Hawa hata kitabu cha Imaam Ibn Kathir hawana.Ndo kitu ambacho anashindwa kukielewa huyo..
Uthibitisho lazima atuambie kutoka katika vitabu vya İbn kathir, na sio Google..
Mpaka sasa ameshindwa kutuletea huo uthibitisho..
Ukisoma tafsir ya Ibn Kathir imeweka maoni yote wazi na athari yenye ngu ni ile ya swahaba Ibn Abbas,ambayo imewataja Sadiq,Saduq na Shalum.
Lakini imaam akaonyesha ya kuwa hao wanazuoni walioutja mji huo wa Antioki hawana uhakika.
Swali lingine ni je hao mitume kina Paulo walitumwa na Yesu au Allah ? Ukisoma aya inaonyesha ni Allah na wao wanadai wametumwa na Yesu. Haya maswali hawawezi kujibu.
Lingine ni kuwa aya inaonyesha dhahiri hao mitume walitumwa kabla ya Musa,ndiyo maana mji husika na wstu wake ukaangamizwa. Ndiyo maana baada ya Kuondoka Musa hapakuwa na maangamizo mengine ya halaiki kwa watu walio kataa imani ya kweli. Sasa swali ni je lipi linalo wafanya waseme Bulus ni Paulo ?