Huyu Mwanamke......Me n' My lil Girl (happy bday Malaika)

jouneGwalu

JF-Expert Member
Apr 11, 2011
2,687
1,780
Leo ni siku ya kuzaliwa binti yangu wa pekee (mpaka sasa) mpendwa sana!
Kwa mpaka sasa katika maisha yangu, huyu kiumbe ndio kitu kikubwa sana cha mafanikio yangu, na ndio sababu pekee inayonifanya napambana na ndio msingi wa furaha na mafanikio mengine.
Anatimiza miaka mitatu (3), nipo mimi na yeye tu!

Ilianza hivi.....!

Miaka minne iliyopita.

Kuna maeneo hapa mjini dar, unaweza kupata muono wa bahari ya hindi vizuri sana, hapo ndio utatambua utamu na uzuri wa bahari hiyo vilevile maisha.

Golden Tulip Hotel ni miongoni mwa maeneo hayo, najua yapo mengi na wewe unayajua!

Ilikuwa ni ratiba ya mimi na vijana wenzangu wa uswazi, kwamba kila mwisho wa mwezi tunachagua kiwanja kimoja ambapo tunaenda kubadili mandhari (kusafisha macho)

Wakati tupo hapa, eneo la "Maasai pub" stori za hapa na pale huku tuk-enjoy mawimbi yanavyopiga.... haikuchukua mda mwingi kabla sijajua kuwa huo muonekano wa bahari ya hindi na uzuri wake havikuwa na maana tena mbele ya huyu binti aliyepita hapa mbele yetu mda si mrefu.

Ni cashier. Toka nilivyomuona, akili ikawa ishanihama wala sikutaka kupoteza tena muda na kushangaa uzuri wa-view ya bahari ya hindi.

Wakati tunaondoka, nilimpitia pale counter nikamuuliza kama anaujua wimbo wa "All 4 One" unaitwa "As beatiful as You"
Akasema anaujua! Nikamwambia walimtungia yeye...... akacheka, nikachukua namba yake ya simu, mahusiano yakaanza.
Nyuma ya msichana mzuri sana, kuna tabia usiyoitarajia na itakushangaza (nzuri au mbaya)
Ilichukua miezi miwili nikawa nje ya Dar, then akawa ana mimba ya "Malaika"

Kwa bahati mbaya sana, mahusiano hayakudumu (stori nyingine) ila tulichoumba kilidumu.
Akajifungua "Baby girl".... Kabinti kangu ka kike my first born, raha sana!
Sababu sikuwa dar, hivyo baada ya kumuona tu nilirudi huko na mawasiliano ya mara kwa mara pia nilimuunganisha na familia yangu.
Baada ya miezi 6 ya umri wa mtoto, sikuamini nilivyomkuta mwanangu.... mtoto kama katoka Somalia ati ndio "kabemendwa" hivyo. Na alikuwa kishamuachisha ziwa.

Basi bibi yake hapa (Mama yangu) akasema inabidi mtoto abaki naye ili amshughurikie LISHE.
Inaonekana hiyo ndio ilikuwa ahueni ya huyo "shosti" maana toka siku hiyo binti (Mama mtoto) hadi leo hii wala hajatia pua yake hapa! Kamuacha mtoto.

Leo anatimiza miaka 3.
Mtoto lazima awe na mtu wa kumuita Mama, kadiri anavyokuwa shangazi yake mkubwa (dada yangu) ndio amemchagua kama Mama yake.
Tumeamua kumuacha tu aendelee hivyo sababu kwake aunt ndio anaziba pengo la Mama kimalezi, japo anachanganya na sisi tunavyomuita Bibi yake (Mama yetu) Mama, so na yeye anamwitaga Mama kwa kukosea.
Kiukweli sitamani Mama yake arudi kwa mda huu sababu nadhani itamchangnya zaidi mwanangu.

Nachukua wasaha huu kumtakia heri ya siku ya kuzaliwa, Mungu ambariki sana na amzidishie hekima, akili na azidi kuwa mtoto mzuri.
Sanasana Mungu awabariki wakina Baba wote. (Kwa niaba yangu binafsi)
Pia awabariki wakina Mama wote (kwa niaba ya bibi yake na shangazi zake)
Mungu awabriki watoto wote wa Tanzania
 
Congratulations are in order to your adorably cute little Princess for adding yet another year into this world.

I bet she's cute as pie. Means the world to you. And last but not least she's the center of your universe!

Trust me. I know how these cute little girls can be. They can cunningly wrap you around their finger and get away with just about anything. But that's the beauty of it all so just savor it to the fullest.
 
JouneGwalu:
This story is quite interesting..........................................Anyways, hongera sana for stepping up and being a real man. Bila kusahau
:A S-rose::A S-rose::A S-rose:HaPpY BiRthDay to your baby girl:A S-rose::A S-rose::A S-rose:
 
Hongera sana mkuu
kikubwa zaidi napenda kukupongeza
kwa hatua uliochukua kumtunza mwanao
maana wababa wengi ndio wanao kimbia wanao
(wakwangu mmoja wapo) nimefurahishwa sana na story
ingawa mama mtu haji kumuona mwana lakini kama kuna
familia inayomzunguka na kumtunza kumpenda na kumpa
maadili yote then umempa mwanao zawadi ya maisha bora..

Hongera wababa wote ambao wanawatafuta na kuwatunza wanao




Happy Birthday Princess ....
 
Hongera sana kwa mwanao kutimiza umri. Mwanao atajivunia kuwa na baba kama wewe..........Happy Birthday Malaika!!
 
journe i see it is getting better and better... nimependa the whole story
nimependa the fact kwamba the baby is soo young with a father as a single parent
maana in this case tushazoea it is always the mother, nimependa the fact you
are proud of her and you love her saaana... I am proud of you and impressed pia.


To your baby... Happy birthday baby gal, may you be one of the future

ladies who will make positive impact in this world of today

:flypig:and may you forever be Blessed by The Almighty GOD.:flypig:


 
Congratulations are in order to your adorably cute little Princess for adding yet another year into this world.

I bet she's cute as pie. Means the world to you. And last but not least she's the center of your universe!

Trust me. I know how these cute little girls can be. They can cunningly wrap you around their finger and get away with just about anything. But that's the beauty of it all so just savor it to the fullest.

Hahahaha Nyani Ngabu, sijazisahau comment zako,
Kwenye ile sred moja jamaa alileta hapa "Nani kama Baba vs Nani kama Mama"
Post zako zilinifanya nitafakari mara ya pili kama na mimi nampenda mwanangu kama wewe, niliona kama unanifunika!
Ila kwa hii naona nimetoa droo.........!
 
JouneGwalu:
This story is quite interesting..........................................Anyways, hongera sana for stepping up and being a real man. Bila kusahau
:A S-rose::A S-rose::A S-rose:HaPpY BiRthDay to your baby girl:A S-rose::A S-rose::A S-rose:

Ahsante sana.....
Yupo happy sana, aunt zake wanamwandalia keki.
Kaanza kuimba wimbo wake wa birthdya toka majuzi.
 
Nachukia wanawake wanaotekeleza watoto wao zaidi ya wanaume wafanyao hivyo!!

Nwy we ni mmoja kati ya wachache wasioogopa majukumu na nnakupa hongera nyingi kwa hilo.Jitihada zote unazofanya kumlea mwanao ndo zinalipa hivyo kwa kukupa furaha isiyo na kipimo wala masharti!
Hongera tena!!

Happy birthday to your lil‘ girl.May she grow up to be admirable and be loved by many!

Huyo mwanamke hata akija kesho usimruhusu akachakachua akili ya mwanao!
 
Hongera sana mkuu
kikubwa zaidi napenda kukupongeza
kwa hatua uliochukua kumtunza mwanao
maana wababa wengi ndio wanao kimbia wanao
(wakwangu mmoja wapo) nimefurahishwa sana na story
ingawa mama mtu haji kumuona mwana lakini kama kuna
familia inayomzunguka na kumtunza kumpenda na kumpa
maadili yote then umempa mwanao zawadi ya maisha bora..

Hongera wababa wote ambao wanawatafuta na kuwatunza wanao




Happy Birthday Princess ....




Tuko pamoja Afro Denz!
Thanks vile ur there for me.
Pia ahsante kwa niaba ya Malaika wangu.
Nadhani zawadi uliyompa ni anastahili sana,
Sure yeye ni malkia, wa tunu kama hiyo.......
Najaribu kufanya perfect, japo kwa hichi nilichokabidhiwa na Mungu.

(wish nisikie stori yako pia, naamini umwanamke imara sana)
 
Nachukia wanawake wanaotekeleza watoto wao zaidi ya wanaume wafanyao hivyo!!

Nwy we ni mmoja kati ya wachache wasioogopa majukumu na nnakupa hongera nyingi kwa hilo.Jitihada zote unazofanya kumlea mwanao ndo zinalipa hivyo kwa kukupa furaha isiyo na kipimo wala masharti!
Hongera tena!!

Happy birthday to your lil‘ girl.May she grow up to be admirable and be loved by many!

Huyo mwanamke hata akija kesho usimruhusu akachakachua akili ya mwanao!


Sure Lizzy,
Pamoja na maisha yanatusumbua,
Mtu unaweza kujiuliza ubinadamu na unyama wa watu wengine.
Mungu anaendelea kumjalia furaha huyu, na ananijalia baraka tele,
Ili niweze kumlea bila kikwazo chochote, atakuwa binti mkubwa mwenye akili nyingi.
Ahsante sana Lizzy kwa kujua tupo pamoja katika hili, umenizidishiaa nguvu na moyo.
 
journe i see it is getting better and better... nimependa the whole story
nimependa the fact kwamba the baby is soo young with a father as a single parent
maana in this case tushazoea it is always the mother, nimependa the fact you
are proud of her and you love her saaana... I am proud of you and impressed pia.


To your baby... Happy birthday baby gal, may you be one of the future

ladies who will make positive impact in this world of today

:flypig:and may you forever be Blessed by The Almighty GOD.:flypig:



Hii wala sio nzuri nilikuwa najaribu kuifanya iwe fupi sana,
Ili nisimkere Lizzy, matokeo yake nimeacha vitu vingi sana!
Anyway, ahsante sana kama umeipenda na kwa kunitia moyo.
Huyu Malaika yupo hapa, ni mzuri sana jamani zaidi ya Mamake,
Ninaraha sana mwenzio.
Karibu leo jioni kwa kuchezea nae keki!
Kwa uweza wa Mungu, nitafika naye mbali..
 
Hongera sana kwa mwanao kutimiza umri. Mwanao atajivunia kuwa na baba kama wewe..........Happy Birthday Malaika!!

Mheshimiwa Katavi!
Ahsante sana kiongozi.
Sherehe ya binti yangu naona imehudhuruwa na watu wakubwa sana.
Nafurahi tupo pamoja, binti yetu Malaika hajambo kwa dua zako mkuu.
 
Leo ni siku ya kuzaliwa binti yangu wa pekee (mpaka sasa) mpendwa sana!

Kwa mpaka sasa katika maisha yangu, huyu kiumbe ndio kitu kikubwa sana cha mafanikio yangu, na ndio sababu pekee inayonifanya napambana na ndio msingi wa furaha na mafanikio mengine.
Anatimiza miaka mitatu (3), nipo mimi na yeye tu!

Ilianza hivi.....!

Miaka minne iliyopita.

Kuna maeneo hapa mjini dar, unaweza kupata muono wa bahari ya hindi vizuri sana, hapo ndio utatambua utamu na uzuri wa bahari hiyo vilevile maisha.

Golden Tulip Hotel ni miongoni mwa maeneo hayo, najua yapo mengi na wewe unayajua!

Ilikuwa ni ratiba ya mimi na vijana wenzangu wa uswazi, kwamba kila mwisho wa mwezi tunachagua kiwanja kimoja ambapo tunaenda kubadili mandhari (kusafisha macho)

Wakati tupo hapa, eneo la "Maasai pub" stori za hapa na pale huku tuk-enjoy mawimbi yanavyopiga.... haikuchukua mda mwingi kabla sijajua kuwa huo muonekano wa bahari ya hindi na uzuri wake havikuwa na maana tena mbele ya huyu binti aliyepita hapa mbele yetu mda si mrefu.

Ni cashier. Toka nilivyomuona, akili ikawa ishanihama wala sikutaka kupoteza tena muda na kushangaa uzuri wa-view ya bahari ya hindi.

Wakati tunaondoka, nilimpitia pale counter nikamuuliza kama anaujua wimbo wa "All 4 One" unaitwa "As beatiful as You"
Akasema anaujua! Nikamwambia walimtungia yeye...... akacheka, nikachukua namba yake ya simu, mahusiano yakaanza.
Nyuma ya msichana mzuri sana, kuna tabia usiyoitarajia na itakushangaza (nzuri au mbaya)
Ilichukua miezi miwili nikawa nje ya Dar, then akawa ana mimba ya "Malaika"

Kwa bahati mbaya sana, mahusiano hayakudumu (stori nyingine) ila tulichoumba kilidumu.
Akajifungua "Baby girl".... Kabinti kangu ka kike my first born, raha sana!
Sababu sikuwa dar, hivyo baada ya kumuona tu nilirudi huko na mawasiliano ya mara kwa mara pia nilimuunganisha na familia yangu.
Baada ya miezi 6 ya umri wa mtoto, sikuamini nilivyomkuta mwanangu.... mtoto kama katoka Somalia ati ndio "kabemendwa" hivyo. Na alikuwa kishamuachisha ziwa.

Basi bibi yake hapa (Mama yangu) akasema inabidi mtoto abaki naye ili amshughurikie LISHE.
Inaonekana hiyo ndio ilikuwa ahueni ya huyo "shosti" maana toka siku hiyo binti (Mama mtoto) hadi leo hii wala hajatia pua yake hapa! Kamuacha mtoto.

Leo anatimiza miaka 3.
Mtoto lazima awe na mtu wa kumuita Mama, kadiri anavyokuwa shangazi yake mkubwa (dada yangu) ndio amemchagua kama Mama yake.
Tumeamua kumuacha tu aendelee hivyo sababu kwake aunt ndio anaziba pengo la Mama kimalezi, japo anachanganya na sisi tunavyomuita Bibi yake (Mama yetu) Mama, so na yeye anamwitaga Mama kwa kukosea.
Kiukweli sitamani Mama yake arudi kwa mda huu sababu nadhani itamchangnya zaidi mwanangu.

Nachukua wasaha huu kumtakia heri ya siku ya kuzaliwa, Mungu ambariki sana na amzidishie hekima, akili na azidi kuwa mtoto mzuri.
Sanasana Mungu awabariki wakina Baba wote. (Kwa niaba yangu binafsi)
Pia awabariki wakina Mama wote (kwa niaba ya bibi yake na shangazi zake)

Mungu awabriki watoto wote wa Tanzania

Mungu ampe hekima na busara tele bintiyo katika ukuaji wake.
 
Leo ni siku ya kuzaliwa binti yangu wa pekee (mpaka sasa) mpendwa sana!
Kwa mpaka sasa katika maisha yangu, huyu kiumbe ndio kitu kikubwa sana cha mafanikio yangu, na ndio sababu pekee inayonifanya napambana na ndio msingi wa furaha na mafanikio mengine.
Anatimiza miaka mitatu (3), nipo mimi na yeye tu!

Ilianza hivi.....!

Miaka minne iliyopita.

Kuna maeneo hapa mjini dar, unaweza kupata muono wa bahari ya hindi vizuri sana, hapo ndio utatambua utamu na uzuri wa bahari hiyo vilevile maisha.

Golden Tulip Hotel ni miongoni mwa maeneo hayo, najua yapo mengi na wewe unayajua!

Ilikuwa ni ratiba ya mimi na vijana wenzangu wa uswazi, kwamba kila mwisho wa mwezi tunachagua kiwanja kimoja ambapo tunaenda kubadili mandhari (kusafisha macho)

Wakati tupo hapa, eneo la "Maasai pub" stori za hapa na pale huku tuk-enjoy mawimbi yanavyopiga.... haikuchukua mda mwingi kabla sijajua kuwa huo muonekano wa bahari ya hindi na uzuri wake havikuwa na maana tena mbele ya huyu binti aliyepita hapa mbele yetu mda si mrefu.

Ni cashier. Toka nilivyomuona, akili ikawa ishanihama wala sikutaka kupoteza tena muda na kushangaa uzuri wa-view ya bahari ya hindi.

Wakati tunaondoka, nilimpitia pale counter nikamuuliza kama anaujua wimbo wa "All 4 One" unaitwa "As beatiful as You"
Akasema anaujua! Nikamwambia walimtungia yeye...... akacheka, nikachukua namba yake ya simu, mahusiano yakaanza.
Nyuma ya msichana mzuri sana, kuna tabia usiyoitarajia na itakushangaza (nzuri au mbaya)
Ilichukua miezi miwili nikawa nje ya Dar, then akawa ana mimba ya "Malaika"

Kwa bahati mbaya sana, mahusiano hayakudumu (stori nyingine) ila tulichoumba kilidumu.
Akajifungua "Baby girl".... Kabinti kangu ka kike my first born, raha sana!
Sababu sikuwa dar, hivyo baada ya kumuona tu nilirudi huko na mawasiliano ya mara kwa mara pia nilimuunganisha na familia yangu.
Baada ya miezi 6 ya umri wa mtoto, sikuamini nilivyomkuta mwanangu.... mtoto kama katoka Somalia ati ndio "kabemendwa" hivyo. Na alikuwa kishamuachisha ziwa.

Basi bibi yake hapa (Mama yangu) akasema inabidi mtoto abaki naye ili amshughurikie LISHE.
Inaonekana hiyo ndio ilikuwa ahueni ya huyo "shosti" maana toka siku hiyo binti (Mama mtoto) hadi leo hii wala hajatia pua yake hapa! Kamuacha mtoto.

Leo anatimiza miaka 3.
Mtoto lazima awe na mtu wa kumuita Mama, kadiri anavyokuwa shangazi yake mkubwa (dada yangu) ndio amemchagua kama Mama yake.
Tumeamua kumuacha tu aendelee hivyo sababu kwake aunt ndio anaziba pengo la Mama kimalezi, japo anachanganya na sisi tunavyomuita Bibi yake (Mama yetu) Mama, so na yeye anamwitaga Mama kwa kukosea.
Kiukweli sitamani Mama yake arudi kwa mda huu sababu nadhani itamchangnya zaidi mwanangu.

Nachukua wasaha huu kumtakia heri ya siku ya kuzaliwa, Mungu ambariki sana na amzidishie hekima, akili na azidi kuwa mtoto mzuri.
Sanasana Mungu awabariki wakina Baba wote. (Kwa niaba yangu binafsi)
Pia awabariki wakina Mama wote (kwa niaba ya bibi yake na shangazi zake)
Mungu awabriki watoto wote wa Tanzania


dah pole
km naona vile ambavyo unawish siku ya leo ungesherehekea na mama mtu lakin ndo ivo tena si kila mwanamke ni mama....

ajui wala hathamini uwepo wa kiumbe chake...

congrats kwa mama na ant kwa kumsaidia malaika wetu

sherehe wap?
sema naweza nkavunja yangu nkakujoin..pole mshkaji wangu dah
 
The Best Thing You Ever Did Together ni kumleta Malaika duniani!..Mwambie Malaika anasalimiwa na Malaika mwenzie:)))

Hongera sana kama mzazi kwa malezi, kwa upendo na pia roho ya kumsamehe mama wa mtoto wako kwa aliyokutenda!..You make a very proud father!!!..I salute you!!
 
dah pole
km naona vile ambavyo unawish siku ya leo ungesherehekea na mama mtu lakin ndo ivo tena si kila mwanamke ni mama....

ajui wala hathamini uwepo wa kiumbe chake...

congrats kwa mama na ant kwa kumsaidia malaika wetu

sherehe wap?
sema naweza nkavunja yangu nkakujoin..pole mshkaji wangu dah

Jamani Rose!
Hapo kwenye red, sio kweli kabisa hata kidogo.
Huyo mwanamke ni pasua kichwa mbaya, mtata yaani havumiliki, ndio hatukuweza ku-work out our thing!
Ahsante sana,
Sherehe ni hapo hom tu na Bibi yake na mashosti zake, pia nitampeleka kupiga picha Mayfair.
Karibu sana 1980
 
Hii wala sio nzuri nilikuwa najaribu kuifanya iwe fupi sana,
Ili nisimkere Lizzy, matokeo yake nimeacha vitu vingi sana!
Anyway, ahsante sana kama umeipenda na kwa kunitia moyo.
Huyu Malaika yupo hapa, ni mzuri sana jamani zaidi ya Mamake,
Ninaraha sana mwenzio.
Karibu leo jioni kwa kuchezea nae keki!
Kwa uweza wa Mungu, nitafika naye mbali..


hahaha.... nimshindwa hata kusoma maneno vizuri baada ya kukuta your weakness is Lizzy... ngoja niisome upya narudi...lol
 
Nakupa hongera sana wababa wachache wanaweza kukubali kuchukua majukumu hayo
endelea kumpatia malaika malezi bora na upendo usioisha
Namtakia malaika siku njema ya kuzaliwa
Mungu amlinde na kumjalia baraka tele


 
Mbona wengi mnammwagia sifa kama vile yeye ndiye anayemlea mwanaye au mimi sielewi maana ya kulea. Mimi nilivyomuelewa ni kuwa anampenda sana mwanaye (Hapa anastahili hongera zake za kumwaga) lakini amesema wazi kuwa mwanaye analelewa na mama yake kwa kushirikiana na dada yake (ambao ni bibi na shangazi wa mtoto respectively).
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom