Huyu ndiye Nicholas Mgaya - Katibu Mkuu TUCTA

Mheshimiwa Rais hongera kwa kutambua udhaifu wa watanzania na kuwa very smart katika kutumia udhaifu huo.
GS unampongeza raisi kwa lipi? goli la kuotea??
Mgaya hajamuangusha yeyote kwa kuahirisha mgomo. Tuseme TUCTA wametumia busara kufanya hivyo kwa sababu ingelikuwa ni loosing war. Nguvu ya raisi wa TZ inajulikana kikatiba na lolote ambalo lingetokea angekua na uwezo wa kuwatupia lawama TUCTA hivyo bora hiyo subira izidi kuwatia hasira watanzania ili siku wakisema mgomo na wawe tayari kwa hizo risasi za moto.

Kwa ile hotuba ya raisi tayari alishawagawa wafanyakazi na kumtwisha Mgaya mzigo kwamba yeye ndiye anashinikiza mgomo kwa kutumwa na wapinzani wa JK. Cha maana wafanyakazi tuzidi kushikamana na kuendeleza mapambano kwa njia zote, kelele, mahakama, vitisho na mkakati wa mgomo mwingine wenye ufanisi zaidi.
 
Namsifu Mgaya nawasifu wafanyakazi na naisifu TUCTA,
Huu ni mwanzo mzuri nia yako mfanyakazi si kugoma bali kuonyesha hali halisi ya mfanyakazi kiungwana. Usifikiri hakuna asiyejua athari ya mgomo. Mfanyakazi amekaa katika hali hii (ya mshahara mdogo, kodi kubwa, na mafao madogo ya uzeeni) kwa muda mrefu. Hali ya siasa na matukio ya ubadhirifu(ufisadi) anaiona na haishughulikiwi wakati yeye akiendelea kunyanyasika. Anendelea kupata msukumo na chama kinajaribu kumsaidia, NATUMAIMINI siku moja ataota mbawa
(A point of no return) hatajali kiasi hiki kidogo apatacho na kusema bora nikose hiki kidogo na hakuna haja ya kuishi. Mungu apishie mbali!
 
Mhh!.,huyu Mgaya amekuwa maarufu kweli, akigombea ubunge anaweza kupata huyu.

Like president like citizens (Ndiyo hiyo ajenda aliyokuwa anasema mkulu unayotuambia au?)

Binafsi naona TUCTA wamerudi nyuma kupisha nafasi ya majadiliano yaliyopangwa tarehe 08.05.10. Ni issue ya kisheria zaidi maana unaingia kwenye mgomo baada ya kikao cha maridhiano kutokupata muafaka ten unatangaza mgogoro. Bado twende mbele turudi nyuma bado sioni essence ya president kuwasuta tukta kwa wale wazee katika issue ya wafanyakazi angetumia muda huo kuongea na TUCTA nadhani angeonyesha anajali zaidi.
 
GS unampongeza raisi kwa lipi? goli la kuotea??
Mgaya hajamuangusha yeyote kwa kuahirisha mgomo. Tuseme TUCTA wametumia busara kufanya hivyo kwa sababu ingelikuwa ni loosing war. Nguvu ya raisi wa TZ inajulikana kikatiba na lolote ambalo lingetokea angekua na uwezo wa kuwatupia lawama TUCTA hivyo bora hiyo subira izidi kuwatia hasira watanzania ili siku wakisema mgomo na wawe tayari kwa hizo risasi za moto.

Kwa ile hotuba ya raisi tayari alishawagawa wafanyakazi na kumtwisha Mgaya mzigo kwamba yeye ndiye anashinikiza mgomo kwa kutumwa na wapinzani wa JK. Cha maana wafanyakazi tuzidi kushikamana na kuendeleza mapambano kwa njia zote, kelele, mahakama, vitisho na mkakati wa mgomo mwingine wenye ufanisi zaidi.

Nimemsifu Rais kwa kuwa mjanja kwa kaumua kumshambulia Ngaya badala ya TUCTA kwa kuwa alijua akifanya hivyo lengo lake litafanikiwa na kusitisha mgomo.Ni kweli kikatiba Rais anamamlaka ya kuamua chochote na ni kweli mgomo ungefanyika lawama zingekwenda kwa TUCTA,kwahiyo unakubaliana nami kuwa TUCTA walikuwa wanatishia mtu mzima nyau?
 
WAMEFANYA VIZURI KUAHIRISHA MGOMO.TENA IKIWEZEKANA WAUFUTE KABISA.WAKAE CHINI WAJADILIANE NA SERIKALI HADI KIELEWEKE. NANI ANAPENDA MGOMO?TENA MGOMO WA NCHI NZIMA. FIKIRI SANA KILA MFANYAKAZI AGOME.ASIENDE KAZINI.SIJUI KAMA WENZANGU MLILIWAZA HILI. HALI ITAKUWAJE?
FIKIRI TENA.HALI ITAKUWAJE?UNAJUA MAANA YAKE HAKUNA HUDUMA YOYOTE,HAKUNA BIDHAA YOYOTE!1!!!!!!!!!!!!!!!!. CHA AJABU SIKUONA MTANZANIA YEYOTE AKIJIANDAA KWA JAMBO LOLOTE ILI ASIPATE SHIDA WAKATI WA MGOMO.BINAFSI SIPENDI MIGOMO.MADHARA NI MAKUBWA KULIKO FAIDA.
Haya ndio mawazo yangu.
 
Leo nimeshangazwa sana baada ya kusikia eti TUCTA wamesitisha mgomo kwa muda. Natambua kwamba maneno ya Rais yalimtisha Mgaya akaamua kurudi nyuma. Rais was very clever and strategc alivyoamua kumshambulia Mgaya as if yeye ndio TUCTA pekee. Rais alitambua kabisa kwamba watanzania tu waoga na tunafuata mkumbo tu

Mkuu inawezekana pia kuwa pale shambani mwa bibi waliogeza hisia katika hotuba zao. Inawezekana pia kuwa waliahidiana kukutana tena tarehe nane kwa ajili ya mazungumzo zaidi, so wangejibana wao kama wangeamua kugoma. Tusubiri hiyo tarehe 8
 
mkuu inawezekana pia kuwa pale shambani mwa bibi waliogeza hisia katika hotuba zao. Inawezekana pia kuwa waliahidiana kukutana tena tarehe nane kwa ajili ya mazungumzo zaidi, so wangejibana wao kama wangeamua kugoma. Tusubiri hiyo tarehe 8
amini usiamini hakuna mgomo utakaokuwepo tena..........ndio imetoka hiyo.
 
mgaya bwana ndo mwanaume
ila sema tu jk alitumia ubabe wake ila ngoja hiyo tar 8
wasipokubaliwana basi tunarud barabarani
 
tatizo liko serikalini maana baada ya vikao mgaya alikuwa anaitisha press conference tofauti na hawa serikali
wao wameenda kumpa jk maneno ya uongo nalo lisivyojua kuchambua mambo likalopoka hovyo
huku likishangiliwa na kima mama sita waliokuwa wameandaliwa humo ndani ili kulishangilia

na hao kina kapuya wangekuwa wanatoa taarifa ya mazungumzo tungejua wamefikia wapi lakini hili nalo li kapuya kazi imelishinda na sasa ndo na amini msemo wa mwl wangu wa chemistry bwana makonikovu kuwa ''a profesor is a person who knows much about a very little thing'' kama anajua habari ya sikio basi hajui habari ya jicho.kapuya yuko hapo
 
Namfahamu vizuri mgaya...ni mtu wa maneno yake...ikifika tarehe 8 may ukweli zaidi utajulikana na mgomo utakuwa palepale...hapa jk alichofanya ni kuahirisha tumbo la kuhara...likisokota zaidi lazma uwahi maliwatoni huna ujanja....yeye anadhani tarehe 8 ni mbali kwakuwa wageni wake wa wef watakuwa weshaondoka na yeye kwa style yake ya uoga wa kunguru atakimbilia ziarani nje ya nchi awaache kina mgaya wagome yeye akibembea jamaica nyingine...

Only time will tell how the clock tik....
 
Natofautiana na wewe. Ishu si uoga bali ni ukweli wa lile linalotaka kufanyika. Mie naomba nifaham CV za hawa watu wa TUCTA. Nami nawaona si wa kweli. Pamoja na watu wengi kujenga hoja kisiasa zaidi lakini lazima ufike wakati kila mmmoja wetu aseme ukweli hata kama unauma. Kuna concept ndogo tu ya kifedha hebu tuitumie then tukubalie.

Kuna usemi unasema dhamana za sriakali zina attract interest ndogo kwa sababu serikali haiwezi kudefault. Ina maana kwamba serikali inaweza kuprint note za ziada na kulipa deni husika. Mf leo JK na serikali wangeamua kulipa mshahara wa TUCTA inamaana inflation ya hali ya juu ingehitokeza na hata hiyo pesa inayodaiwa isingekuwa na thamani tena.

Kwahiyo madai ya mshara huo wa laki 3, takribani 300% increment hayaingii akilini. TUCTA walidai kisichowezekana. Ina maana hawana jopo la watu la kufanya tathmini ya madai yao badala ya kukimbilia kuandika madai kama hayo kwenye vyombo vya habari. Kwanini wasing'ang'anie kwenye inflation. Maana inflation kwa sasa ndiyo adui wa kipato cha mfanyakazi. Kwanini wasihakikishe serikali inachukua hatua kwenye kupanda ovyo kwa chakula na nyumba?

Na kwanini wasidai kinachowezekana? Yaelekea hawa TUCTA hawajui collection ya serikali ni kiasi gani na wafanyakazi ni wapo wangapi?

Mkuu,
TUCTA wanajua sana, hadi wanajua ni jinsi gani serikali inavo fuja na inavo fanya uzembe kukusanya mapato hasa kwa wezi wa raslimali zetu kwa kilemba cha wawekezaji!

Ikipatikana serikali makini, kwa utajiri uliopo bongo, hata laki 5 kima cha chini zinapatikana tu mkuu. Tabu yetu kubwa, ni kukosa hiyo makini
 
mgaya bwana ndo mwanaume
ila sema tu jk alitumia ubabe wake ila ngoja hiyo tar 8
wasipokubaliwana basi tunarud barabarani

Nashawishika hawa jamaa wa TUCTA wapo vizuri sana! Ukisoma press conference yao ina mantiki si kama mkulu alivyobwa bwaja! Jamaa waliita press conference na kuongea na walengwa. Mkuu wa Nchi aliamua kuwa na Mkuu wa Majeshi, IGP halafu anaenda kuongea na wazee waliokata tamaa na maisha wanasubiria kifo tu Mhhhh ama wale wazee wasiofikiri wa CCM! Mwanzo mgumu ila safari tutafika tu
 
Mkuu inawezekana pia kuwa pale shambani mwa bibi waliogeza hisia katika hotuba zao. Inawezekana pia kuwa waliahidiana kukutana tena tarehe nane kwa ajili ya mazungumzo zaidi, so wangejibana wao kama wangeamua kugoma. Tusubiri hiyo tarehe 8

Tarehe 8 hakutakuwa na jipya.Mheshimiwa Rais ameshaweka wazi kuwa mishahara waliyoomba haitekelezeki hivyo hata kama watagoma kwa miaka nane ijayo hawatapata wanachokitaka.Hakutakuwa na jipya zaidi ya kukubaliana na hoja za viongozi wa serikali.
 
wajamani ebu angalieni majira ya leo, kuna jambo mzee alisema juu ya TUCTA, ..... ya kuwa walitakiwa kuonana na maafisa wa Wizara vya Fedha tarehe 23/04/2010 saa 4.00 asubuhi, lakini walifika saa 8, .......................kwa balua waliyopewa sisi hiyo tena kwa kutunia nukusi ya saa 4.30, walitakiwa fika saa 8.30, sasa nani muongo? MGAYA AU JK NA WASHAURI WAKE?
 
Kwa wale wanao mlaumu MGAYA kuwa ni mwoga basi wao ndo wazandiki kabisa. Mafanikio ya TUCTA. Kwa mara ya kwanza katika historia ya Wadanganyika TUCTA imefanikiwa kumpiga chini Rais kuwa mgeni rasmi wa may mosi. Baada ya kukosa pa kuzungumzia aka mwagiza mpiga zumari wake Makamba awatafute wana CCM akawabandika uzee wa dar es salaaam. Kila aliyepata mwaliko wa mpiga zumari alikamatishwa elfu kumi. JK akaanza kughani mashairi wana ccm wanaitikia, hiyo taarabu iliyo chukuwa muda wa dakika 90. MGAYA ni kiongozi anaye simamia maamuzi ya vikao. Mgomo ulipitishwa na baraza kuu la TUCTA kama kiongozi hawezi kuenda tofauti na maamuzi mpaka hapo maamuzi yabatilishwe na vikao husika. Kabla ya mei mosi hakukuwa na kikao kingine kilicho itishwa hivyo Mgaya alikuwa na haki kabisa yakusema mgomo uko pale pale hata JK analijua hilo ila kwa sababu ni kilaza basi akaamua kughani mashairi.

Serikali iliomba mazungumzo baada ya kutangazwa mgomo ambao kisheria unatakiwa utangazwe siku 60 kabla na TUCTA wamefanya hivyo sasa JK kateka uwezo wa mahakama kwa kusema ni batili, ni mahakama au TUCTA ndo wenye uwezo wa kusitisha huo mgomo. Well done TUCTA ya akina MGAYA sio ya marehemu BRUNO, KOLIMBA ambao walikubali kuuza uhuru wao kwa ajili ya ccm
 
Hivi kati yenu nyote mnaozungumza hapa kuna mmoja kati yenu ni mwanachama wa TUCTA?...Kuna yeyote mfanyakazi ambaye anaguswa moja kwa moja na mgogoro huu wa mishahara ya wafanyakazi, kodi na malipo ya uzeeeni?..Kuna mtu kenda kuzungumza na TUCTA kupata habari kamili ya vikao vilivyokwisha fanyika?..

Kabla ya TUCTA kutangaza habari ya mgomo, nini yalikuwa majibu ya serikali kuhusiana na mishahara maanake nakumbuka vizuri swala hili lilizungumziwa kwa hoja Bungeni na halikupatiwa jibu.

Mimi nadhani tutakuwa hatukumtendea haki Mgaya kwa sababu tu JK kasema.. tukaamini maneno yake hali sote humu tunafahamu kwamba swala la mishahara ya Wafanyakazi sii swala la maamuzi ya mtu mmoja huyo Mgaya. Ni ujinga mkubwa sana kuamini kwamba huyu mtu mmoja Mgaya ndiye anayeweza kuwadanganya Wafanyakazi wote Tanzania kuchukua hatua ya mgomo wakati mifano mingi ya nyuma imetuonyesha kwamba viongozi wote wa migomo wamekuwa wakichukuliwa hatua kali inapofikia hatua ya makosa ya makusudi kama aloyafanya Mgaya.

JK ni rais wa nchi kama kweli yeye anaamini Mgaya alitumwa na watu kuendesha kampeni chafu kama hii basi bila shaka hatua za kisheria zingechukuliwa dhidi yakea na sii kuendesha mkutano wa kupakana tope..Tumefikia mahala pa kujiuliza ati nani mkweli baina ya JK na Mgaya?.. hivi ndivyo tunavyotaka kuongozwa kweli?

Wakuu zangu mkutano wa JK na wazee kuhusiana na TUCTA ulikuwa uswahili mtupu na kwa bahati mbaya - Ndivyo Miafrika tulivyo! tukayapokea majungu hayo kama hotuba ya kitaifa.
 
Natofautiana na wewe. Ishu si uoga bali ni ukweli wa lile linalotaka kufanyika. Mie naomba nifaham CV za hawa watu wa TUCTA. Nami nawaona si wa kweli. Pamoja na watu wengi kujenga hoja kisiasa zaidi lakini lazima ufike wakati kila mmmoja wetu aseme ukweli hata kama unauma. Kuna concept ndogo tu ya kifedha hebu tuitumie then tukubalie.

Kuna usemi unasema dhamana za sriakali zina attract interest ndogo kwa sababu serikali haiwezi kudefault. Ina maana kwamba serikali inaweza kuprint note za ziada na kulipa deni husika. Mf leo JK na serikali wangeamua kulipa mshahara wa TUCTA inamaana inflation ya hali ya juu ingehitokeza na hata hiyo pesa inayodaiwa isingekuwa na thamani tena.

Kwahiyo madai ya mshara huo wa laki 3, takribani 300% increment hayaingii akilini. TUCTA walidai kisichowezekana. Ina maana hawana jopo la watu la kufanya tathmini ya madai yao badala ya kukimbilia kuandika madai kama hayo kwenye vyombo vya habari. Kwanini wasing'ang'anie kwenye inflation. Maana inflation kwa sasa ndiyo adui wa kipato cha mfanyakazi. Kwanini wasihakikishe serikali inachukua hatua kwenye kupanda ovyo kwa chakula na nyumba?

Na kwanini wasidai kinachowezekana? Yaelekea hawa TUCTA hawajui collection ya serikali ni kiasi gani na wafanyakazi ni wapo wangapi?
Unataka Cv za watu wa TUCTA za nini, kwa sababu unasema wangekua na jopo la watu kufanya tathimini kidogo wasingekuja na madai hayo na Wahadhiri wa Chuo Kikuu nao ilikuaje warudi tena darasani kudai kitu ambacho hakiwezekani ni tatizo kubwa hivi Watanzania tumerogwa na nani ?
 
Back
Top Bottom