MAHENDEKA
JF-Expert Member
- Jul 9, 2010
- 306
- 152
p { margin-bottom: 0.08in; } Kwa wale waishio tanzania sijui kama uchunguzi huu mlishaufanya ama vipi ni kwamba ukitazama kwa makini noti ya shillingi elfu moja na noti ya shilingi elfu mbili(ila sio ya sh 5000/10000)sijui kwa nini, mara nyingi utakuta ule mstari wa kung'aa-ng'aa uliopo kwenye pesa hizo huwa umekwanguliwa na kufutika kabisa, na katika pitapita zangu za hapa na pale kuuliza kulikoni niliambiwa kuwa eti hiyo ni bidhaa muhimu kwa wale mateja(watumiaji wa madawa ya kulevya) na wanayoyauza pia...Nimejitahidi kuuliza jina la hiyo bidhaa na kwa madhumuni gani huwekwa kwenye pesa hizo bila mafanikio yeyote..Sasa swali nalojiuliza ni kwa nini bidhaa hiyo haramu ipatikane katika pesa halali za nchi?,na kwa jinsi inavyoonekana kama kweli kuna biashara chafu inafanyika kwa bidhaa hiyo basi soko lake litakuwa kubwa sana manake kila noti nayokutana nayo huwa imekwanguliwa!!manake inawezekana tukawa tunamtafuta mchawi kumbe ni sisi wenyewe