Huyu ndiye Christopher Kasanga Tumbo (RIP) - Mwanasiasa Machachari

Wakurugenzi,

Nilibahatika kuzaliwa kijiji kimoja na Chritopher Kasangatumbo, alikuwa si mbinafsi mjamaa wa kweli, nilibahatika kumjua nikiwa kijana mdogo sana pale kijijini kwetu ipole, alikuwa mzee mpole na kwenye hekma sana; kwenye misiba alikuwa anatumia muda mwingi kutuelimisha, nakumbuka alituambia mambo ya demokrasia na dhana nzima ya vyama vingi kipindi nipo darasa la tatu; sikuielewa philosophy yake hadi nilipofika kidato cha sita na kukutana na kitu kinaitwa vyama vingi (1995) hapo ndipo nikafungua macho na kujua ni nini hasa Kasangatumbo alimaanisha those days.

Kuna tetesi kwamba wale wote waliohoji au kwenda tofauti na mawazo ya mwalimu walipata ban; yule mzee Kasangatumbo alifanyiwa visa vingi sana hadi kufikia kuibiwa ngombe zake zote, Pamoja na kuishi uingeleza lakini hakuwa na mali yoyote ile mbali ya ngombe zisizozidi therathin alizorithi kutoka kwa wazazi wake. Nilibahatika kusoma na watoto wake, nakumbuka hata viatu hawakuwa navyo; tulienda shuleni pekupeku pamoja ingawa wenzangu waliyaonja maisha ya Uingeleza.

Mzee alikuwa mjamaa wa kweli na hilo halina ubishi, tatizo ni kwamba je alikorofishana vipi na mwalimu? Mimi na wewe hatujui, kuishi kijijini ilikuwa ni moja ya adhabu alizopewa toka juu. Kuna kipindi pale Tabora mjini Bendera ya taifa ilikuwa inashushwa, yeye hakusimama, akakamatwa kupelekwa kituo kikuu, pale kituoni akawaambia mapolice kwamba hawezi kuongea ya yeyote yule pale isipokuwa mwalimu tu. Police hawakumpa nafasi hiyo bali wakamsweka ndani - habari zikamfikia mwalimu ikulu na mara moja akawaambia wamfungulie aende zake - hizo zilikuwa moja ya story zake tukiwa kwenye misiba pale kijijini kwetu.

Kuna siku nilikuwa nimepanga foleni kwa ajiri ya kupata vitu adimu (sukari, sabuni), kwa wale mnaokumbuka yale maduka ya RTC basi watoto tuliambiwa twende mapema ili wakati duka linafunguliwa saa 9 basi tupate vitu hivyo; mida ya saa kumi duka linafunguliwa foleni ikiwa ndefu sana, nikamwona Kasangatumbo anafika eneo la duka, akatuambia tumsikilze dk tano, pale nakumbuka alituambia tutapanga foleni hizo hadi tutakapoamua kuwa na demokrasia ya vyama vingi - pale sikuelewa kitu kwamba hiyo demokrasia ndiyo italeta maduka mengi? I was young by age anyway. (9)

Inaendelea post #2 chini...

cc Ngongo, JingalaFalsafa, Mzee Mwanakijiji, Ogah, Mohamed Said, Nguruvi3, Mchambuzi, WOWOWO, Mkandara, Jasusi, Gembe, Phillemon Mikael, Mwanagenzi, Rutashubanyuma, Augustine Moshi, Pasco,
Je, wamfahamu mzee Obed Mgongo?
 
Last edited by a moderator:
Swali dogo tu, chama kilikuwa na uhai wa miaka 2, uliwezaje kukipima na kusema kilikuwa na nguvu saaana, wakati hata hakikushiriki kwenye uchaguzi? Hivi kipimo cha nguvu ni watu kufika mkutanoni? Kumbuka katika nchi zetu, ambazo watu kazi zao ni za msimu kama wakulima, mikutano, ni moja pa mahala kwenda kutoa stress, na kuona vimwana kama ngomani.

I really doubt your analysis
 
Nilibahatika kukutana na huyu Mzee na alikuwa anapenda sana kueleza historia yake.

Alikuwa mwakilishi wa kwanza wa serikali ya tanu nchini Uingereza kama balozi.

Lakini alirudi Tanganyika 1962 akaanza kudai vyama vingi na kuanzisha NDP ndipo akapelekwa detention gereza la Uyui tabora huyu mzee alikuwa ni mfungwa wa kwanza kuwekwa katika Gereza la Uyui wakati huo bado jipya kabisa. Ina maana ni mfungwa namba moja.

Kuanzia hapo akaitupa kadi yake ya TANU akawa mpinzani bila chama na hakuwahi kurudi tena TANU wala kuwa mwanachama wa CCM.

Alisema kuna siku alikuwa analima shambani kwake akawa anasikiliza taarifa ya habari saa 7 mchana kwenye redio yake akasikia Nyerere anatangaza kuwa Tanzania tunaingia kwenye mfumo wa vyama vingi.

Akarudi nyumbani kwake haraka sana akamwambia mke wake ampangie vitu viwili vitatu kwenye begi lake safari ikawa moja kwa moja Dar es salaam na akakutana na akina Chief Fundikira na kuanzisha UMD.

Alikuwa kiongozi mpinzani wa kweli na kwenye historia ya wakati ule ni kiongozi wa upinzani pekee ambaye hakuwahi kuwa mwanachama wa CCM.

Wengine wote walishawahi kuwa wanachama wa CCM kwa namna moja au nyingine. Sababu kubwa ilikuwa huwezi kupata kazi bila kuwa mwanachama wa CCM kwa maana nyingine uanachama ulikuwa lazima
.
 
Hii thread ndiyo kwanza naiona.

Kasanga Tumbo, Abdallah Fundikira Na nduguye Mtemi Lugusha wa Sikonge walionja kichapo cha Nyerere.

Fundikira yeye alikimbilia Kenya ila Lugusha Na Kasanga Tumbo walipata kifungo cha nyumbani.

Walikuwa hawaruhusiwi kukutana Na watu wengi bila idhini ya Polisi.

Kuna Siku nilimuona Nyerere akiongea Na Lugusha Chang'ombe karibu Na kajiji cha Mlogoro Na bandage akamfungulia mlango wa Benz, wakaagana Na akaufunga mlango yeye Na siyo Walinzi au Dereva.

Baada ya Miaka kadhaa, Lugusha akaja kuwa Mbunge wa Sikonge kwa CCM. Ila alikuwa bomu Sana.

nafikiri baadaye ikawa order arudi kwao kijijini, na ndiyo maana anakarudi ipole; ni kweli alikuwa kama mtu aliyechanganyikiwa na hakuwa na marafiki pale kijijini, alikuwa mpweke sana na muda wa kuongea na wanakijiji ulikuwa ni wakati wa misiba tu. Na kila utakapomwona lazima awe na radio yake ndogo maskioni na mara nyingi tulikuwa tukisogelea tunasikia habari za kiingeleza, nafikiri alikuwa nasikiliza BBC

Mzee huyu alikuwa anachunga ngombe kutwa nzima juani, mavazi duni sana, kiujumla hali ya miasha yake ilikuwa vigumu kuielezea.
 
Nawafahamu Watoto wake kadhaa ukianzia Dr wa SUA, L, A, M.... Na wajukuu kadhaa. Ar... Yuko Mwanza mama sikosei.

Mzee Obed sikuwahi kubahatika kumuona au kukutana naye. Ila nilikuwa namfahamu Baba yake Prof. Kategile kutoka Ipole pia.

Je, wamfahamu mzee Obed Mgongo?
 
Nilibahatika kukutana na huyu Mzee na alikuwa anapenda sana kueleza historia yake.

Alikuwa mwakilishi wa kwanza wa serikali ya tanu nchini Uingereza kama balozi.

Lakini alirudi Tanganyika 1962 akaanza kudai vyama vingi na kuanzisha NDP ndipo akapelekwa detention gereza la Uyui tabora huyu mzee alikuwa ni mfungwa wa kwanza kuwekwa katika Gereza la Uyui wakati huo bado jipya kabisa. Ina maana ni mfungwa namba moja.

Kuanzia hapo akaitupa kadi yake ya TANU akawa mpinzani bila chama na hakuwahi kurudi tena TANU wala kuwa mwanachama wa CCM.

Alisema kuna siku alikuwa analima shambani kwake akawa anasikiliza taarifa ya habari saa 7 mchana kwenye redio yake akasikia Nyerere anatangaza kuwa Tanzania tunaingia kwenye mfumo wa vyama vingi.

Akarudi nyumbani kwake haraka sana akamwambia mke wake ampangie vitu viwili vitatu kwenye begi lake safari ikawa moja kwa moja Dar es salaam na akakutana na akina Chief Fundikira
na kuanzisha UMD.

Alikuwa kiongozi mpinzani wa kweli na kwenye historia ya wakati ule
ni kiongozi wa upinzani pekee ambaye hakuwahi kuwa mwanachama wa UMD.

Wengine wote walishawahi kuwa wanachama wa CCM kwa namna moja au nyingine. Sababu kubwa ilikuwa huwezi kupata kazi bila kuwa mwanachama wa CCM kwa maana nyingine uanachama ulikuwa lazima
.

Hapo vipi? Umetuchanganya.
 
Kwasababu aliaminisha watu vyama vingi ni vita. Dikteta sana yule dingi[/QUO

Hahahaaa.....Mwacheni BABA WA TAIFA apumzike. Mwisho a sikumtaanza kusema yeye ndo amekuwa akisaini mikataba ya kinyonyaji. Kwamba fisadi wote ni matokeo yake sio ujinga wetu watz
 
[QUOTEzinawezaunist, post: 6010545, member: 87184"]Ukweli ni kwamba histori ya Tanganyika imechakachuliwa sana na Baba CCM yaani Tanu, yapo mengi kama haya. Na miaka 20 ijayo yanaweza yasipatikane tena. Maana wale wazee waliokuwepo wakati huo wanaishia. Namkumbuka Zuberi Mtemvu, Michael Sanga, Patric Kunambi, Kasela bantu, Lifa Chipaka, Kassim Hanga, Oscar Kambona, Aboud Jumbe, Mwamwindi the Great, NK. Ni vizuri kujua upande wa pili wa historia.[/QUOTE]
Pasi zinaweza kupigwa na karibia wachezaji wote uwanjani including goalkeeper lakini finally atakayefunga goli ndo atakayebeba sifa zote.
 
Kinachosikisha ni namna treatment ilifanyika kwa wapinzani wa wakati huo; walionekana ni maadui wakubwa - its just the same what is happening now.

Watu wenye mawazo badala katika uongozi wa taifa lao ni watu muhimu sana; kazi yao kubwa ni kuonyesha watawala the 2nd option to rulling the nation; sasa kuwakandamiza hawa ni kuliua taifa. Hili ndilo lilifanyka enzi hizo na ndilo linafanyika sasa. Killing opposition.
 
At least I have seen someone who is unveiling the truth, What happened to him?
Kafa maskini kazikwa kienyeji; kaburi la udongo; just thinking kama wanafamilia watanikubalia basi nitalijengea. Huyu ndie balozi wetu wa kwanza nchini ui geleza baada tu ya uhuru wa nchi yetu 1961.Sidhani kama watanzania wengi wanajua h5istiria hii.
 
Back
Top Bottom