i like Dr Slaa As My Next President,I Can't Stand F.A.M Inside The Government Walls!

TEKNOLOJIA

JF-Expert Member
Jan 6, 2014
4,306
2,559
Dr Slaa ni kila kitu ninachokihitaji kutoka kwa rais wangu mwingine ajaye,tatizo linakuja kwa huyu bwana F.A.M ambaye atakuwa na ushawishi mkubwa serikalini kama naye si kuwa sehemu ya hiyo serikali ijayo.Huyu bwana ana tuhuma nyingi za matumizi mabaya ya rasilimali za chama,udikteta,ung'ang'anizi wa madaraka,upendeleo.Ikiwa Dr Slaa atakuwa rais ataweza kumdhibiti huyu bwana hasa ikizingatiwa kuwa ndiye anayekifadhili chama?Ndipo tunapoona umuhimu wa kuwa na katiba itakayodhibiti madaraka ya rais ili kuondoe uwezekano wa rais ajaye kutawaliwa kimaamuzi na nguvu zilizo nje ya taasisi ya urais.Kuichagua CCM sitaweza kamwe,kwani kufanya hivyo ni sawa na kuisaliti imani yangu.Ninapingana na kila kitu CCM kinachoamini na kufuata.ACT-Tanzania ndiyo siifikirii kabisa kujiunga nayo,kile chama kinaundwa na watu waliopoteza mwelekeo na maono ya kisiasa,katika dunia hii ya leo tunahitaji chama chenye watu wenye vichwa safi vitakavyoweza enda sambamba na hii dunia iliyojaa watu wajanja sana.
 
Dr Slaa ni kila kitu ninachokihitaji kutoka kwa rais wangu mwingine ajaye,tatizo linakuja kwa huyu bwana F.A.M ambaye atakuwa na ushawishi mkubwa serikalini kama naye si kuwa sehemu ya hiyo serikali ijayo.Huyu bwana ana tuhuma nyingi za matumizi mabaya ya rasilimali za chama,udikteta,ung'ang'anizi wa madaraka,upendeleo.Ikiwa Dr Slaa atakuwa rais ataweza kumdhibiti huyu bwana hasa ikizingatiwa kuwa ndiye anayekifadhili chama?Ndipo tunapoona umuhimu wa kuwa na katiba itakayodhibiti madaraka ya rais ili kuondoe uwezekano wa rais ajaye kutawaliwa kimaamuzi na nguvu zilizo nje ya taasisi ya urais.Kuichagua CCM sitaweza kamwe,kwani kufanya hivyo ni sawa na kuisaliti imani yangu.Ninapingana na kila kitu CCM kinachoamini na kufuata.ACT-Tanzania ndiyo siifikirii kabisa kujiunga nayo,kile chama kinaundwa na watu waliopoteza mwelekeo na maono ya kisiasa,katika dunia hii ya leo tunahitaji chama chenye watu wenye vichwa safi vitakavyoweza enda sambamba na hii dunia iliyojaa watu wajanja sana.

TEKNOLOJIA,

Kwanza naungana na nakubaliana na wewe kabisa tunahitaji kudhibiti madaraka ya Rais

Pili,Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali hajawahi kuonyesha sehemu yoyote katika ripoti yake juu ya hizo tuhuma ulizorusha

Hebu tuwe na facts tunapoanzisha mada hapa JF sasa ili kulinda heshima yako,wenzako na Jukwaa kwa ujumla wake

Siku njema.
 
Last edited by a moderator:
TEKNOLOJIA,

Kwanza naungana na nakubaliana na wewe kabisa tunahitaji kudhibiti madaraka ya Rais

Pili,Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali hajawahi kuonyesha sehemu yoyote katika ripoti yake juu ya hizo tuhuma ulizorusha

Hebu tuwe na facts tunapoanzisha mada hapa JF sasa ili kulinda heshima yako,wenzako na Jukwaa kwa ujumla wake

Siku njema.

Uko dunia ipi usione tuhuma za ubadhirifu zinazoelekezwa kwa king muswati?
 
Last edited by a moderator:
Kumbuka pia slaa ni mzinzi sana.amepora mke wa mtu na kutelekeza familia

Hiyo ahusiani na utendaji wake,mbona tulikuwa na-rais aliyemchukua mke wa kigogo mwingine wa serikali kuwa mke wake?au wenzetu uadilifu mnautazamaje?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom