Huyu fundi wa hizi sarakasi ni nani?

Huyo ni gwajima huwa ni mhuni kabla hata ya ugomvi na bashite kala wanakondoo sana na hyo video alirekodi mwenyewe acheni kumtetea na kujificha eti kachafuliwa yeye ni rijali na sio hanisi
Kwa vile wew mwanamke umekiri kuwa GWAJI ni RIJALI mimi ni nani hata nipinge?ntajuaje....@Extrovert
 
Weee Mzee inji hii ukiiwaza sana utachanganyikiwa, kuna kitu kinaitwa agenda denie hiyo walifaulu sana mataifa ya kijamaa, na kitu hii inafanya kazi sehemu nyingi hasa kwetu na siku wananchi wakistuka utaona moto wake, ndio maana inaitwa bandika bandua na ujue wako well calculated maaana tozo chali, katiba chali, mbowe atapewa dhamana na kuachiwa kisela maana marekani wamewavua nguo, maisha yanaendelea na hii ndio bongo ambayo kabla ya kuingia lazima upite maili moja
😂😂
 
Baada ya rais mstaafu Jakaya Kikwete kurudi tena madarakani kwa mara ya pili alifanya jambo ambalo lilishutumiwa sana.. Alikusanya watendaji wa serikali karibia wote na kwenda kufanya semina elekezi kwenye hotel ya kifahari ya Ngurdoto mkoani Arusha.

Kiuhalisia maudhui ya semina naweza kusema kwamba hayakupewa kipaumbele zaidi ya watu kula bata kwa raha zao...Hakika usemi wa kazi na bata ulipata umaarufu sana kipindi kile.

Ukiachana na mapungufu ya ile semina lakini watendaji wale walitoka pale na kitu kikubwa sana! Kule kuwakutanisha nje ya taratibu zao za kawaida za majukumu ya kila siku kulisaidia sana kuwajenga na kuwaleta pamoja na kuwafanya kuwa kitu kimoja
Semina elekezi hizi ziliendelea kila wakati kwa kipindi chote cha utawala wa JK.. Hawa watendaji walipata nafasi ya ku relax, kupunguza uchovu,kutoa stress kufahamiana kwa karibu nje ya taratibu za kazi.

Baada ya Kikwete kumaliza muda wake alimkabidhi kijiti marehenu hayati Magufuli....Huyu alifuta kila kitu... Si senina elekezi wala makongamano makazini... Maono yake hayakuwa ya JK! Watendaji lile bata la JK likakoma na kuanza kutimiza majukumu yao kwa pressure kubwa..na hata kama kulikuwa na semina au kongamano kukawa tena hakuna bajeti za vyakula na kumbi za kukodi..mambo yaliishia idarani tena kwa maji na biskuti ikawa sasa sio KAZI NA BATA tena bali HAPA KAZI TUU.

Haya mambo ya sasa ya watendaji kupishana kauli ama kila mmoja kuongea lake ni matokeo ya kauli mbiu ya hapa kazi tuu.. Na wala hayakuanza sasa..huu ni mwendelezo tuu toka enzi za mwendazake.

Huu mgongano wa kauli na kulifungia gazeti la chama kwa siku saba ni matokeo yaleyale ya kukosekana mawasiliano, umoja na kujitambua kwamba nani anapaswa kufanya nini kusema nini na wapi! Nikikumbuka matamko ya watendaji wakati wa Magufuli nabaki tu kucheka.

Hakuna aliyekubali kuwa chini ya mwingine bali kila mmoja alijitahidi kutoa tamko kali kuliko mwenzake ili kumfurahisha bwana Mkubwa.

Sakata la mchungaji Gwajima aliyeichokonoa serikali vilivyo limechukua sura mpya baada ya serikali kupitia waziri wa afya kutoa amri/agizo la kukamatwa Gwajima mchungaji na jeshi la polisi ambalo ni organ ya serikali

Mkuu wa jeshi la polisi bila fikra na tafakuri alipoulizwa kuhusu kukamatwa Gwajima alisema hajapata wito rasmi wa maandishi toka serikalini, lakini hata hivyo akaenda mbali na kutoa ushauri na maelekezo.

Kwamba hata akipokea oda ya kumkamata Gwajima mchungaji basi wataangalia kama kuna jinai na kama basi ipo jeshi la polisi litashauri wamalizane kwa njia ya mazungumzo!

Kwanza mzee Sirro ajue kwamba hili si suala la ndugu wawili mtu na shemeji yake hata atoe ushauri 'wamalizane wenyewe' hili ni la kiserikali.

Pili mzee Sirro alikuwa kwenye nafasi nzuri kabisa kujibu kuwa wanafanga mawasiliano na wizara au na waziri ..! Full stop! Mengine yote aliyoongea hayakuwa mahali pake! Je wakati wa kayafa angefanya hivi?

Mawasiliano ya watendaji yanafanyika mitandaoni na bila kuwasiliana kwanza..yaani ni kama kuna kuoneshana ubabe na ujuaji!
LAKINI ukiachana na hayo yote kuna tatizo kubwa huko ndani, waziri ni mdomo wa rais, akisema waziri ni agizo la serikali lenye ridhaa ya rais na organs za serikali zinachotakiwa kufanya ni KUTEKELEZA KWANZA!

Kuna dharau juu ya wanawake inajitanabaisha hapa na kuna kikundi ndani ya mamlaka hakikubali kuongozwa na wanawake! Je Gwajima na Sirro ni sehemu yao?
Sirro ameshaona kesho anataka akapumzike amechoka. Wala hakuna jingine uwenda ameumia kubeba mambo yana muharibia ustaafu wake. Mimi huwo ndio muono wangu. Nisawa na RC wa Mwanza alivyo fanya makusudi kusema watu waje na mabango hata ya matusi akatenguliwa akarudi kwao bila wala kelele. Unajuwa wakati mwingine sio lazima kuwa kiongozi. Kinacho endelea kwa sasa ni kikundi cha watu fulani kuwaaribia wenzao kwa jina la jamuhuri. End
 
Weledi wa jeshi letu ungekuwa hivyo basi mahabusu zetu zisingefurika watuhumiwa wala mahakama zetu zisingekuwa na msururu wa kesi zisizo na kichwa wala miguu

Two wrongs doesnt make a right. Jeshi kuwa limefanya hivyo sio justification ya kuendelea kufanya vile vile ili tu kukidhi matakwa fulani. Tunahitaji mabadiliko kwa jeshi letu na labda mabadiliko haya yameanzia kwa Gwajiboy, hivyo Siro yuko sahihi.
Gwajigirl anafahamu kabisa taratibu za kuadabisha wahalifu, so kama anaona kuna uhalali wa hoja yake aende moja kwa moja akafungue kesi dhidi ya Gwajiboy.
Wakati mwingine tumewatwisha sana misalaba yetu jeshi la polisi na kuliacha likilaumiwa kila kukicha..
 
@Mshanajr nakumbuka ulikuwa mmoja wa wadau wa ANAUPIGA MWINGI ila now days na naona akili zimeanza kurudi.
Ni kweli kabisa na bado nina msimamo uleule na wala si kuwa zilinipotea na sasa zimerudi...
Iko hivi kimsingi na kiuhalisia Mamaa yuko njema sana na nia yake ni thabiti sana lakini kazungukwa na nje nzige na tandu... Kwa wote mnaoona kabadilika kuna mengi nyuma ya pazia hamyajui ila muda utasema
 
Mimi kwa mawazo yangu sidhani jinsia imekuwa sababu ingawa ikawa nayo inachangia.
Huyu bwana alikuwa akitoa matamko na yalikuwa yanatoka juu, sasa anaona yanatoka chini,

Huyu Siro alikuwa na lugha za kejeri akijua analindwa na nguvu za juu sasa hakuna tena cha juu bali ni ukweli na uwazi.

Vitisho alivyokuwa anavitoa kwa upinzani bado vinakubalika sawa ila hakuna nguvu za juu zimetajwa kama akina DC aliyeko lupango alivyokuwa anawatisha wapinzani na watu baki.

Siro bado amelewa kileo cha kubembelezwa na mwanakwendazake ili azidi kulindwa na majeshi yote ya nchi hii hata helkopter nasikia zilikuwa zinaruka juu ya msafara kumlinda aliyetangulia bila kumiminiwa risasi kama Lisu.
 
Two wrongs doesnt make a right. Jeshi kuwa limefanya hivyo sio justification ya kuendelea kufanya vile vile ili tu kukidhi matakwa fulani. Tunahitaji mabadiliko kwa jeshi letu na labda mabadiliko haya yameanzia kwa Gwajiboy, hivyo Siro yuko sahihi.
Gwajigirl anafahamu kabisa taratibu za kuadabisha wahalifu, so kama anaona kuna uhalali wa hoja yake aende moja kwa moja akafungue kesi dhidi ya Gwajiboy.
Wakati mwingine tumewatwisha sana misalaba yetu jeshi la polisi na kuliacha likilaumiwa kila kukicha..
utali Suluhu ni katiba mpya sio the Gwajis n their dramas
 
Sirro ameshaona kesho anataka akapumzike amechoka. Wala hakuna jingine uwenda ameumia kubeba mambo yana muharibia ustaafu wake. Mimi huwo ndio muono wangu. Nisawa na RC wa Mwanza alivyo fanya makusudi kusema watu waje na mabango hata ya matusi akatenguliwa akarudi kwao bila wala kelele. Unajuwa wakati mwingine sio lazima kuwa kiongozi. Kinacho endelea kwa sasa ni kikundi cha watu fulani kuwaaribia wenzao kwa jina la jamuhuri. End
Kinacho endelea kwa sasa ni kikundi cha watu fulani kuwaaribia wenzao kwa jina la jamuhuri. End
 
Anatoa huduma za mwili na roho sio?
Lakini tuzipime hoja zake tusijifiche kwenye mapungufu yake...
Gwajigirl alichemka kuikana cirona na leo yuko mbele kushawishi tuchanjwe, ahamishwe Wizara
Huu ubini wa Gwajima una shida nadhani kwenye kizalia
 
Back
Top Bottom