Labrujita
JF-Expert Member
- Jun 12, 2015
- 399
- 126
Ni vizuri ukatambua kwamba Iringa siyo koloni, sio shamba la mtu binafsi wala sio hekalu la walioshiba kufanyia mambo yao bali Iringa ina wenyewe ambao kimsingi wenyewe hawa ni wavumilivu, wastahimili na marafiki wa kweli kwa wanaoheshimu mkoa wao na watu wake.
Nakushauri ni bora ukajikita kuendeleza biashara zako za malori ya mafuta, viwanda vya mikate, maziwa na ufugaji ng'ombe ambao wazazi wenu waliwaachia na kuacha figisufigisu za kuingilia siasa za Iringa na kutaka kuiharibu Iringa yetu ambayo wazee wetu wakiongozwa na Mkwawa waliipigania dhidi ya maharamia wa kijerumani, wangoni na jamii nyingine tena kukiwa na kumbukumbu ya kumwaga damu (armed struggle) historia ambayo sidhani kama unaifahamu au inamanufaa kwako. TUACHIE IRINGA YETU tafadhali kwani naogopa siku wanaIringa wakiamua hakika amini maneno yangu HAPATATOSHA........
Nawasilisha, mwenye kung'amua na ang'amue.........
Nakushauri ni bora ukajikita kuendeleza biashara zako za malori ya mafuta, viwanda vya mikate, maziwa na ufugaji ng'ombe ambao wazazi wenu waliwaachia na kuacha figisufigisu za kuingilia siasa za Iringa na kutaka kuiharibu Iringa yetu ambayo wazee wetu wakiongozwa na Mkwawa waliipigania dhidi ya maharamia wa kijerumani, wangoni na jamii nyingine tena kukiwa na kumbukumbu ya kumwaga damu (armed struggle) historia ambayo sidhani kama unaifahamu au inamanufaa kwako. TUACHIE IRINGA YETU tafadhali kwani naogopa siku wanaIringa wakiamua hakika amini maneno yangu HAPATATOSHA........
Nawasilisha, mwenye kung'amua na ang'amue.........