Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 46,887
- 143,983
Miezi karibu sita kapita katika tanuru la uhakika,tanuru lenye mabonde, milima na miba maana zoezi hili lilikuwa na gharama zake kwa watumishi ikiwa ni pamoja na usumbufu mbalimbali ulioambatana na zoezi hili kama vile kushinda kwenye foleni,n.k.
Wako waliosafiri umbali mrefu kufuata vyeti,wako waliotoka vyuoni kurudi makazini kwa ajili ya kuhakikiwa,wako waliolazimika kwenda baraza la mitihani kwa ajili ya kusaka vyeti, wako waliolazimika kutangaza kupotelewa vyeti ili wapate vyeti vyao na wako waliolazimika kwenda polisi kuripoti kupotolewa vyeti vyao,n.k.
Pamoja na yote hayo,mtumishi huyu mpaka leo hii hajui kama kuna nyongeza ya mshahara na kibaya zaidi hata madai yake mbalimbali hajui atalipwa lini!Waliondolewa kazini nao hatima yao haijulikani.
Ukitaka kuchoka zaidi juu ya kazia hii inayowakabili watumishi, wasikilize wenye dhamana wanapohojiwa na vyombo mbalimbali vya habari kuhusu matatizo haya ya watumishi na majibu wanayoyatoa.
Utawasikia kila siku wanaongelea mambo yale yale yaani ni mipango na michakato isiyo na timeframe huku wakikwepa kujibu maswali ya msingi na kupiga siasa tu maana shida hizi wao haziwahusu.Yaani ni mwendo wa ku-buy time tu.
Cha ajabu na cha kushangaza ni jinsi mtumishi huyu anavyopelekeshwa wakati maslahi yake yamesahaulika.
Kwa mfano, hivi sasa wameibuka ma-RC ambao wamekuja na kauli za kuwabeza na kuwadharau kama vile kuwaita watumishi hawa mizigo, kuwadhalilisha mbele ya akadamnasi, n.k.
Kama hiyo haitoshi,baadhi ya watumishi hawa sasa wanakabiliwa na tishio jipya la makato ya asilimia 15 kwa ajili ya kulipia deni la bodi ya mikopo huku mshahara ukiwa ni ule ule.
Hivi katika hali ya kawaida mtumishi huyu morali ya kazi anaitoa wapi?
Kabla ya kuwaza kuwatimua na kuwasema hadharani huku miktaka kuona tija kutoka kwao, jiuluzeni kwanza kama nanyi mnatimuza wajibu wenu kama waajiri kwa watumishi hawa.
Jamani hata ng'ombe huwezi kumkamua kama huumpi majani hivyo acheni kujisahau kwani hawa nao ni binadamu kama nyie na wanahitaji kuthaminiwa na zaidi wanastahili kupewa incentives wawapo makazini
Msisahau kura mlizopewa nyinyi ni kura walizonyimwa wenzenu hivyo msijisahau na muwe considerate.
Wako waliosafiri umbali mrefu kufuata vyeti,wako waliotoka vyuoni kurudi makazini kwa ajili ya kuhakikiwa,wako waliolazimika kwenda baraza la mitihani kwa ajili ya kusaka vyeti, wako waliolazimika kutangaza kupotelewa vyeti ili wapate vyeti vyao na wako waliolazimika kwenda polisi kuripoti kupotolewa vyeti vyao,n.k.
Pamoja na yote hayo,mtumishi huyu mpaka leo hii hajui kama kuna nyongeza ya mshahara na kibaya zaidi hata madai yake mbalimbali hajui atalipwa lini!Waliondolewa kazini nao hatima yao haijulikani.
Ukitaka kuchoka zaidi juu ya kazia hii inayowakabili watumishi, wasikilize wenye dhamana wanapohojiwa na vyombo mbalimbali vya habari kuhusu matatizo haya ya watumishi na majibu wanayoyatoa.
Utawasikia kila siku wanaongelea mambo yale yale yaani ni mipango na michakato isiyo na timeframe huku wakikwepa kujibu maswali ya msingi na kupiga siasa tu maana shida hizi wao haziwahusu.Yaani ni mwendo wa ku-buy time tu.
Cha ajabu na cha kushangaza ni jinsi mtumishi huyu anavyopelekeshwa wakati maslahi yake yamesahaulika.
Kwa mfano, hivi sasa wameibuka ma-RC ambao wamekuja na kauli za kuwabeza na kuwadharau kama vile kuwaita watumishi hawa mizigo, kuwadhalilisha mbele ya akadamnasi, n.k.
Kama hiyo haitoshi,baadhi ya watumishi hawa sasa wanakabiliwa na tishio jipya la makato ya asilimia 15 kwa ajili ya kulipia deni la bodi ya mikopo huku mshahara ukiwa ni ule ule.
Hivi katika hali ya kawaida mtumishi huyu morali ya kazi anaitoa wapi?
Kabla ya kuwaza kuwatimua na kuwasema hadharani huku miktaka kuona tija kutoka kwao, jiuluzeni kwanza kama nanyi mnatimuza wajibu wenu kama waajiri kwa watumishi hawa.
Jamani hata ng'ombe huwezi kumkamua kama huumpi majani hivyo acheni kujisahau kwani hawa nao ni binadamu kama nyie na wanahitaji kuthaminiwa na zaidi wanastahili kupewa incentives wawapo makazini
Msisahau kura mlizopewa nyinyi ni kura walizonyimwa wenzenu hivyo msijisahau na muwe considerate.