G4rpolitics
JF-Expert Member
- Jul 29, 2015
- 4,335
- 5,184
Nadhani watumishi wote wa serikali mshahara wao unajulikana, lakini inapokuja mtu mmoja anatoa misaada ambayo ipo nje ya mshara wake, inaleta uwalakini. Mtu huyu amekuwa akifanya kazi nzuri sipingani na hilo, ni mtumishi ambaye kiwango chake kinajulikana kwa mwezi kama wakuu wa m*** wengine. cha kushangaza ukimuangalia bado ni kijana mdogo ambaye ni majuzi juzi tu ameingia serikalini ingawa ana kinga na namba one.
Hana biashara kama akina Mo ya kusema kuwa hela zake anazivuna kutoka huko.
Sitamtaja jina ila ametangaza tena baada ya Taifa Stars kushinda jana atampa golikipa milioni kumi, sina chuki na hilo la kuhamasisha, ni vizuri sana kufanya hivyo lakini katika fungu gani hizi hela unazogawa gawa unazitoa? Asante kwa kujitolea kuwatibu wagonjwa tofauti, kuwatolea michango kwenda kutibiwa ndani na nje ya nchi, kuhamasisha katika michezo, tena nia yako ni ya kuigiwa ila mkuu pato lako ni lipi?
Mbona wenzako ambao ni wakuu wa *****kama wewe huko mi*** kwao hawatowi misaada kama hiyo, na tunajua mishahara yenu ni sawa sawa. Wabunge, Mawaziri, Wafanyabiashara wote hawana kapu la hizi hela la kutoa misaada kama hii. Nisiwachoshe la msingi huyo mheshimiwa, na mtumishi mkuu, anatoa pesa wapi za kutoa misaada ni kodi zetu au...?
CC: BAK, Mshana jr, Tindo.
kumbe huwa anaisoma jf...thank you jf ujumbe umemfikia mlengwa.
UPDATE:- 18/09/2019 Tarehe hii ya leo nashukuru mtumishi huyu kuja na majibu mepesi kuwa
-ana marafiki wengi wanaomchangia hivyi yeye akiwa amekaa nao hata wanakunywa kahawa huwa anachomekea kuomva misaada, ya kuwasaidia watu wenye shida zao, lkn protocol ya utumishi wa umma inasemaje kuhusu kupokea zawadi kwa mtumishi wa umma?
-mbna hizo zawadi huwa anapewa kimya kimya? ni ngapi anatangaza na kuweka wazi? niishie hapo kwanza.....
Hana biashara kama akina Mo ya kusema kuwa hela zake anazivuna kutoka huko.
Sitamtaja jina ila ametangaza tena baada ya Taifa Stars kushinda jana atampa golikipa milioni kumi, sina chuki na hilo la kuhamasisha, ni vizuri sana kufanya hivyo lakini katika fungu gani hizi hela unazogawa gawa unazitoa? Asante kwa kujitolea kuwatibu wagonjwa tofauti, kuwatolea michango kwenda kutibiwa ndani na nje ya nchi, kuhamasisha katika michezo, tena nia yako ni ya kuigiwa ila mkuu pato lako ni lipi?
Mbona wenzako ambao ni wakuu wa *****kama wewe huko mi*** kwao hawatowi misaada kama hiyo, na tunajua mishahara yenu ni sawa sawa. Wabunge, Mawaziri, Wafanyabiashara wote hawana kapu la hizi hela la kutoa misaada kama hii. Nisiwachoshe la msingi huyo mheshimiwa, na mtumishi mkuu, anatoa pesa wapi za kutoa misaada ni kodi zetu au...?
CC: BAK, Mshana jr, Tindo.
kumbe huwa anaisoma jf...thank you jf ujumbe umemfikia mlengwa.
UPDATE:- 18/09/2019 Tarehe hii ya leo nashukuru mtumishi huyu kuja na majibu mepesi kuwa
-ana marafiki wengi wanaomchangia hivyi yeye akiwa amekaa nao hata wanakunywa kahawa huwa anachomekea kuomva misaada, ya kuwasaidia watu wenye shida zao, lkn protocol ya utumishi wa umma inasemaje kuhusu kupokea zawadi kwa mtumishi wa umma?
-mbna hizo zawadi huwa anapewa kimya kimya? ni ngapi anatangaza na kuweka wazi? niishie hapo kwanza.....