Nikukumbushe
JF-Expert Member
- Jun 4, 2013
- 2,602
- 408
Hiki ni kisa cha mume na mke kuachana.
Watu hawa walifunga ndoa mapema. Mke alianza kumfahamu mume baada ya kuolewa tu,hakuwahi kukutana na mwanaume awaye yote.
Wamejenga familia pamoja,wamezaa watoto na kulea . Wameishi pamoja kama familia,wakiwakosoa majirani kwa kushindwa kuwa na familia imara nk.
Bahati mbaya sana,mwanamke alianza urafiki na mke wa jirani ambaye mume wake ana ukwasi.
Familia ya huyu mwanamke iliyumba baada ya mwanaume kutambua kuwa urafiki huo haukuwa wa dhati zaidi ya kutafutaiana wanaume. Basi,yule bwana alikasirika na hatimaye aliwafukuza watoto baada ya kupima DNA kuwa wamezaliwa nje ya ndoa na yule jamaa(mwenye mahusiano na mke wa jamaa)
Alimuonya mke wake kuwa,mke wangu achana urafiki na huyo mwanamke,maana nahisi una mahusiano na mwanaume karibu nyumba ya rafiki yako na mchakato mzima unafanywa na rafiki yako. Baadae yule jamaa aliamua kumfukuza mke wake kwa kuhisi kuwa anatoka nje ya ndoa.
Baada ya kusikia hivyo mwanamke alilia sana na kukimbilia kwa balozi kupata suluhu akidhani kuwa ameonewa na kunyimwa haki yake ya ndoa. Baada ya balozi kutoa uamuzi,yule mwanamke aliwaaga maswaiba zake rasmi ili kuwaandaa kisaikolojia kuwa anaondoka na achana na mume wake wa zamani.
Na baada siku moja,alikutwa na mume wake akifunga ndoa na mume aliyekuwa anakataa kuwa hana mahusiano naye. Huku watoto wakiwa wandaaji wa misosi,wapambaji nk
Je,kama huyu mwanamke alikataa kuwa hana mahusiano na huyu mwanaume,mbona kafunga ndoa naye? Mahusinao yalianza lini?
Je,kwa nini watoto wake waliohisiwa na mume wake kuwa inawezekana walizaliwa nje ya ndoa wako kwa jamaa huyu aliyefunga ndoa baada ya siku moja kuwaaga majirani?
Je,huyu mwanamke aliwezaje kumuacha mume wake wa kwanza aliyemzindua usichana wake? Sababu ni nini?. Je,sababu ya pesa au tamaa ya mwili?
Tusemezane.
Watu hawa walifunga ndoa mapema. Mke alianza kumfahamu mume baada ya kuolewa tu,hakuwahi kukutana na mwanaume awaye yote.
Wamejenga familia pamoja,wamezaa watoto na kulea . Wameishi pamoja kama familia,wakiwakosoa majirani kwa kushindwa kuwa na familia imara nk.
Bahati mbaya sana,mwanamke alianza urafiki na mke wa jirani ambaye mume wake ana ukwasi.
Familia ya huyu mwanamke iliyumba baada ya mwanaume kutambua kuwa urafiki huo haukuwa wa dhati zaidi ya kutafutaiana wanaume. Basi,yule bwana alikasirika na hatimaye aliwafukuza watoto baada ya kupima DNA kuwa wamezaliwa nje ya ndoa na yule jamaa(mwenye mahusiano na mke wa jamaa)
Alimuonya mke wake kuwa,mke wangu achana urafiki na huyo mwanamke,maana nahisi una mahusiano na mwanaume karibu nyumba ya rafiki yako na mchakato mzima unafanywa na rafiki yako. Baadae yule jamaa aliamua kumfukuza mke wake kwa kuhisi kuwa anatoka nje ya ndoa.
Baada ya kusikia hivyo mwanamke alilia sana na kukimbilia kwa balozi kupata suluhu akidhani kuwa ameonewa na kunyimwa haki yake ya ndoa. Baada ya balozi kutoa uamuzi,yule mwanamke aliwaaga maswaiba zake rasmi ili kuwaandaa kisaikolojia kuwa anaondoka na achana na mume wake wa zamani.
Na baada siku moja,alikutwa na mume wake akifunga ndoa na mume aliyekuwa anakataa kuwa hana mahusiano naye. Huku watoto wakiwa wandaaji wa misosi,wapambaji nk
Je,kama huyu mwanamke alikataa kuwa hana mahusiano na huyu mwanaume,mbona kafunga ndoa naye? Mahusinao yalianza lini?
Je,kwa nini watoto wake waliohisiwa na mume wake kuwa inawezekana walizaliwa nje ya ndoa wako kwa jamaa huyu aliyefunga ndoa baada ya siku moja kuwaaga majirani?
Je,huyu mwanamke aliwezaje kumuacha mume wake wa kwanza aliyemzindua usichana wake? Sababu ni nini?. Je,sababu ya pesa au tamaa ya mwili?
Tusemezane.