juu vimewekwa na Katiba ya Muungano na hata muundo wa serikali yake na nguvu zake uko kwenye Serikali ya Muungano. Ndio maana Rais wa Zanzibar anaapa kulinda Jamhuri ya muungano na kiapo cha serikali ya Zanzibar.
 
Kiranga, vyeo vya Serikali ya Zanzibar vya juu vimewekwa na Katiba ya Muungano na hata muundo wa serikali yake na nguvu zake uko kwenye Serikali ya Muungano. Ndio maana Rais wa Zanzibar anaapa kulinda Jamhuri ya muungano na kiapo cha serikali ya Zanzibar.

Kumbe unaongelea kutajwa, mimi nilifikiri unaongea hierarchy. Nchi yetu bora katiba na wala si katiba bora. Ndiyo maana tushawahi kuwa na "Naibu Waziri Mkuu" Mrema ambaye hakuwemo hata kwenye katiba.

Kuna watu wamesema kwa sababu hii ni serikali ya mpito hili halishangazi, lakini inakuwa awkward, ndiyo maana hata juzi Hamad alivyotaka kuingia bungeni ilibidi wabunge waulizwe, kwa sababu hatambuliki kwa katiba ya muungano.

Ingekuwa vizuri mabadiliko ya katiba yaangalie vitu hivi pia.
 
Mimi nina shaka sana kuwa huenda hata viongozi wetu waandamizi katika serikali hawaijui katiba!!
 
Mimi nina shaka sana kuwa huenda hata viongozi wetu waandamizi katika serikali hawaijui katiba!!

Katiba yenyewe haieleweki, kila ibara ya pili inaanza kwa kusema "bila ya kuathiri sehemu nyingine ya katiba hii blah blah blah..." clawbacks on clawbacks bonge la labyrinth fulani hivi.

Sehemu moja wanakwambia kila Mtanzania ana haki ya kupiga na kupigiwa kura, sehemu nyingine wanakwambia ili kupigiwa kura lazima uwe mwanachama wa chama cha siasa. Ile haki iliyotolewa mwanzo inachukuliwa na kifungu cha pili, na the most restrictive clause wins kwa sababu most of the ibaras zinaanza na "bila kuathiri sehemu nyingine ya katiba' or some bull like that.

Inatakiwa tuondoe huu upuuzi.

Mara nyingine naona wamefanya makusudi tu
 
Katiba ya Muungano inaweka utaratibu wa vyeo vikuu vya Serikali ya Zanzibar na inaelezea juu ya vyeo vingine au taratibu nyingine kwa mujibu wa "katiba hii (ya MUungano) na Katiba ya Zanzibar". Je Makamu wa Rais wa Zanzibar Seif na Idi wana nafasi yoyote wanapokuja kwenye Muungano. Kwa mfano, wakisimama mawaziri wa Tanzania na Waziri Mkuu wa Tanzania hawa wanasimama kama viongozi wa kitaifa?

Kwa muundo wa sasa wa muungano vyeo vyao havitambuliki kwani Katiba ya nchi haijabadilishwa kutambua hivyo vyeo. Hivyo kuja na kupokelewa kama viongozi wenye hadhi ya muungano ni kosa. Na hili ndio limekuwa tatizo la nchi yetu kwani mambo yanabadilishwa kienyeji. Vilevile ukifuata katiba ya sasa Rais wa Zanzibar ni mjumbe wa baraza la mawaziri hivyo ni kama mawaziri wengine chini ya Waziri Mkuu. Hii imebainishwa na Ibara ya 54 ya Katiba inayosema:

54.-(1) Kutakuwa na Baraza la Mawaziri ambalo wajumbe wake watakuwa ni Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Rais wa Zanzibar na Mawaziri wote.
(2) Rais atahudhuria mikutano ya Baraza la Mawaziri na ndiye atkayeongoza mikutano hiyo. Na endapo Rais hayupo basi mikutano itaongozwa na Makamu wa Rais na kama wote wawili Rais na Makamu wa Rais hawapo Waziri Mkuu ndiye ataongoza Mikutano hiyo.

Kwa hiyo kikatiba Raisi wa Zanzibar katika masuala yote ya Muungano yuko chini ya Waziri Mkuu. Lakini sivyo ilivyo kwani Raisi wa Zanzibar anafanywa kuwa ni kama mtu anayemfuata Raisi na baada ya hapo Makamu wa Raisi na Waziri Mkuu. Huu ni upindishaji wa wazi wa Katiba ya nchi. Kama kuna hoja kuwa mabadiliko ya 8 ya Katiba yalimshusha hadhi Raisi wa Zanzibar hilo ni suala la kufanyia kazi ili lirekebishwa na kumpa hadhi inayomstahili.

Kuhusu vyeo vya Seif na mwenzake hivyo kwa sasa havitambuliki na katiba yetu na hivyo wanapokuja Bara wao ni raia wa kawaida na hawatakiwi kupewa heshima yoyote ile ya uongozi zaidi ya ule wa vyama vyao. Kwa hiyo ni lazima vyeo hivi vipingwe kikatiba kwamba hadhi wanayopewa haitambuliwi na katiba ya JMT. Pili ni hoja nyingine ambayo inaonyesha kuwa Katiba yetu imepitwa na wakati na ni ni muhimu kwa nchi kuwa na katiba mpya.
 
Kiranga, vyeo vya Serikali ya Zanzibar vya juu vimewekwa na Katiba ya Muungano na hata muundo wa serikali yake na nguvu zake uko kwenye Serikali ya Muungano. Ndio maana Rais wa Zanzibar anaapa kulinda Jamhuri ya muungano na kiapo cha serikali ya Zanzibar.

Mwanakijiji:

Kwa sababu tupo kwenye katiba. Basi haitakuwa vibaya kuelezea mapungufu ya katiba. Moja ya mapungufu ya katiba ya Tanzania ni kuwa detailed. Na hivyo kufanya katiba yenyewe kuwa kitabu kikubwa na kigumu.

Hili katiba iwe a living document, vitu vingi vinatakiwa viwe abstract concepts. Kwa mfano kwa ibara ulizoelezea kuhusu serikali ya mapinduzi Zanzibar ilitakiwa iwe abstract concept tu. Katiba ingeweza kusema: "Serikali ya Zanzibar iundwe kwa kufuata taratibu za katiba ya Zanzibar".
Kwa mfano huu katiba ingewaachia waZanzibar kuunda muundo wa serikali yao wenyewe.

Mfano mwingine kuhusiana na abstract concept ni kufanya katiba iwe ndogo yenye kueleweka hata kwa mwananchi wa kawaida na yenye kutoa nafasi kwa vizazi vinavyokuja kutafsiri katiba kutokana na wakati wao bila kufanya mabadiliko ya katiba yenyewe. Marekani wana zaidi ya miaka 200 na katiba yao ina kurasa chini ya 40 na mabadiliko yasiopungua 30. Wakati sisi tuna kurasa zaidi ya 100 na bado hakuna kinachoeleweka.
 
Mwanakijiji:]Mfano mwingine kuhusiana na abstract concept ni kufanya katiba iwe ndogo yenye kueleweka hata kwa mwananchi wa kawaida na yenye kutoa nafasi kwa vizazi vinavyokuja kutafsiri katiba kutokana na wakati wao bila kufanya mabadiliko ya katiba yenyewe. Marekani wana zaidi ya miaka 200 na katiba yao ina kurasa chini ya 40 na mabadiliko yasiopungua 30. Wakati sisi tuna kurasa zaidi ya 100 na bado hakuna kinachoeleweka.

Yaani hapo mi ndo nachoka kabisa!!

Hata baraza la mawaziri la Marekani (yenye watu zaidi ya mil. 300) ni dogo kuliko la Tanzania yenye watu mil. 37-40! Go figure.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom