TEKNOLOJIA
JF-Expert Member
- Jan 6, 2014
- 4,306
- 2,559
Dr Slaa ni kila kitu ninachokihitaji kutoka kwa rais wangu mwingine ajaye,tatizo linakuja kwa huyu bwana F.A.M ambaye atakuwa na ushawishi mkubwa serikalini kama naye si kuwa sehemu ya hiyo serikali ijayo.Huyu bwana ana tuhuma nyingi za matumizi mabaya ya rasilimali za chama,udikteta,ung'ang'anizi wa madaraka,upendeleo.Ikiwa Dr Slaa atakuwa rais ataweza kumdhibiti huyu bwana hasa ikizingatiwa kuwa ndiye anayekifadhili chama?Ndipo tunapoona umuhimu wa kuwa na katiba itakayodhibiti madaraka ya rais ili kuondoe uwezekano wa rais ajaye kutawaliwa kimaamuzi na nguvu zilizo nje ya taasisi ya urais.Kuichagua CCM sitaweza kamwe,kwani kufanya hivyo ni sawa na kuisaliti imani yangu.Ninapingana na kila kitu CCM kinachoamini na kufuata.ACT-Tanzania ndiyo siifikirii kabisa kujiunga nayo,kile chama kinaundwa na watu waliopoteza mwelekeo na maono ya kisiasa,katika dunia hii ya leo tunahitaji chama chenye watu wenye vichwa safi vitakavyoweza enda sambamba na hii dunia iliyojaa watu wajanja sana.