Hydroponic fodder, Mkombozi pekee wa wafugaji wa ng'ombe, kuku, nguruwe, mbuzi na kadhalika

Ni sahihi pia kutumia mtama mweupe na hata uwele, kwani jamii zote hizi kuwa zinauwezo wa kukusanya virutubisho vingi vinavyohitajika kwa wanyama katika hatua za awali za ukuaji wa mimea hii.
 
14084122803_543d8455e0_b.jpg


images
Kenya_1.jpg


Gharama za kutengeneza chakula cha mifungo hautaji kuanza na vitu vya gharama kubwa, muhimu ni kutenga eneo, kisha jenga banda kama la kuku, juu funika kwa plastic pembeni pia funika kwa plastic. Tengeneza vichanja vya miti vya kushikilia tray za bati au plastic. Kichanja kimoja kinaweza kuwa na row tatu, nne, sita au kumi itategemea urefu wa banda lako.

Zipo mbegu na virutubisho vingine unachanganya pamoja kisha unamwaga juu ya tray na kumwagilia maji, baada siku mbili mbegu huchipua na baada ya siku nane tayari unakuwa na malisho kwa mifungo yako. Kumbuka kilimo hiki hakihitaji udongo kuoteshea mbegu.

Ukiwa na banda la futi 20 kwa 10 linatosha kuotesha nyasi za kulisha ng'ombe 50 wakubwa, au kulishia mbuzi zaidi ya 150 kwa mwaka mzima.



0.jpg


48c0dede5a1e164757de75bdac57e9d3.jpg
Banda lina umuhimu gani?
 
Hydroponic fodder haihitaji mbolea yoyote zaidi ya maji.
Hatua ya kwanza ni uchaguzi wa mbegu,
Unaweza kutumia mbegu za mahindi, mtama, uwele, shayiri au ngano. Unaziloweka kwenye maji na zile zinaoelea unazitupa.
Baada ya hapo unaziloweka kwenye ndoto ya maji chumvi au magadi kwa masaa mawili Kisha unazitoa na kuzisafisha na maji ili kuondoa chumvi au magadi.
Ukishatoka hatua hii unazifuka kwenye kitambaa cheusi na kuziweka gizani masaa 48.
Baada ya hapo unazisambaza kwenye beseni ambalo Lina vitundu vidogo dogo ili kuruhusu maji yanayotoka kupita. Hakikisha tray zako umezitengenezea sehemu ya kukaa pia ziwe zimewekwa sehemu yenye kivuli.
Inatakiwa kumwagilia asubuhi na jioni baada ya siku saba zitakuwa tayari kutumika hapo Kila moja inazalisha kilo nane.
Nimeeleza kwa ufupi hatua muhimu.
Hydroponic fodder haihitaji mbolea ya haina yoyote zaidi ya maji.
 
Back
Top Bottom