Ni hivi... Nimeajiriwa katika taasisi ambayo imepakana na taasisi nyingine karibu. Ndani ya taasisi yetu kuna Canteen ambapo huwa tunajipatia chai na chakula cha mchana. Sasa kwa siku za karibuni taasisi ya jirani wameajiwa watumishi wapya na huwa ukifika muda chai/kula hufika canteen iliyopo katika campus yetu kwa ajili ya kujipatia chochote.
Hivi karibuni nikiwa nimeenda kujipatia chai walitokea wasichana warembo wawili kujipatia chai na tokea hapo tumekuwa tukikutana almost kila siku. Bahati mbaya huwa nawaogopa/siwashobokei wanawake warembo sana kwani ni pasua kichwa. Mmoja wa hao wasichana ni mrembo kwelikweli, maji ya kunde, mrefu wa wastani, ana meno ya kung'aa, mnene wa wastani na chura la haja. Kweli kumuona tu nilihisi moyo kama unanitoka. nilimuangalia naye akaniangali kisha akatabasamu na kila mara hufanya hivyo ila hatujaongea
mwishoni mwa wiki jana nilivyoenda kunawa mikono baada ya kula bomba lilikuwa halitoi maji hivyo nikawa natumia jagi kunawia kwa shida kidogo. Aliniona akaacha kula akaja na kuninawisha. nilimshukuru kisha akaondoka. Niliondoka, muda wa kutoka kazini ulipofika nilitoka nikiwa na-drive, hamad nikakutana nae nikaamua kumpa lift. nilitazama mapaja yake nikajikuta hoi. nilimfikisha kwao, akanikaribisha ila sikuingia nikaondoka kwenda kwa mke wangu.
Jana naona hali imejirudia tena. wakati wa chai nilikutana nae akaniomba tukae wote. Alikuwa mcheshi sana akaniuliza kama nimeoa baada ya kunisikia nikiongea kwa simu nikamwambia ndio (ila hatujafunga ndoa). Ameniomba namba na kuahidi kunitafuta.
Inawezekana nae ananipenda wadau? Nipeleke majeshi?
Hivi karibuni nikiwa nimeenda kujipatia chai walitokea wasichana warembo wawili kujipatia chai na tokea hapo tumekuwa tukikutana almost kila siku. Bahati mbaya huwa nawaogopa/siwashobokei wanawake warembo sana kwani ni pasua kichwa. Mmoja wa hao wasichana ni mrembo kwelikweli, maji ya kunde, mrefu wa wastani, ana meno ya kung'aa, mnene wa wastani na chura la haja. Kweli kumuona tu nilihisi moyo kama unanitoka. nilimuangalia naye akaniangali kisha akatabasamu na kila mara hufanya hivyo ila hatujaongea
mwishoni mwa wiki jana nilivyoenda kunawa mikono baada ya kula bomba lilikuwa halitoi maji hivyo nikawa natumia jagi kunawia kwa shida kidogo. Aliniona akaacha kula akaja na kuninawisha. nilimshukuru kisha akaondoka. Niliondoka, muda wa kutoka kazini ulipofika nilitoka nikiwa na-drive, hamad nikakutana nae nikaamua kumpa lift. nilitazama mapaja yake nikajikuta hoi. nilimfikisha kwao, akanikaribisha ila sikuingia nikaondoka kwenda kwa mke wangu.
Jana naona hali imejirudia tena. wakati wa chai nilikutana nae akaniomba tukae wote. Alikuwa mcheshi sana akaniuliza kama nimeoa baada ya kunisikia nikiongea kwa simu nikamwambia ndio (ila hatujafunga ndoa). Ameniomba namba na kuahidi kunitafuta.
Inawezekana nae ananipenda wadau? Nipeleke majeshi?