Huyu mwanajeshi wa JWTZ ana misifa anaporusha ndege za kivita

Mdakuzi mkuu

JF-Expert Member
Dec 27, 2016
212
719
Za jion jamani.

Kuna afisa mmoja wa JWTZ kambi ya pale Kibaha maili moja,ana misifa sana anaporuhusu ndege za kivita kupita chini chini kabisa ya usawa wa nyumba za watu.

Anafanya kitendo hiki makusudi kabisa.

Siku moja akiwa bar Kibaha maili moja akasema:-
."Kesho nitazipitisha ndege hizo chini kabisa,nitawapigia cm nikianza kuziruhusu zikatize hapa Kibaha maili moja".

Baada ya hapo akachukua namba ya mmojawapo.

kesho yake mida ya saa 3 asubuhi,tukasikia muungurumo mkubwa sana wa ndege mbili zilizopita kwa kasi ya ajabu zikiwa chini chini kuelekea kikosi cha JWTZ kule Msata. Baada ya muda mfupi,akapiga simu:-

"mmeziona ee??,hapo nimezielekeza kwenda kutua Msata.Zitarudi kesho"

Aache misifa ya kuungurumisha ndege karibu na watu atakuja kutumaliza aisee...
 
FB_IMG_1483690901272.jpg
tupo nao tunakula selfie tu
 
Za jion jamani.

Kuna afisa mmoja wa JWTZ kambi ya pale Kibaha maili moja,ana misifa sana anaporuhusu ndege za kivita kupita chini chini kabisa ya usawa wa nyumba za watu.

Anafanya kitendo hiki makusudi kabisa.

Siku moja akiwa bar Kibaha maili moja akasema:-
."Kesho nitazipitisha ndege hizo chini kabisa,nitawapigia cm nikianza kuziruhusu zikatize hapa Kibaha maili moja".

Baada ya hapo akachukua namba ya mmojawapo.

kesho yake mida ya saa 3 asubuhi,tukasikia muungurumo mkubwa sana wa ndege mbili zilizopita kwa kasi ya ajabu zikiwa chini chini kuelekea kikosi cha JWTZ kule Msata. Baada ya muda mfupi,akapiga simu:-

"mmeziona ee??,hapo nimezielekeza kwenda kutua Msata.Zitarudi kesho"

Aache misifa ya kuungurumisha ndege karibu na watu atakuja kutumaliza aisee...
Hahaa
 
Hii nchi mpaka wote akili zetu ziwe sawa dadadeki.Kuna siku hizi ndege zitatua kwenye hiyo bar.
 
Wacha wanajeshi wapate raha kidogo kazini. U.K kulikuwa na wanajeshi walikuwa wanaenda na helicopter kununua nyama ya kuliwa manyumbani mwao
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom