huyu waziri anawaonya vijana au anawahamasisha kujirusha na mafataki?

Akili Kichwani

JF-Expert Member
Jan 7, 2010
1,508
216
wadau......

hapo kwenye hiyo link kuna habari inayomhusu waziri mpta terezya hovisa akisimulia maisha yake chuoni............. eti ali[okuwa cho kikuu alipewa mimba na "fataki" na kisha huyo "fataki" alimsomesha hadi leo ni dr............ hajasema kama huyo "fataki" ndiye aliyemuoa........... fuatilia mwenyewe uone zaidi.............

Waziri atoa ushuhuda alivyorubuniwa na fatak

sasa naona maana ya fataki imechukua mkondo mwingine............. natarajia mwanafunzi wa cho kikuu ni mtu mzima na kila anachofanya anakielewa vizuri na madhara yake............ sioni haja ya kutumia fataki hapo ............ pia anasema baada ya kumpa mimba aliendelea kumsomesha hadi leo amefikia u-dr na sasa uwaziri......... sasa nauliza....

1. hivi huyu fataki ni mbaya kweli?...........
2. hapo anawaonya au anawahamasisha kujitafutia mafataki wazuri watakaowasaidia kufikia malengo yao ya elimu?............
3. mwanafunzi wa chuo kikuu amabaye anatarajiwa kuwa mwerevu kuhusu mapenzi na hata masuala ya uzazi wa mpango, anapojiingiza kwenye mapenzi na hata baadaye kupata mimba naye asingizie fataki?..............

naona mawaziri kama hawa hawajaanza kazi bado............ bado wamelewa na uteuzi................
 
Waziri atoa ushuhuda alivyorubuniwa na fatak Send to a friend Tuesday, 30 November 2010 21:23 0diggsdigg

i Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dk Terezya Luoga Hovisa jana alitoas ushuhuda wa kusikitisha wa maisha yake katika kongamano lililoandaliwa na Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), alipoeleza kuwa alipewa uja uzito na 'Fataki' wakati akisoma Chuo Kikuu.

Waziri Luoga alilazimika kushirikisha vijana hao kuhusu maisha yake kutaka kuwaonyesha alivyomudu kuvumilia na kupambana na maisha hadi kufikia mafanikio aliyoyapata sasa, akisema badala yake sasa anaweza "kuchakachua" hadi wanaume watano lakini "haoni sababu" na kuwataka wanafunzi kuepuka watu wenye tabia za kifataki kwa kuwa wanaweza kuwaharibia mwelekeo wa maisha.

Fataki ni jina maarufu waliopachikwa wanaume ambao wana tabia ya kufuata mabinti wadogo na kuwatelekeza baada ya kuwaharibia maisha kwa kuwapa mimba. Waziri Luoga alieleza jinsi alivyokutana na mwanamume huyo ambaye alimpa uja uzito, lakini akaongeza kuwa baadaye mtu huyo alimsomesha na hivyo kumaliza vizuri masomo. "Sio kwamba muige mfano nilioutoa," alisema Waziri Luoga akiwaambia wanafunzi hao. "Si kwamba na nyie kama wanafunzi mkayafanye haya, la asha! Badala yake ninawapa changamoto kwamba katika maisha silaha mnayopaswa kuing'angania ni elimu peke yake na si vibaka wa mitaani," alisema Dk Luoga. "Acheni kudanganywa na mafataki ambao ni matapeli na ambao huweza kuwapotezea dira ya maisha, badala yake msome kwa bidii, kwa ajili ya mafanikio ya maisha yenu." Dk Luoga alisema kuwa vijana wengi, hasa wanafunzi wamekuwa wakirubuniwa kutokana na kushindwa kustahimili tamaa za maisha na kuamua kujiingiza kwa vijana wa mitaani ambao aliwaelezea kuwa hawana sera.

Waziri huyo, ambaye ni sura mpya katika baraza lililoundwa hivi karibuni na Rais Jakaya Kikwete, alikumbushia taaluma yake ya ualimu kwa kutumia kalamu na kuwafundisha washiriki wa kongamano hilo masuala ya maisha na athari za ukimwi kwa vijana, huku akijitangza kuwa naye ni mtoto wa mkulima. "Ni bora kuacha kabisa na kuamua kusubiri kwani kwa kuwa mahusiano katika masomo ni hatari... badala yake mzidi kumuomba Mungu na kuwa waadilifu," alisisitiza "Leo hii, ninamshukulu Mungu kwa Elimu aliyonipa kwa sababu alinijua mimi ni mtoto wa mkulima, hivyo niliamua kutochezea maisha yangu kiholela. "Hapa unavyoniona, kama waziri nina fedha za kutosha; gari la kifahari ninalo ehe! Unadhani nikitaka kuwa na mafataki hata watano, nitashindwa?" "Nikiamua kuchakachua wanaume hata watano, naweza kwa sababu uwezo ninao na fedha ninayo.

Lakini sioni faida yeyote badala yake ni kujitumbikiza mahali ambapo ni hatari zaidi," alisema. "Cha msingi hapa ni kuhakikisha mnajenga maadili mema mnapokuwa shuleni na nyumbani ili kuepuka kurubuniwa na kupoteza mwelekeo wa elimu mliopata." Naye mtaalamu wa ushauri wa afya katika kamati ya vijana, Dk Telesphoy Kyaruzi alisema tatizo kubwa linalowapelekea vijana wengi kujiingiza katika ngono zembe na kupata maambukizi ni uchumi mbovu. Dk Kyaruzi alisema kwa kuliona hilo, wanaiomba serikali kuhakikisha inatoa mikopo kwa vijana ili kuwasaidia waweze kujiendesha na kuepuka vishawishi.
 
Rais wangu mpendwa aliwahi kusema wanaopata mimba mashuleni ni kiherehere chao... Si mimi bali nime-quote tu kutoka kwenye literature

Una uhakika ulimchagua?
 
KWELI KABISA MKUU.... kazi anayo na ukizingatia jamaa mwenyewe ndio aliwaita viherehere... LOL

dah, mkuu umenikumbusha kauli muafaka sana ya mkuu wa kaya............. kumbe ndio hao waliopata mimba kwa viherehere vyao na sasa anawaambia dada zetu kuwa sometimes viherehere vinalipa.................. aisee!!!...................
 
Waziri atoa ushuhuda alivyorubuniwa na fatak Send to a friend Tuesday, 30 November 2010 21:23 0diggsdigg

i Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dk Terezya Luoga Hovisa jana alitoas ushuhuda wa kusikitisha wa maisha yake katika kongamano lililoandaliwa na Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), alipoeleza kuwa alipewa uja uzito na 'Fataki' wakati akisoma Chuo Kikuu.

Waziri Luoga alilazimika kushirikisha vijana hao kuhusu maisha yake kutaka kuwaonyesha alivyomudu kuvumilia na kupambana na maisha hadi kufikia mafanikio aliyoyapata sasa, akisema badala yake sasa anaweza "kuchakachua" hadi wanaume watano lakini "haoni sababu" na kuwataka wanafunzi kuepuka watu wenye tabia za kifataki kwa kuwa wanaweza kuwaharibia mwelekeo wa maisha.

Fataki ni jina maarufu waliopachikwa wanaume ambao wana tabia ya kufuata mabinti wadogo na kuwatelekeza baada ya kuwaharibia maisha kwa kuwapa mimba. Waziri Luoga alieleza jinsi alivyokutana na mwanamume huyo ambaye alimpa uja uzito, lakini akaongeza kuwa baadaye mtu huyo alimsomesha na hivyo kumaliza vizuri masomo. "Sio kwamba muige mfano nilioutoa," alisema Waziri Luoga akiwaambia wanafunzi hao. "Si kwamba na nyie kama wanafunzi mkayafanye haya, la asha! Badala yake ninawapa changamoto kwamba katika maisha silaha mnayopaswa kuing'angania ni elimu peke yake na si vibaka wa mitaani," alisema Dk Luoga. "Acheni kudanganywa na mafataki ambao ni matapeli na ambao huweza kuwapotezea dira ya maisha, badala yake msome kwa bidii, kwa ajili ya mafanikio ya maisha yenu." Dk Luoga alisema kuwa vijana wengi, hasa wanafunzi wamekuwa wakirubuniwa kutokana na kushindwa kustahimili tamaa za maisha na kuamua kujiingiza kwa vijana wa mitaani ambao aliwaelezea kuwa hawana sera.

Waziri huyo, ambaye ni sura mpya katika baraza lililoundwa hivi karibuni na Rais Jakaya Kikwete, alikumbushia taaluma yake ya ualimu kwa kutumia kalamu na kuwafundisha washiriki wa kongamano hilo masuala ya maisha na athari za ukimwi kwa vijana, huku akijitangza kuwa naye ni mtoto wa mkulima. "Ni bora kuacha kabisa na kuamua kusubiri kwani kwa kuwa mahusiano katika masomo ni hatari... badala yake mzidi kumuomba Mungu na kuwa waadilifu," alisisitiza "Leo hii, ninamshukulu Mungu kwa Elimu aliyonipa kwa sababu alinijua mimi ni mtoto wa mkulima, hivyo niliamua kutochezea maisha yangu kiholela. "Hapa unavyoniona, kama waziri nina fedha za kutosha; gari la kifahari ninalo ehe! Unadhani nikitaka kuwa na mafataki hata watano, nitashindwa?" "Nikiamua kuchakachua wanaume hata watano, naweza kwa sababu uwezo ninao na fedha ninayo.

Lakini sioni faida yeyote badala yake ni kujitumbikiza mahali ambapo ni hatari zaidi," alisema. "Cha msingi hapa ni kuhakikisha mnajenga maadili mema mnapokuwa shuleni na nyumbani ili kuepuka kurubuniwa na kupoteza mwelekeo wa elimu mliopata." Naye mtaalamu wa ushauri wa afya katika kamati ya vijana, Dk Telesphoy Kyaruzi alisema tatizo kubwa linalowapelekea vijana wengi kujiingiza katika ngono zembe na kupata maambukizi ni uchumi mbovu. Dk Kyaruzi alisema kwa kuliona hilo, wanaiomba serikali kuhakikisha inatoa mikopo kwa vijana ili kuwasaidia waweze kujiendesha na kuepuka vishawishi.

ushuhuda mzuri coz unatoa picha halisi ya maisha yetu ,na yeye kama mtanzania mwanamke alipitia yanayofanywa na wengi vyuoni, sasa tatizo lake nini hapo hebu someni kwa makini mmpate ujumbe mi naona ni ushauri mzuri tu, au kwa sababu ni waziri, angeutoa mtu wa kawaida kwa lengo lilelile la kuisa jamii ungechukuliwa hivyo mlivyouchukulia, acheni hayo mambo wandugu
 
ushuhuda mzuri coz unatoa picha halisi ya maisha yetu ,na yeye kama mtanzania mwanamke alipitia yanayofanywa na wengi vyuoni, sasa tatizo lake nini hapo hebu someni kwa makini mmpate ujumbe mi naona ni ushauri mzuri tu, au kwa sababu ni waziri, angeutoa mtu wa kawaida kwa lengo lilelile la kuisa jamii ungechukuliwa hivyo mlivyouchukulia, acheni hayo mambo wandugu

umesoma tu hujatafakari ndugu yangu.................any way............. ukitafakari zaidi utagundua kuwa anawahamasisha badala ya kuwaonya................
 
Waziri Luoga alilazimika kushirikisha vijana hao kuhusu maisha yake kutaka kuwaonyesha alivyomudu kuvumilia na kupambana na maisha hadi kufikia mafanikio aliyoyapata sasa, akisema badala yake sasa anaweza "kuchakachua" hadi wanaume watano lakini "haoni sababu" na kuwataka wanafunzi kuepuka watu wenye tabia za kifataki kwa kuwa wanaweza kuwaharibia mwelekeo wa maisha.

nitafakarie hiyo paragrah na unieleze umehamasishwa kudo au otherwise.........................,eti bwana akili kichwani,hebu twende paragraph kwa paragraph, stress iwe ktk mstari uliokoza tafadhali
 
Waziri Luoga alilazimika kushirikisha vijana hao kuhusu maisha yake kutaka kuwaonyesha alivyomudu kuvumilia na kupambana na maisha hadi kufikia mafanikio aliyoyapata sasa, akisema badala yake sasa anaweza "kuchakachua" hadi wanaume watano lakini "haoni sababu" na kuwataka wanafunzi kuepuka watu wenye tabia za kifataki kwa kuwa wanaweza kuwaharibia mwelekeo wa maisha.

nitafakarie hiyo paragrah na unieleze umehamasishwa kudo au otherwise.........................,eti bwana akili kichwani,hebu twende paragraph kwa paragraph, stress iwe ktk mstari uliokoza tafadhali

angalia hapo penye colou na bold............. kwa anayejua maana ya kushawishi hawezi kuletaswali zaidi........... anyway, kwa kukusaidia.... sasa anaweza lakini haoni sababu kwa kuwa ni waziri........... alivokuwa chuoi aliweza na aliona sababu na "alichakachua" akafanikiwa kusoma............ ndiyo lugha iliyo nyuma ya maneno hayo na utaipata "ukitafsir"i, sio"ukisoma".............
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom