Karot
JF-Expert Member
- Mar 6, 2017
- 1,159
- 1,309
Tuna Sheha kwa upande wa Bara mnamwita Mwenyekiti anatuuzi sana wananchi kwa kulazimisha michango ambayo haistahili kwakweli. Zanzibar tuna masheha wengi lakini sijawahi kuona vituko anavovinya huyu wa mtaani kwangu.
Habari kamili....
Ni sheha ambae aliamua kupitisha michango kwa wananchi kwa kisingizio cha kwamba anatengeneza ulinzi shirikishi kitu ambacho wanamtaa wote hawakuafiki. Na kitu kilichofanya wasikubali kuchanga ni kwamba huyu sheha wanajua vyema anapenda pesa kuliko kuwahudumia watu wake.
Pia hawezi kukuhudumia huduma yoyote hata kama ni ya bure bila kukudai rushwa. Na pia ulinzi huo hauleti faida kwa maana hakuna hata mmoja anaepiga doria sana sana pesa zinatakiwa kuliwa tu.
Na ndomaana wananchi wa shehia yake walikataa kutoa michango hiyo.
Na kibaya zaidi tangia juzi anamtuma mtoto wake apitie michango baada ya kumjibu sina pesa nimejibiwa sitakuja kupewa huduma yoyote pindi nitakapokuja kuwa na shida ya ofisi yake na ndo maana nikasema nasubiri nije niende aninyime huduma nimpeleke kwa Mkuu wa Wilaya akajibie hili.
Mwisho.. Naomba kufahamishwa au kupewa mawazo nimefanya kosa kutochangia? Ilihali mwenyewe naweza kulinda nyumbani kwangu?
Habari kamili....
Ni sheha ambae aliamua kupitisha michango kwa wananchi kwa kisingizio cha kwamba anatengeneza ulinzi shirikishi kitu ambacho wanamtaa wote hawakuafiki. Na kitu kilichofanya wasikubali kuchanga ni kwamba huyu sheha wanajua vyema anapenda pesa kuliko kuwahudumia watu wake.
Pia hawezi kukuhudumia huduma yoyote hata kama ni ya bure bila kukudai rushwa. Na pia ulinzi huo hauleti faida kwa maana hakuna hata mmoja anaepiga doria sana sana pesa zinatakiwa kuliwa tu.
Na ndomaana wananchi wa shehia yake walikataa kutoa michango hiyo.
Na kibaya zaidi tangia juzi anamtuma mtoto wake apitie michango baada ya kumjibu sina pesa nimejibiwa sitakuja kupewa huduma yoyote pindi nitakapokuja kuwa na shida ya ofisi yake na ndo maana nikasema nasubiri nije niende aninyime huduma nimpeleke kwa Mkuu wa Wilaya akajibie hili.
Mwisho.. Naomba kufahamishwa au kupewa mawazo nimefanya kosa kutochangia? Ilihali mwenyewe naweza kulinda nyumbani kwangu?