kyagata
JF-Expert Member
- Oct 18, 2016
- 6,495
- 12,594
Habari wakuu?
Mimi ni mwanaume mwenye umri wa miaka 32,nilikuwa naishi na mzazi mwenzangu ambae tulibahatika kupata mtoto mmoja wa kiume mwenye miaka miwili sasa.mzazi mwenzangu ni mtu kutoka kabila la wahehe.
Mwaka jana mwezi wa saba nilipeleka barua ya posa nyumbani kwao na wakanipangia mahari, mipango yangu ilikuwa mwaka jana december ningeipeleka hiyo mahari huko kwao but mambo yakaingiliana hapo katikati yaliyopelekea mpaka leo bado sijaipeleka hiyo mahari.Huyu mwanamke kiukweli naweza sema ananipenda sana tu coz sijawahi kuona dosari yoyote kwake.so tatizo limeanza mwezi uliopita, ambapo alianza tabia ya kuwa anashika simu yangu hovyo akakutana na messages kutoka kwa wanawake wengine.
Well, ni kweli nilikuwa nacheat kipindi flani hivi, nilikiri kosa na kumuomba msamaha,alichosema ni kwamba amenisamehe but anahitaji nafasi kwanza ya kuwa mwenyewe coz anaona hana amani kuendelea kuishi na mimi kwa hayo yaliyojitokeza na mengine kadhaa yaliwahi kutokea siku za nyuma, nikamsihi asiondoke but ikashindikana, akaondoka na mtoto wakaenda kupanga mtaa jirani na kwangu..kiukweli sio kwamba simpendi huyu mwanamke,ila tu ni tamaa zetu wanaume ndizo zilizonifanya nikaanza kutoka nje.najua nimemuumiza sana moyo wake kwani alikuwa ni mtu mwenye matarajio makubwa sana na mimi.
Ombi langu kwenu wakuu ni kwamba,nawezaje kumrudisha huyu mwanamke ili maisha yetu yaendelee kama mwanzo?au kwa scenerio hii ya yeye kuondoka nyumbani kwa hasira na kwenda kupanga kwingine nimpotezee tu aendelee na maisha yake?na vipi nikiamua kumpotezea ile barua ya posa niliyopeleka kwao haitokuwa na madhara yoyote?
karibuni kwa mawazo yenu wakuu.
Mimi ni mwanaume mwenye umri wa miaka 32,nilikuwa naishi na mzazi mwenzangu ambae tulibahatika kupata mtoto mmoja wa kiume mwenye miaka miwili sasa.mzazi mwenzangu ni mtu kutoka kabila la wahehe.
Mwaka jana mwezi wa saba nilipeleka barua ya posa nyumbani kwao na wakanipangia mahari, mipango yangu ilikuwa mwaka jana december ningeipeleka hiyo mahari huko kwao but mambo yakaingiliana hapo katikati yaliyopelekea mpaka leo bado sijaipeleka hiyo mahari.Huyu mwanamke kiukweli naweza sema ananipenda sana tu coz sijawahi kuona dosari yoyote kwake.so tatizo limeanza mwezi uliopita, ambapo alianza tabia ya kuwa anashika simu yangu hovyo akakutana na messages kutoka kwa wanawake wengine.
Well, ni kweli nilikuwa nacheat kipindi flani hivi, nilikiri kosa na kumuomba msamaha,alichosema ni kwamba amenisamehe but anahitaji nafasi kwanza ya kuwa mwenyewe coz anaona hana amani kuendelea kuishi na mimi kwa hayo yaliyojitokeza na mengine kadhaa yaliwahi kutokea siku za nyuma, nikamsihi asiondoke but ikashindikana, akaondoka na mtoto wakaenda kupanga mtaa jirani na kwangu..kiukweli sio kwamba simpendi huyu mwanamke,ila tu ni tamaa zetu wanaume ndizo zilizonifanya nikaanza kutoka nje.najua nimemuumiza sana moyo wake kwani alikuwa ni mtu mwenye matarajio makubwa sana na mimi.
Ombi langu kwenu wakuu ni kwamba,nawezaje kumrudisha huyu mwanamke ili maisha yetu yaendelee kama mwanzo?au kwa scenerio hii ya yeye kuondoka nyumbani kwa hasira na kwenda kupanga kwingine nimpotezee tu aendelee na maisha yake?na vipi nikiamua kumpotezea ile barua ya posa niliyopeleka kwao haitokuwa na madhara yoyote?
karibuni kwa mawazo yenu wakuu.