Huyu ndio mwanaume ninayemtaka, sitaki kuumiza moyo wangu una thamani

Utafiti unaonesha kuwa wanokuwaga na mbwembwe nyiiingi mara nyingi wanaishia kuolewa na watu wa kawaida sana tofauti na vigezo 10+ alivyoviweka
 
Wakuu salaam.

Kwa malezi niliyolelewa mimi sistahili kufanya ili jambo, pia kwa mila na desturi za kiafrika sistahili kufanya hiki kitu, lakini huu moyo ni wangu, na mmiliki wa moyo wangu ni mungu. Sasa nikajiuliza kwa nini niendelee kuumia? Hakuna sababu ya kuendelea kuumia? ingawa najua mwanamke kumtafuta mwanaume ni aibu kubwa, ila nikawaza kwakuwa kuna sababu ambayo najua ni muhimu sana akipatikana na nikampenda nitamuweka wazi na atanielewa. Mamayangu amenilea vizuri kwa maadili na heshima, nina Imani ninachokiandika hapa mungu yupo anashuhudia,

Wale mtakaokuja kuniponda eti kwa nini nitafute mtandaoni huku niishiko hawapo? Jibu ni kwamba wapo kibao na wengine nikili wananililia kunioa but, for the sake of my heart wacha niweke wazi mwanamme ninae mtaka staki wahuni mm sio mhuni mung ndo shihidi.

SIFA ZA MWANAUME NINAE MTAKA.

1. Awe na mama yake mzazi/mlezi lakini akiwa na wazazi wot itapendeza sana.kama hana wazazi basi sawa ni mpango wa mungu ingawa itaniuma sana,

Why awe na mama yake? wakuu nataka kumuona huyu mwanamke duniani kote yeye ndo atokee anizalie mme? Nataka kumuona nimwambie ‘mama asante kwa kubeba mimba miezi 9 ukanizalia mwanaume wa ndoa nitakupenda kama mama yangu mzazi.’

2. Awe msafiiiiii. Narudia tena awe msafi kupitiliza spendi mwanaume mchafu sipend aina yeyote ya uchafu, No no nataka siku nikikutana nae macho yangu yadhibitishe kuwa ni msafi,yaan kuanzia kwake ndani mavazi awe smart.

3 Awe mrefu.

4. Rangi Yeyote haina shida kwangu la muhimu iwe inang'aa loh maana wengine hawajuagi hata lotion nzuri za kiume.

5. Awe anajua kuvaa. kama hajui kuvaa smart nitamfundisha hii sector niko vizuri sana

6. Asiwe mwembamba. nataka zawadi za nguo nitakazokuwa nampa zimkae vizuri yaan awe na body size ya kati.(gentleman

7.Awe ana upendo. jamani kama mimi.nasisitiza kama una roho ya paka usijidanganye nataka nionje taste of love

8 Awe ana care, jamani awe na mkono mwepesi hata akinipa pipi ina thamani kwamgu, namiss hii kitu mm natoa sana nikimpenda mwanaume siwezi kutoka mjini bila kumnunulia chochote nguo ndo usiseme.sitaki MTU bahili aisee

9.Awe kristo rc na mcha Mungu

10. Awe na miaka 34+ ni lazima.

11. Awe ameshafika stage Fulani ya maisha. Staki mwanaume tegemezi, atleast awe na mradi mmoja wa kumuingizia pesa tofauti na ajira.staki mwanaume mzembe ambae hajui kutafuta pesa. Inshort awe na mipango ya kuwa somebody na future nzuri .staki mwanaume anaemiliki p.u.m.b.u na smartphone.mm ni mtafutaji staki mwanaume wa ovyo.

12,Awe na kucha zote miguuni, napenda weekend nikimkata vizuri kucha zikae fresh avae sandles sometimes pensi fulan amaizing atoke bomba.

13 Asiwe alishawahi kuoa wala kuwa na mtoto nje ya ndoa, Mtoto ni Baraka ila watoto wa nje ya ndoa wanaleta migogoro .staki mme wa mtu mm.

14. elimu degree, masters phd vyote sawa.
15 asiwe mhaya .plz naomba msinielewe vibaya samahani sana mnisamehe
16 asiwe mvuta sigara.
17 awe tiyari kupima HIV
18.awe na pua ndefu.


SIFA ZANGU

1. Namshukuru mungu kunipa upendo nina upendo kwa kila mtu

2. Mimi ni msafiiiiiiiiii yaaani ni msafiiiii kupitiliza

3. Nimeajiriwa ila nimejiajiri kimradi changu kidogo pemben tho sipendi kuajiriwa ndo mana nataka mwanaume ambae atanipa sapport tupanga miradi tuwe na maisha bora.

4. Elimu –degree

5. Rangi –mweusi kiasi

6. Urefu size ya kati umbo mm sio bonge.

7. nacare sana nikimpenda mtu nampenda kwa vitendo

8. Sijawahi kumsaliti mtu

9. Dini mkristo –rc

10, najitegemea sitegemei mwanaume vitu vidogovidogo nina uwezo navyo in short mm ni mtafutaji.

11mimi ni mcha mungu.

12 napenda sana competition sipend mme wangu azidiwe na wanaume wengine hasa kimaendeleo

13 sina mtoto na sijawahi kuolewa.

14 nina akili ya maisha yaani IQ yangu ipo juu saa upstairs niko vizuri.

15 Mm ni mchangamfu sana mcheshi namshukuru mungu kuniumba hivi.

16. mm ni mvumilivu ila ikiwa too much, siwezi kuvumilia tena.
17. Situmii pombe na sijawahi tumia.
18. niko tiyari anytime kupima ngoma
19 mimi sio mtu wa kurirusha viwanja ovyo ovyo na sijawahi kukanyaga hata club.

N.B. Mimi ni binadamu sijakamilika nina mapungufu yangu lakini hivyo kidogo mungu alichonijalia kinaendana na ukweli niliouandika hapa. hasa sifa zangu.


NOTE. Ningependa nikutane na mwanaume ambae alishawahi kuishi nje nchi yaani ana exposure ya mambo mengi nina sababu ya msingi hasa kimaendeleo / biashara LAKINI AKIDHI VIGEZO VYOTE NO 1-15 . lakini kama hajawahi kuishi nje na ana vigezo hakuna mbaya najua nikiwa nae tutafika mbali.


NINAVYO MISS.

1. Mme wamgu uko wapi? Nimekusubiri nimejitunza nimechoka kukusubiri

2. Nimemiss kukumbatiwa miaka sasa

3. Nimemiss kukiss staki kukiss na jitu la ajabu lichafu

4. Nimemiss kubebwa

5. nina upweke staki kukaribisha vijianaume vya ajabu kwangu

6. Uko wapi baba nikupikie uone ninavyojua kupika.

7. Njoo uone nilivyo msafiii sijawahi kuingiza mwanaume kwangu njoo uone kwangu nilivyo msafi

8. Njoo uone ninavyojipenda

9. Njoo nikuoneshe upendo
10 Njo baba mama yangu anataka kukuona.
11. Namiss neno baba njoo nikuite baba.

Kiukweli nimeniss vingi sana sio kwamba nilipo hakuna wanaume wapo wengi kazini ila nataka wangu wa moyo nimuoneshe upendo nae anioneshe maana hiki ndicho ninachokimiss kutoka kwa mtu nimpendae.

Mwisho mm ni mwanamke ninaejitambua wale ambao mtakuja hapa kunitusi eti nichonge au nizae mme wangu nawaomba tafadhari mkae kimya najua ninachokita. na nina imani huyu mtu mwenye sifa hizi yupo.

Angalizo.

kama unajua huna vigezo hivyo hapo juu plz usijisumbue kuja pm maana niko makini, najua kuna vitoto vinavyomiliki laptop baada ya kupata mkopo wa board vitakuja plz tuheshimiane ninaomba.



Karibuni.
Hujataja umri wako,,,
 
Kwa sifa zako ulizojitaja kama upo ivyo na huna mume Wewe unamatatzo


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
kwa bahati mbaya wenye sifa hizo ni wahaya kwa hapa Tanzania,wasomi,warefu,wenye hela na upendo wa dhati.
 
Kumbe bado hajapatikana huyo mwanaume,,, maana hili tangazo ni la mda kidogo anyway ngoja niongeze juhud naweza nikabeba mtoto...
 
Endelea kusubiri mama mungu ume mmiliki?
Kiufupi kuolewa kwa mwana mke hakuji kama mvua ya masika yaani ifikapo january itaanza kunyesha. Bali nafasi ya kuolewa huja kama bahati.

Mimi nakushauri bure kabisa ya kwamba ukipata mwanaume yeyote narudia tena yeyote wewe olewa, hivyo vigezo vyako ulivyo viweka viondoe kabisa vita kufanya usiolewe kabisa, kwa maana inaonekana unawasifu ufuatao.

1. Unamiaka 34 na ndo maana ume weka mpaka kwamba lazima mwanaume atayekuja awe na miaka 34 , hii ni kutokana na ukweli kwamba hutaki kuolewa na mdogo wako.

2. Mpaka ulipo fikia hapo inaonekana umewahi kutendwa saana kiasi kwamba umeamua kuigia sokoni ukijaribu kutoa vugezo fulani fulani kama viambata vya kukusaodia kumpata mwanaume unaye mtaka. Nathibitisha hili kutokana na ukweli kwamba ni vigumu saana kwa umri wako ikatokea hujawahi kupenda au kupendwa maishani.

3. Wewe ni mwana mke unanye ogopa shida na ndo maana unataka mwana mume aliyesoma ukiamimi kusoma vizuri ndio kupata kazi nzuri , lakini umesahau kwamba unapoishi na mwanaume haushi na pesa yake au ukwasi alio nao bali huishi na mtu mwenyewe vingine ni matokeo. Rejea wimbo wa marijani rajab (ooooo oòoo shida) ukutie moyo ili ujue shida inaweza kutokea hata baadan ya kumpata anaye miliki kitu.

4. Unapo sema awe na kucha zote miguuni je nawewe una meno yote je huna jino lililo toboka? Kama unalo basi utajiongeza mwenyewe hapo.

5. Umejaribu kuonyesha sifa nyingi ulizo nazo lakini kuna sifa kuu ambayo wanawake wengi wasio na sifa kama zako ndo wanao sumbua ndoa nyinhi hapa mjini wanazo, yaani KIUNO FENI je nawewe sifa hiyo unayo? Siunajuwa mjini msingi kiuno ukisha tendwa ndo baibai? Rejea ( omy dimpose) kwa faida yako

6. Umesema wewe ni masafi saana huja fafanua ni msafi kivipi kwa maana kwa asili mwanadamu ni mchafu na ndomaana tukitembea kwa muda mrefu juani hurejea nyumbani kuoga , na kama ishu n usafi wa ndani hilo ndo litakuwa jukumu lako kumbe usikimbie majukumu.


USHAURI
ukimpata mtu yeyote olewa naye kwa maana duniani hakuna mwana ume wala mwana mke mkamilifu bali wanaume na wanawake bora wako kila mahali. Chaguwa moja kuishi dhamiri au kuishi katika kristo .

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom