Barikiel
JF-Expert Member
- Feb 2, 2014
- 403
- 401
Kama kichwa cha habari kinavyo jieleza hapo juu. Niliwahi kuwa na mahusiano na Dada mmoja kumbe alikua na mwanamme mwingine lakini hakuniambia kabla nilivyo ji ingiza ndo akaniambia ana bwana na in Dereva wa mabasi. Akaniambia yule bwana amekaa nae mda mrefu ameshindwa kumjaza mimba. Akaniambia nikibeba mimba tu namkimbizia Frenk. Jina siyo halisi, kweli tukaenda kupima afya tukaendelea na maisha sisi tuko Mwanza Frenk yupo DSM. Kweli baada ya mwezi tu, kitu kikatinga mwanamke kanitoroka kimya kimya kampelekea Frenk mimba. Frenk kalea mimba hadi mtoto, nimejaribu kuwasiliana na huyu Dada lakini imeshindikana nimeongea na Mama mkwe nae ananitukana. Naombeni msaada wa mawazo nifanyeje nimpate mwanangu. Au nisubiri mtoto ajitambue nimfuate mwenyewe? Mtoto yupo darasa la kwanza sasa hivi. Nairudia hii mada Mara ya pili. Jamani matusi sivyo naomba ushauri. Nawakilisha