khamis kilo
JF-Expert Member
- May 23, 2016
- 1,049
- 1,192
Rafael Caro Quintero
Achana na Pablo Escobar, kuna huyu gwiji mwingine wa kuuza madawa ya kulevya kutoka Mexico, huyu anaitwa Rafael Caro Quinteto maarufu kama "Narco of Narcos" au ukipenda muite "Chapo" (Jina la Chapo lilianzia kwake). Alizaliwa October 3 1952 huko Badiraguato, Sinaloa nchini Mexico.
Rafa alipokuwa mdogo taratibu alianza kupanda zao la bangi kwenye shamba la kaka yake Jorge Luis. Sio chini ya miaka 5 na yeye akafanikiwa kununua mashamba kadhaa na kuanza kujikita zaidi kwenye biashara hiyo.
Lakini baadae serikali ya huko Sinaloa ilifanya msako mkali na kuchoma mashamba yote ya bangi huko Sinaloa. Hali hiyo ilipelekea Rafa pamoja na washirika wenzake akiwemo Miguel Angel Felix Gallardo kuhamia kwenye jimbo la Guadalajara ili kuendeleza biashara yao. Baada ya kufika huko kazi ya kupata connection za madoni mbalimbali wa biashara hiyo ilikuwa chini ya usimamizi wa mtaalamu Miguel Gallardo, huku Rafa yeye akijikita zaidi kwenye kilimo cha bangi.
Rafael alifanikiwa kupata mahali ambapo palikuwa na asili ya ukame na ni mbali kwa maaskari kupadhania wala kufika, eneo lililokuwa na zaidi ya hekari 2500. Na eneo lote hilo likajaa kwa zao hilo la bangi!!! Wakishirikiana pamoja na Gallardo wakaanzisha kundi lao la Guadalajara Cartel huku wakisambaza mihadarati Mexico yote mpaka nchini Marekani!
*Hii ni sehemu ya kwanza, ngoja sehemu ya pili*
Achana na Pablo Escobar, kuna huyu gwiji mwingine wa kuuza madawa ya kulevya kutoka Mexico, huyu anaitwa Rafael Caro Quinteto maarufu kama "Narco of Narcos" au ukipenda muite "Chapo" (Jina la Chapo lilianzia kwake). Alizaliwa October 3 1952 huko Badiraguato, Sinaloa nchini Mexico.
Rafa alipokuwa mdogo taratibu alianza kupanda zao la bangi kwenye shamba la kaka yake Jorge Luis. Sio chini ya miaka 5 na yeye akafanikiwa kununua mashamba kadhaa na kuanza kujikita zaidi kwenye biashara hiyo.
Lakini baadae serikali ya huko Sinaloa ilifanya msako mkali na kuchoma mashamba yote ya bangi huko Sinaloa. Hali hiyo ilipelekea Rafa pamoja na washirika wenzake akiwemo Miguel Angel Felix Gallardo kuhamia kwenye jimbo la Guadalajara ili kuendeleza biashara yao. Baada ya kufika huko kazi ya kupata connection za madoni mbalimbali wa biashara hiyo ilikuwa chini ya usimamizi wa mtaalamu Miguel Gallardo, huku Rafa yeye akijikita zaidi kwenye kilimo cha bangi.
Rafael alifanikiwa kupata mahali ambapo palikuwa na asili ya ukame na ni mbali kwa maaskari kupadhania wala kufika, eneo lililokuwa na zaidi ya hekari 2500. Na eneo lote hilo likajaa kwa zao hilo la bangi!!! Wakishirikiana pamoja na Gallardo wakaanzisha kundi lao la Guadalajara Cartel huku wakisambaza mihadarati Mexico yote mpaka nchini Marekani!
*Hii ni sehemu ya kwanza, ngoja sehemu ya pili*