Makanyaga
JF-Expert Member
- Sep 28, 2007
- 10,318
- 6,846
walokole wengi sana ni wachawi..... (MLOKOLE NI MTU ANAYEJIFANYA ANAJUA MAMBO YA ROHONI SANA)
Na hili nalo niachie nilifanyie utafiti, you possibly could be right or wrong siwezi ku-rule out mda huu!. Wanaweza kuwa siyo, except kwamba "uchawi" ni portion tu ya kile kilichochakachuliwa kutoka kwenye knowledge sahihi ya Mungu. Kumbuka kuwa Shetani alikuwa Malaika Mkuu Mbinguni, na alikuwa Special kwa ajili ya Sifa na Ibada.Malaika Gabriel ambaye yeye yupo ana-operate mpaka muda huu, ni Special kwa ajili ya kuleta jumbe kutoka Mbinguni kuja Duniani, na malaika Mikaeli, yeye ni Specia kwa ajili ya Vita.
Kwa ufupi tu anachofanya Shetani tuseme ni kama mtu umemfundisha kupika ugali nyumbani ili watoto wako wale. Huyo mtu akaasi akawa anapika ugali kama kawaida halafu kwenye maji ya kusongea ugali anaongeza sumu ya panya. Knowlegde yote wanayotumia wachawi imetokana na knowledge aliyoipata Shetani kutoka kwa Mungu, halafu akaamua kuichakachua. Ndiyo maana ukikuta kwa mfano, mtu mchawi anayejua pia maandiko matakatifu, huyo ni mbaya zaidi kuliko Mganga wa Kienyeji au mchawi anayeogopwa Bagamoyo nzima, ila ambaye hajui chochote kuhusu Biblia. Shetani anachofanya ni kutumia knowledge ya Mungu halafu anaongeza manuio ambayo ni negative kwa ajili ya kuleta madhara, au ana-negate neno la maandiko matakatifu kwenye Biblia. Kwa mfano, Mungu aliwaambia Adam na Hawa kuwa wakila tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya WATAKUFA HAKIKA. Shetani yeye akaja aka-negate neno hilo na kuwaambia HAKIKA HAWATAKUFA, na aliya-reverse maneno hayo. Neno alilotamka Mungu mwisho, yeye ndilo aliloanza nalo, na kumalizia na lile aliloanza nalo Mungu.
Kwa uhakika tu ni kwamba ukijikita zaidi kwenye kumtafuta Mungu na njia zako zikawa zimenyooka na ukawa huna mchanganyiko wa kitu kingine chochote kile isipokuwa Mungu peke yake, utamjua kila mtu alivyo, hakuna atakayeweza kujificha kwako, na possibly kwa mtu ambaye hajui maandiko matakatifu, anaweza akakuona wewe ni mchawi zaidi. Could be Walokole wanaonekana kuwa ni wachawi kutokana na fact hii. Hata hivyo sikubishii hoja yako, given time nitakuja kujua ukweli wa claims unazojaribu ku-raise, kama ziko sahihi ama la! Ubarikiwe sana