Huyu mwanamke inapoelekea nitampiga nifungwe bure

Hakuna kitu kigumu kama kumshauri mtu kuhusu mapenzi. Broh wewe tuliza kichwa na moyo, alafu jiulize ni kitu gani unataka. Huwezi fanya uhamuzi wowote wa busara ukiwa high ( na hasira).

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana mkuu kwa yote yaliyokukuta
achana naye huyo binti lakini kunywa pombe na kununua malaya sio njia nzuri jaribu kuludi kwa mungu utakaa sawa na utapata mwanamke mzuri na utayasahau yote
 
Pole Sanaa Jimmy
Nakushauri jaribu kutafuta mwanasheria umueleze hili jambo huenda atakushauri kiundani zaidi....ili baadae isije kukuletea shida maana kwa sasa unatawaliw na hasira zaidi kila unapomuona.....

Ila sisi wanawake ni pasua kichwa kwa kweli..
mwanasheria au mwanasaikolojia?
 
...."nikamuomba simu nikaweka namba ya demu nikakuta wako na jamaa flan,nikacheki status nyingi wakiwa wanapika pmj,"...

Hivi ikiwa Mimi Sina namba yako Ila wewe una namba yangu, Je, unaweza ku VIEW STATUS KWANGU...???

Sent using Jamii Forums mobile app

Kwenye whatsapp kuna option inauliza nani anaweza kuona status au profile picture. Ni settings tu mzee baba.
Who should view your profile?
Everyone
Contacts only
Selected
 
Yaani kama gunia la pili la mkaa huna sema nikuchangie. Ndugu wa maana na ambaye asingekusaliti ni huyo mama yako/yetu aliyelala tayari. Nasubiri jibu kama mkaa hautoshi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole kwa hesabu ya haraka hujapoteza zaidi ya mamilion kumi au zaidi na hata ingekuwa hvyo pesa hutafutwa acha kufikiria kufanya uhalifu huumpendi, hakupendi au huwezi gharama zake mwache
Wanaume pesa zetu ni za kuhonga ama kutunza familia usishangae hata Ukitoka jela girlfriend anaweza kukuuliza umeniletea zawadi gani baby?
 
Yawezekana amegundua amekosea, msikilize!
Wasikilize wazazi wake.
Samehe kisha fanya uamuzi.

Kwa jinsi ulivyokuwa ukishiriki masuala yote ya familia yake, sijasikia ni vipi wao walishiriki katika ugonjwa wa mama yako hata kumjulia hali Muhimbili. Mahusiano ya familia hizi mbili yalikuwaje?

Mimi naona bado una mapenzi makubwa na huyo dem na ndiyo maana unaona bora umdhuru.

Ushauri wangu: Tafuta siku, lala naye na uhakikishe ummalizie hasira zote. Then fanya maamuzi na muombe ayaheshimu na wote mkubaliane hivyo!
Maisha ni haya haya.. furaha ya mama yako alipolala si kukuona ukiwa mikononi na miguuni mwa malaya.
 
Nitofautiane na mtazamo wa wengi.

Mbona naona umasikini ndio adui yako!!
Tuambie ulitaka nani akutunzie mbunye wewe uwe unapunguzia mawazo kwa kuifiligisa?

Mbona binti kakwambia wazi hitaji la MATUNZO!! Unakwama wapi kuelewa?

Hajasema hakupendi! Kwa kudhihirisha hilo anaomba na mpaka kulazimisha vikao vya maridhiano.
Tafuta pesa we fundi gereji. Wanawake hawataki maelezo ya shida zako
 
Pole mkuu, ingekuwa ni mimi ningeshamnywa kisusio siku nyingi sana. Ila wewe usifanye hivyo.

Mpige marufuku ikiwezekana report hata polisi ili aache kukusumbua.

Akiendelea kuleta uwaki mchome hata vidagger vya mapaja akili imkae sawa.
vidagger nn?

All in all, mleta uzi pole sana kwa kumpoteza mama hakika kibinadam mlipambana wewe na ndugu zako ila Mungu akampenda zaid mama,

Kikubwa huyo fisi maji mripoti hata polisi, au hama mtaa let say kama unaishi kitangiri hamia hata igoma, nenda kapange huko uwe unaenda home tu kuwasalimia. Ukiona amekufata na huko bas atakuwa anahtaji umtoe au akutoe roho. Vilevile badilika mkuu, tafuta mwanamke jenga nae mahusiano weka nae malengo, wanawake hawalingani boss unaweza kupata wako wa maisha,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
48 Reactions
Reply
Back
Top Bottom