Bbade
JF-Expert Member
- Mar 15, 2013
- 6,725
- 21,804
Kwanini haondoki?
Jibu linabaki kwa mtu binafsi, na sababu zinaweza kuwa ngumu sana. Ukweli ni kwamba, kuondoka kunaweza kuwa vigumu hata wakati unajua ni jambo sahihi. Wengi wetu tunaweza kujaribu kuondoka mara nyingi kabla ya kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi ya mwisho.
Sababu nyingine zinaweza kuwa, hapati ushirikiano/msaada kutoka kwa ndugu jamaa na marafiki au hata serikali za mitaa.
Kushindwa kujikimu kifedha, hapa kama mumewe hampatii fedha ni ngumu kuweka akiba itakayomsaidia kuondoka pale nyumbani.
Pengine akiondoka mumewe atamnyanganya watoto wake, kama mama asingependa kuondoka kuwaacha watoto nyuma.
Akifikiria kazi atapata wapi? ni mda sasa tokea kamaliza chuo na hakupata work experience yoyote, itamchukua muda kupata kazi yenye kipato.
Na kama hajawahi kuishi mwenyewe ataanzia wapi kuanza kuishi mwenyewe na kujitegemea?
Pengine familia aliyokulia au kwenye jamii yake wanawake hawaruhusiwi kuachika/kuacha ndoa zao, anaogopa kuleta aibu na fedhea.
Sababu nyingine, anaweza kujihisi yeye ndio mwenye matatizo/makosa na anastahili hizo adhabu akaona sawa tu, kumbe sisi tulioko nje tunaona tofauti.
Kama mleta mada alivyosema, mwanamme akiwa nje ya nyumbani ni mcheshi huwezi dhania ndio anamnyanyasa mkewe, pengine akishampa vibano anambembeleza na kuhaidi hatorudia tena, hapa huyo dada anaona jamaa atabadilika anaona abakie kusubiria siku atakayobadilika.
Hizo siku anazoenda kwao halafu anarudi inawezekana mumewe anamtisha asiporudi atakuja mpiga zaidi ya mara ya mwisho, mdada anaona bora arudi nyumbani Kwake.
Mnisamehe kwa maelezo mengi ila unyanyasaji kwenye ndoa/mahusiano yapo sana hata wanaume wananyanyaswa.
Wale wanao pitia haya manyanyaso poleni sana.
Jibu linabaki kwa mtu binafsi, na sababu zinaweza kuwa ngumu sana. Ukweli ni kwamba, kuondoka kunaweza kuwa vigumu hata wakati unajua ni jambo sahihi. Wengi wetu tunaweza kujaribu kuondoka mara nyingi kabla ya kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi ya mwisho.
Sababu nyingine zinaweza kuwa, hapati ushirikiano/msaada kutoka kwa ndugu jamaa na marafiki au hata serikali za mitaa.
Kushindwa kujikimu kifedha, hapa kama mumewe hampatii fedha ni ngumu kuweka akiba itakayomsaidia kuondoka pale nyumbani.
Pengine akiondoka mumewe atamnyanganya watoto wake, kama mama asingependa kuondoka kuwaacha watoto nyuma.
Akifikiria kazi atapata wapi? ni mda sasa tokea kamaliza chuo na hakupata work experience yoyote, itamchukua muda kupata kazi yenye kipato.
Na kama hajawahi kuishi mwenyewe ataanzia wapi kuanza kuishi mwenyewe na kujitegemea?
Pengine familia aliyokulia au kwenye jamii yake wanawake hawaruhusiwi kuachika/kuacha ndoa zao, anaogopa kuleta aibu na fedhea.
Sababu nyingine, anaweza kujihisi yeye ndio mwenye matatizo/makosa na anastahili hizo adhabu akaona sawa tu, kumbe sisi tulioko nje tunaona tofauti.
Kama mleta mada alivyosema, mwanamme akiwa nje ya nyumbani ni mcheshi huwezi dhania ndio anamnyanyasa mkewe, pengine akishampa vibano anambembeleza na kuhaidi hatorudia tena, hapa huyo dada anaona jamaa atabadilika anaona abakie kusubiria siku atakayobadilika.
Hizo siku anazoenda kwao halafu anarudi inawezekana mumewe anamtisha asiporudi atakuja mpiga zaidi ya mara ya mwisho, mdada anaona bora arudi nyumbani Kwake.
Mnisamehe kwa maelezo mengi ila unyanyasaji kwenye ndoa/mahusiano yapo sana hata wanaume wananyanyaswa.
Wale wanao pitia haya manyanyaso poleni sana.