Huyu ndiye Padri Privatus Mutekanga Karugendo (1956-2021)

Katekista alinifundisha nisifiche dhambi hata moja maana ungamo langu halitakubalika, pia aliniambia nitaje dhambi kwa majina yake...kuiba, kuzini, nk na nitaje mara ngapi, lini na wapi nilitenda dhambi hizo, ....pia mkuu huwa tunaungama na dhambi zote TULIZOZISAHAU, sio kujisahaulisha!
"...na wote mtakaowafungulia (wasamehe) duniani pia watakuwa wamefinguliwa mbinguni...."
Imani hizi jamani!
 
Nilichojifunza hapa ni kwamba, Askofu Niguwemizi roho yake inaendeshwa na shetani himself and yet anavaa joho la Uaskofu

Pia nimejifunza kwamba Kanisa Katoliki halimtumaini Mungu wa KWELI bali binadamu anayeitwa Papa.

Tatu nimegundua kwamba Kanisa Katoliki hujivika joho la demokrasia nchi mbalimbali wakati ndani ya Kanisa hilo hawaitambui demokrasia

Nne. Hawa watoto wa mapadri tunaoishi nao mitaani hatima yao ipoje kupitia misimamo ya kipagani ya Kanisa?
Naona kommenti yako imetawaliwa na emotion za chuki ndio maana umeshindwa kuzitetea.Shetani mkubwa ushindwe kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareth.
 
Mapadri wepi hao mkuu?? Hawa hawa wanaoabudu sanamu na kutumia jina la wanaemwita BIKIRA Maria wakati sio BIKIRA?? You can't be serious mkuu
KWELI wewe ni matanga maana ni kichwani inaonyesha kumejaa funza.Hivi Bikira Maria sio Bikira kweli?. Protestant watu wa ajabu sana, Hivi unawezaje kusema kwamba unampenda na kumheshimu Yesu Kristo wakati mama yake unamtukana?.Hivi hujui kwa kumtukana Mama yake unakuwa unashusha hadhi na daraja la Kristo??.
 
Katekista alinifundisha nisifiche dhambi hata moja maana ungamo langu halitakubalika, pia aliniambia nitaje dhambi kwa majina yake...kuiba, kuzini, nk na nitaje mara ngapi, lini na wapi nilitenda dhambi hizo, ....pia mkuu huwa tunaungama na dhambi zote TULIZOZISAHAU, sio kujisahaulisha!
"...na wote mtakaowafungulia (wasamehe) duniani pia watakuwa wamefinguliwa mbinguni...."
Imani hizi jamani!
Ni kweli, tafsida inaungana na dhamiri ndani ya moyo wako. Fungula vizuri tu kama una amani na Padre husika uangamishae dhambi, bado nae ni mwanadamu
 
Naona kommenti yako imetawaliwa na emotion za chuki ndio maana umeshindwa kuzitetea.Shetani mkubwa ushindwe kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareth.
Yesu Kristo aliwaambia ukweli Mafarisayo na makuhani wao kuwa wanafanana na makaburi yaliyopambwa nje kwa nakshi wakati ndani ni mifupa mitupu.

Soma historia ya kanisa lako uujue ukweli kisha ishi ukifahamu Mungu hayupo kwenye ibada ya sanamu na hafungamanishwi na upinga Kristo uliosimikwa na Roma.

Ukimsoma vizuri marehemu Privatus Karugendo utagundua kwamba ili uweze kukua kihuduma ndani ya Katoliki ni lazima uee mnafiki na siyo mkweli
 
Nilichojifunza hapa ni kwamba, Askofu Niguwemizi roho yake inaendeshwa na shetani himself and yet anavaa joho la Uaskofu

Pia nimejifunza kwamba Kanisa Katoliki halimtumaini Mungu wa KWELI bali binadamu anayeitwa Papa.

Tatu nimegundua kwamba Kanisa Katoliki hujivika joho la demokrasia nchi mbalimbali wakati ndani ya Kanisa hilo hawaitambui demokrasia

Nne. Hawa watoto wa mapadri tunaoishi nao mitaani hatima yao ipoje kupitia misimamo ya kipagani ya Kanisa?
Usimchukie Niwemugizi kwa kuenenda na sheria za Kanisa, ukikosea lazima uadhibiwe, Kanisa kulea uozo wa aina hiyo ndio utakuwa mwanzo wa kupoteza thamani yake.

Kuhusu Kanisa Katoliki kutomtumaini mungu wa kweli bali Papa huo ni mtazamo wako, kwanza huyo "mungu" wako hata simjui, Papa ndie kiongozi wa Katoliki ulimwenguni, mbinguni yupo Yesu Kristo, hii taka usitake is up to you.

- Zaidi, Yesu Kristo wakati anawatumia mitume wake kina Paulo, Mathayo, Luka, Marko, na wengine, hakuwabeba na wake zao, sasa wewe na huyo "mungu" wako wa kweli anaekutaka uende na mkeo msalimie ukifika.

Kuhusu demokrasia ya kukaa chini na wakosefu waliojua dhahiri kuwa kile walichofanya walikuwa wanakiuka viapo vyao, tena wakiwa na akili timamu, huu ni ujinga ambao Katoliki haupewi nafasi kabisa, kama alishindwa kuumiliki mwili wake vyema aende kule wanaporuhusu hayo mambo, Katoliki halitaki kelele.

- Kanisa Katoliki siku zote is all about discipline, hata wanafunzi wanaosoma kwenye shule zao waulize nini kinachowafanya wawe na ufaulu mzuri watakwambia masista hawataki kuona ujinga mdogo hata wa nusu centimeter tu.

Hao watoto wa mapadri mitaani wapelekeni kwa baba zao, wao ndio watajua chakufanya, kama uliwaona mapadri wakilala na hao wanawake au kama unafanya biashara ya guest peleka ushahidi jimboni.
 
Yesu Kristo aliwaambia ukweli Mafarisayo na makuhani wao kuwa wanafanana na makaburi yaliyopambwa nje kwa nakshi wakati ndani ni mifupa mitupu.

Soma historia ya kanisa lako uujue ukweli kisha ishi ukifahamu Mungu hayupo kwenye ibada ya sanamu na hafungamanishwi na upinga Kristo uliosimikwa na Roma.

Ukimsoma vizuri marehemu Privatus Karugendo utagundua kwamba ili uweze kukua kihuduma ndani ya Katoliki ni lazima uee mnafiki na siyo mkweli
Na vipi kuhusu Kanisa lako??.
 
Wewe unajua niwemugizi amezini na wake za watu wangapi?,unajua kuwa niwemugizi ana watoto?sasa nani kavunja hiyo amri ya useja?
Weka ushahidi hapa usilete story za mtaani, hayo maneno matupu hata kwenye kanga yapo.
 
Yesu Kristo aliwaambia ukweli Mafarisayo na makuhani wao kuwa wanafanana na makaburi yaliyopambwa nje kwa nakshi wakati ndani ni mifupa mitupu.

Soma historia ya kanisa lako uujue ukweli kisha ishi ukifahamu Mungu hayupo kwenye ibada ya sanamu na hafungamanishwi na upinga Kristo uliosimikwa na Roma.

Ukimsoma vizuri marehemu Privatus Karugendo utagundua kwamba ili uweze kukua kihuduma ndani ya Katoliki ni lazima uee mnafiki na siyo mkweli
Ibada ya sanamu maana yake ni nini? nijibu kulingana na maandiko, usilete story hapa, unaonekana mtoto usieelewa chochote, mihemko tu.

Unazungumzia unafiki kama vile haukuhusu na hii "HAKI" unayojidai nayo hapa duniani, kama hilo Kanisa Katoliki lina "DHAMBI" ndio uliache kwani Yesu alikuja kwa ajili yake, nyie wajuaji pambaneni na hali zenu.

- Mathayo 23:28 inawaonya watu wa aina yako mnaojidai kwa nje mna haki wakati ndani mmejaa maovu ya kila aina.

Mwisho, hiyo historia ya Kanisa Katoliki aliandika nani mpaka iaminiwe na kila mmoja? na huyo Karugendo kama ndio alikuwa mwalimu wako ningekuona una akili kama ungemuuliza kwanini yeye alikimbilia wanawake wakati si Yesu, wala wanafunzi wake, wala Kanisa aliloapa kulitumikia mwanzo, waliokuwa na hao wanawake?
 
Karugendo alikiuka kiapo cha useja kwa kuwa na mahusiano na mwanamke nje akijua fika kufanya hivyo lilikuwa ni kosa, usifanye Askofu Niwemugizi aonekane mbaya kwa kumchukulia hatua mtu ambaye alikiuka kiapo hiki muhimu.

Mtu akikosea lazima aadhibiwe kwa kosa lake, ni adhabu ya aina gani atakayopewa huo ni uamuzi wa kiongozi wake, na zaidi kwa nafasi aliyokuwa nayo alionesha udhaifu dhidi ya imani yake, na pia zaidi, kwa wale waliokuwa waumini wake, huyu kama angesamehewa angeweza kuweka "precedence" mbaya kwa Kanisa Katoliki.

Kwangu nasimama na uamuzi wa Askofu Niwemugizi kumvua cheo cha upadri, lakini pia, nilikuwa napenda nipate wasaa wa kukutana nae nimuulize kwanini alikuwa bado anatumia jina la "Padri" kama nilivyokuwa nikisoma makala zake kwenye magazeti mbalimbali licha ya kuwa alishavuliwa hicho cheo na kanisa?
Padre ni neno la kilatini lenye maana yake baba au father au papa. Pia Nyerere aliitwa Mwalimu MAISHA yake yote,ingawa Dr. Slaa hapendi kutumia Jina hilo japo udaktari wake ni wa Canon Law.
 
Padre ni neno la kilatini lenye maana yake baba au father au papa. Pia Nyerere aliitwa Mwalimu MAISHA yake yote,ingawa Dr. Slaa hapendi kutumia Jina hilo japo udaktari wake ni wa Canon Law.
Baba, au Father, au Papa kwa muktadha wa Kanisa Katoliki limanaanisha waumini ndio wanamuita hivyo Padre, sasa Karugendo licha ya kufukuzwa bado akawa analitumia hilo jina (Padre), alikuwa "Baba" wa nani? au wale watoto wake aliozaa na mke wake nyumbani?

Anaonekana alikuwa mjuaji fulani.
 
Umenena mkuu. Katoliki kuna tatizo la autocracy Sana.
Hii kesi nimeanza kuisikia tangu nikiwa seminari ndg.

Nimefuatilia pande zote mbili na kusoma baadhi ya machapisho yao kwenye magazeti mbalimbali. Zaidi zaidi nimesikia hadi maoni ya baadhi ya members of clergy kuhusu hii issue. Kiufupi bado ilikua na mixed feelings sana.

Unaposema nmesikiliza upande mmoja unakosea sana.

Anyway hio ni view yangu khs hio issue, naheshimu view yako pia.

Ila nikuulize swali, kwa nn kesi ilirushwa step?, kwa nn the late hakusikilizwa kwa namna inavyopaswa?, Barua yake ya kuomba idhini ya kufungwa ndoa iliandikwa na nani na kupelekwa kwa balozi bila the late kujua?

Na kumbuka Papa kiukweli hatoi hukumu, yeye anaidhinisha tu hukumu, coz kama unajua structure ya katoliki nadhan unafahamu kwamba majimbo yanaruhusiwa kujiendesha independently kwa baadhi ya mambo, then wanaomba tu idhinisho la papa. Na papa aliidhinisha kitu ambacho amepelekewa tu na hao wasaidizi wake, hivyo kama ilitumiwa chuki basi Fr Karugendo alikua hana cha kufanya ila kusubiri tu hukumu coz wakubwa ndio wanaamua Papa aone nini na nini?

Kama nilivyosema sina authority yyt kujudge hii issue ila kwa view yangu hii ilikua ni unfair play.

Kama Fr Karugendo alitolewa kwa kosa la adultery basi na bishop ilibidi awe responsible, au watoe ushahidi kwamba nje ya kitubio cha Fr Karugendo nini zaidi kilifanya authority ijue kama Fr Karugendo alifanya hilo kosa?

Double standards, Autocracy ndio matatizo huko RC.
 
Alikuwa na makala gazeti la Rai zilikuwa nzuri Sana kumbe ni padri ndio maana zilivuta hisia
 
Ibada ya sanamu maana yake ni nini? nijibu kulingana na maandiko, usilete story hapa, unaonekana mtoto usieelewa chochote, mihemko tu.

Unazungumzia unafiki kama vile haukuhusu na hii "HAKI" unayojidai nayo hapa duniani, kama hilo Kanisa Katoliki lina "DHAMBI" ndio uliache kwani Yesu alikuja kwa ajili yake, nyie wajuaji pambaneni na hali zenu.

- Mathayo 23:28 inawaonya watu wa aina yako mnaojidai kwa nje mna haki wakati ndani mmejaa maovu ya kila aina.

Mwisho, hiyo historia ya Kanisa Katoliki aliandika nani mpaka iaminiwe na kila mmoja? na huyo Karugendo kama ndio alikuwa mwalimu wako ningekuona una akili kama ungemuuliza kwanini yeye alikimbilia wanawake wakati si Yesu, wala wanafunzi wake, wala Kanisa aliloapa kulitumikia mwanzo, waliokuwa na hao wanawake?
Petro alikuwa na mkewe.

Pia neno Askofu kwenye Agano Jipya anatajwa kama Baba mwangalizi. Mtu mwenye mke wake.....

Ni Paulo pekee ambaye hakuwa na uwezo wa kuwa na mwanamke.

Turudi kwenye Kanisa. Je mnavyoabudu sanamu ni agizo kutoka kwa nani?

Nani aliwaambia kwamba Yesu hakuwa na wadogo zake tumbo moja?

Hakuna mahala ambapo Yesu aliagiza kwamba ukitaka hitaji kwa Mungu basi uombe kwa jina lingine zaidi ya Yesu.

Yesu ni line ya Daudi lakini kumbuka Maria siyo line ya Daudi.

Ninamuomba Roho Mtakatifu akufungue ufahamu wako uelewe haya ninayokueleza. Kumbuka Yesu alisema, njia ya Mbinguni wanaoiona ni wachache na wachache zaidi ndo wanaoipita. Sasa jiangalie vizuri kwenye kujifarijia kwenu kwa bandia mnajikuta mnaingia motoni kwa maelfu.

Yesu alisema ukishakufa unaenda peponi au jehanamu. Lakini wapagani wakaja na kitu kinaitwa toharani.

Shetani ameweka kiti chake pale Vatican ndo maana katoliki na umafia havijaachana.

Tafuta kweli ya Mungu, acha zako hizo
 
Petro alikuwa na mkewe.

Pia neno Askofu kwenye Agano Jipya anatajwa kama Baba mwangalizi. Mtu mwenye mke wake.....

Ni Paulo pekee ambaye hakuwa na uwezo wa kuwa na mwanamke.

Turudi kwenye Kanisa. Je mnavyoabudu sanamu ni agizo kutoka kwa nani?

Nani aliwaambia kwamba Yesu hakuwa na wadogo zake tumbo moja?

Hakuna mahala ambapo Yesu aliagiza kwamba ukitaka hitaji kwa Mungu basi uombe kwa jina lingine zaidi ya Yesu.

Yesu ni line ya Daudi lakini kumbuka Maria siyo line ya Daudi.

Ninamuomba Roho Mtakatifu akufungue ufahamu wako uelewe haya ninayokueleza. Kumbuka Yesu alisema, njia ya Mbinguni wanaoiona ni wachache na wachache zaidi ndo wanaoipita. Sasa jiangalie vizuri kwenye kujifarijia kwenu kwa bandia mnajikuta mnaingia motoni kwa maelfu.

Yesu alisema ukishakufa unaenda peponi au jehanamu. Lakini wapagani wakaja na kitu kinaitwa toharani.

Shetani ameweka kiti chake pale Vatican ndo maana katoliki na umafia havijaachana.

Tafuta kweli ya Mungu, acha zako hizo
Nimekwambia nipe maana ya "kuabudu sanamu" kulingana na maandiko ya Agano jipya, bado nasubiri jibu hapa.

Petro na hao wengine unaosema walikuwa na wake sawa, walikuwa nao, lakini hawakwenda na hao wake zao kutangaza injili, Petro anamwambia Yesu tunaacha familia zetu na vyote huko tuendako tutapata nini, Yesu anawajibu kuna uzima wa milele (ukitaka mstari wa andiko utapata).

Askofu kuitwa "Baba" kulingana na maandiko ya Agano Jipya kama unavyosema coz ana watoto unakosea, yule ni "Baba" wa kiroho, sio Baba wa mwilini kama unavyofikiria, Biblia inazungumzia vya rohoni sio mwilini, haya mawazo potofu yamekujaa ndio maana unaona kuzaa au kuwa na mwanamke kwako ni kila kitu, wacha haya mawazo ya mwilini utaangamia.

Yesu anawaaga wanafunzi wake baada ya kukufuka, anawaambia "pokeeni roho mtakatifu mtakaowaondolea dhambi wataondolewa, na mtakaowafungia watafungiwa" hapa Yesu alikaimisha mamlaka yake kwa wanafunzi wake ambao ndio hao mapadri wa leo, ukitaka sawa ukigoma sawa pia.

Unasema shetani ameweka kiti chake pale Vatican; nakuhurumia sana, maandiko yanasema "usihukumu usije kuhukumiwa", mtu wa aina yako ndio unaniombea roho mtakatifu anifungumie mimi!, wewe kipofu huwezi kunifundisha mimi sio kipofu kama wewe, Yesu alisema kipofu hawezi kumuongoza kipofu mwenzie wote watatumbukia, poleni na Karugendo wako.

Soma biblia itafsiri uielewe, kama hujaelewa mahali tafuta mtu umuulize, ukikurupuka ndio kichwa kinakujaa unajiona unajua zaidi ya wote, una "HAKI" kushinda wengine, mpaka unahukumu, utaangamia.
 
Hukumu ya kuvuliwa daraja la upadre kwa Karugendo haikunishangaza, alikuwa anaandika sana kupinga msimamo wa mwajiri wake kuhusu matumizi ya kondomu.

Naamini hakuonewa, nilimsoma na kusikia misimamo yake alipohojiwa na redio moja ya kimataifa.

Vv
Ni kweli mkuu, maandiko mengi ya huyu padri yalikuwa na utata mwingi kiasi kwamba baadhi yetu tulikuwa tukishangaa padre kuandika vile.
 
Back
Top Bottom