Mi nadhani alale jehanamu na achomwe Sanaa na moto maaana hay mauzauza ya ccm eye ndo ameleta
Ulikuwepo wakati wake?
Hana mpinzani?
Waliompinga aliwasweka ndani ama kuwapoteza ama walikimbia nchi.
Unamjuwa Kambona? Unamjuwa Sheikh Takadiri? Unamjuwa aboud Jumbe?
Uliza walifanywa nini na huyo!
mmmh uchumi alifeli kwa kweli na kutuwekea utawala wa kiimla na hili DUDE BAYA kabisa linaloitwa CCM, na kutuulia nchi yetu pendwa TANGANYIKA na kutuletea nchi ya kusadikika inayoitwa Tanzania.
Nilikkuwepo wakati wake. Namfahamu Oscar Kambona na Mkewe Flora Kambona (aliyepata kuwa mwenyekiti cha chama chao). Namfahamu Aboud Jumbe. Nafahamu walichofanywa na nafahamu walichofanya. Nafahamu pia sababu za waliokimbia kuamua kukimbia.
Jibu langu kwako,
"Tatizo ni udogo wa mawazo, Umasikini wa mawazo ni umasikini kweli kweli. Anaweza akaja tapeli akakwambia hii uliyoshika si almasi ni kichupa tu ila ya kwangu ndiyo almasi. Basi we ukasema "Nipe" halafu ukatoka unashangilia kama zuzu......!!!" - Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Burito.
RIP Mwalimu. A visionary Leader, A writer. A Farmer. A Teacher. A patriotic Citizen. Our Child. Father of the Nation.
Katika watatu tu wa Mwanzo nilowataja umewafahamu wawili tu? Jee huyo watatu?
Kweli, inabidi umsifu. Kwani inaelekea ni mmoja wa wale waliofaidika na uDikteta wake na hukuwa na hisia za mamilioni aliowatesa, maelfu aliowauwa na maelfu kama si malaki aliowadhulumu.
Laiti ungekuwa unatazama na upande wa pili wa shillingi.
Leo, kila mTanzania, kwa njia moja ama nyingine analia kivyake. Anenyimwa haki mahakamani, anaekuwa harassed na polisi anaelilia ufisadi anaekosa haki za msingi wa masomo na afya.
Jee hujui au hutaki kujuwa kuwa hiyo ndio legacy ya Nyerere.
Kang'atuka kaiacha nchi inanuka kwa uozo, haina fedha bank, mpaka kaichoma mto benki kuu kabla ya kung'atuka, kachoma moto makao makuu ya wizara ya mambo ya ndani, kabla ya kung'atuka. Kaacha nchi haina hata diesel ya kuendeshea magari machache yaliokuwepo, seuse ya kuendesha viwanda. Kaacha watu, majority, hawana elimu hawana matibabu, hawana hata kanda mbili za kuvaa kwendea chooni.
Hiyo ndio legacy? Au yote hayo hukuyaona kama ulikuwepo?
Mwacheni tu apumzike, yaani nachukia wale wanaofikia kiasi cha kumwita saint