Huyu Baba Mkwe atanivunjia Ndoa

Elli

Platinum Member
Mar 17, 2008
55,180
85,339
Huyu Baba Mkwe simuelewi kabisa, saa sita au saba usiku eti anampigia simu bintie, kha, umelala usingizi unashtuka simu inaita au mtu anaongea na simu, haya mwenzetu nani huyo usiku huu, oooh Baba anatusalimia!!! Saa hizi!!!

Haya kuna siku kaja, mmmh niko zangu job wife yeye karudi mapema ile narudi namkuta Mkwe kavaa pensi tu miguu iko juu ya sofa mgongo uko chini ya sakafu kwenye jamvi, bintiye yuko sofa ya jirani wanapiga story!!!!!! Sina mawazo mabaya but huyu dingi jamani na hii mikao yake mbele ya binti yake!!! Yaani umevaa pensi halafu miguu juu, kweli si maeneo yote hatarishi yanakua exposed???

Mara oooh wewe Suzy wewe (Ni Housegirl-sio jina lake halisi) nataka nikuoe, nataka Mama fulani (mke wangu) nimtafutie Mama mdogo, naona wewe unafaaa....kwakweli ananinyima raha bhana, yaani mtu aje kwenye himaya yako halafu anaongea huu mchuzi huu, ahaaaaa

Haya kama kawaida yake, muda wa kuondoka lazima ampetipeti mke wangu, mara ooh baba fulani wewe pumzika tu subiri mama nanihii anisindikize.....mmmh haya basi Mama msindikize kwa gari baba hadi hapo kituoni, eti hapana ngoja tutembee tu, kuanzia saa moja kasoro hadi saa mbili ndio anarudi kumsindikiza baba, distance ya dakika kumi hadi kituoni????

Jamani, jamani sihisi chochote but huyu Dingi huyu nitakuja kumkata kidevu, Nice weekend,
 
Jamani, baba wa watu anammisi mwanae. Wako karibu na anataka waongee masaa yote. Kuhusu nikao watu tofauti wana tabia tofauti. Ni kama tamaduni. Ila hiyo tabia ya kumtania hgelo mchunie atajistukia. Akisema hivyo usichangie kitu, fanya kama hujasikia. Ataona aibu.
 
Napata shida sana kuupokea ushauri wako, subiri siku nitamwambia mwanae kuwa sipendi tabia ya mzee
Jamani, baba wa watu anammisi mwanae. Wako karibu na anataka waongee masaa yote. Kuhusu nikao watu tofauti wana tabia tofauti. Ni kama tamaduni. Ila hiyo tabia ya kumtania hgelo mchunie atajistukia. Akisema hivyo usichangie kitu, fanya kama hujasikia. Ataona aibu.
 
Hahahaa...kwani wewe unahisi nn?? Usiogope bana huyo ni daddy's girl tu..
 
Ha ha haaaa!Labda wenyewe wanahisi wanaishi kizunguu maana wabongo kwa ku-copy hatujambo! Vp unamuonaje mkeo jinsi anavyo-behave akiwa na wewe? Uzungu mwingi au ni kama kawaida tu hajaathiriwa sana na uzungu? Maana labda kwao amelelewa hivyona ndivyo wanavyoishi?
 
yawezekana amezoea sana kukaana njinsia ya kike kuliko njinsia ya kiume mpotezeee hawezi kufanya unacho kihisi babaa
 
Mpwa, hii michezo ya kizungu hii waishie kuichezea huko huko kwao sio kwangu, my wife wala hua haonyeshi kushtuka, yaani she is so ok but hua nakosa raha sana, kweli nakosa raha sana, mimi nadhani tujifunze kutenganisha malezi na tabia zetu tuwapo mahali pengine
Ha ha haaaa!Labda wenyewe wanahisi wanaishi kizunguu maana wabongo kwa ku-copy hatujambo! Vp unamuonaje mkeo jinsi anavyo-behave akiwa na wewe? Uzungu mwingi au ni kama kawaida tu hajaathiriwa sana na uzungu? Maana labda kwao amelelewa hivyona ndivyo wanavyoishi?
 
Ndo RAHA YA KUOA WATOTO WA MASAKI HIYOOOO!!!!!!!! Dady! Dady! Dady! 24/7, Hata mkijamba humo ndani uatsika Dady!!!! Sio sie FATHER! Akirudi WOTE MNAKAA MIKAO YA KUJENGA TAIFA!!!!!!!!! Akiondoka ndo uuuuuuuuuh! Mnahema! FATHER KAMA CHLOROQUINE!!!!! Ukiolewa unasema THANKS GOD! Nitarudi nyumbani KUTEMBEA!!!!!!!! Kwako haji ngoooo! Usipomuibukia kumpa HI! Baaaaaaass!!!

Think on the postive side, siku hamna HELA YA MBOGA, Dady will JUMP IN TO HELP ASAP!!!!!!!!
 
No no Mpwa, Masaki wapi bhana, kawaida tu, halafu hio positive side unayozungumza hio ni afadhali nilale njaa kuliko eti Mkwe anipe pesa ya mlo...si ndio sasa nitaanza kuhisi yale ninayohisi?? Nionee huruma jamani
Ndo RAHA YA KUOA WATOTO WA MASAKI HIYOOOO!!!!!!!! Dady! Dady! Dady! 24/7, Hata mkijamba humo ndani uatsika Dady!!!! Sio sie FATHER! Akirudi WOTE MNAKAA MIKAO YA KUJENGA TAIFA!!!!!!!!! Akiondoka ndo uuuuuuuuuh! Mnahema! FATHER KAMA CHLOROQUINE!!!!! Ukiolewa unasema THANKS GOD! Nitarudi nyumbani KUTEMBEA!!!!!!!! Kwako haji ngoooo! Usipomuibukia kumpa HI! Baaaaaaass!!!

Think on the postive side, siku hamna HELA YA MBOGA, Dady will JUMP IN TO HELP ASAP!!!!!!!!
 
Nakumbuka kuna uzi humu wa baba kutembea na binti yake na mme wake akashtukia.Hebu naomba tuache kulemba maneno utafute huo uzi halafu changanya na zako.Inawezekana ilikuwa chakula ya mzee.Samahani lakini
 
Madingi wa siku hizi wanakula kuku na mayai yake!! Mwambie asije tena huyo mkwe.
 
Haahaaa kuna baadhi ya madingi tz yamekengeuka, mkuu kuwa makini, hapo kama hajamtafuna basi anataka kumtafuna!

Mwambie mkeo kwasauti kiume kuwa ni MARUFUKU kuchekacheka na baba yake, MARUFUKU baba yake kumpigia simu usiku labda kuwe na msiba hata hivyoo akitaka kupiga basi apige kwenye namba yako!

Kuna kaugonjwa umekalea wewe mwenyewe mkuu, HATA siku moja usimrusu mkeo amsindikize mkweo!

Labda nikufahamishe, kwa imani yangu ya Kirasta Fari na mila ya kabila langu la Kizanaki ni kuwa mwanamke akishaolewa mamlaka na udhibiti WOTE unakuwa kwa mumewe,

Wazazi wake chochote wanachotaka kumwambia au kukifanya kwa binti yao (mke wangu) ni lazima wapate kibali kwangu!

Mkuu badili mfumo wako wamaisha, MPIGE marufuko mkweo kuja hapo kwako bila sababu maalumu na akihitaji kuja kuongea na mwanae aombe kibali kwako na ikiwezekana shinda zake zote azifikishe kwako na wewe ndio utaamua kumfikishia mkeo!

NB

Ieleweke pia wazazi WANGU nao wakitaka kuongea na mimi hasa mama yangu, nilazima aanze kwanza kuongea na mke wangu kisha aoombe kuongea na mimi

Tambua kuwa huyo ni MKEO wako wewe, wewe ndio mwenye mamlaka ya mwisho iwe mbinguni ama duniani! Ukisema NO na iwe NO kweli!

Ukicheka na NYANI utavuna mabua mkuu!
 
usinidanganye kirahisi hivyo, basi background yao ni mbovu if that is what you mean
Acha mawazo potofu,wababa wengine wako karibu na mabinti zao, nadhan tatizo ni background yako tofauti na ya waifu wako....
 
Yericko Nyerere umetoa wazo zuri kweli, na-admit kosa, nitabadilisha mfumo kwa nia njema kabisa, maana kinachoniudhi huwa hata Mama Mkwe anapiga simu lakini sio night kihivyo na huwa akija bibi hua na msimamo, ni mkali na huwa hapendi kabisa mambo ya kijinga, thanks nimekuelewa mpwa
 
Last edited by a moderator:
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom