Huwezi na Hutoweza Kuongea / Kuandika Kiswahili fasaha

Faida gani tutapata tukitumia hizo herufi za kiarabu?

Post yangu namba 50 ina majibu ya hilo, ngoja nikuwekee tena hapa uisome:

quote_icon.png
By FaizaFoxy
Umenielewa kabisa point yangu na mpaka hapo juu nimeweka mfano wa Wazungu Waalimu wa awali wa Kiswahili wa vyuo vikuu huko nje walivyoona huo umuhimu wakujifunza Kiswahili kwa kujuwa maandiko na matamshi ya Kiarabu, sijuwi hawa ndugu zangu ambao hawalioni hilo na wanalipinga wanapinga nini haswa?

Mimi kuileta hii mada nna maana yangu pana sana, ni juzi juzi tumesikia kuwa Tanzania imetowa maamuzi kuwa lugha ya kufundishia masomo yote iwe Kiswahili. Ni jambo jema sana hilo. Ni wakati muafaka tukatambuwa kuwa inabidi na watu wafundishe kukijuwa Kiswahili fasaha kwa matamshi ya Kiarabu ili wawe na ufasaha na kina cha kuelewa maana ya maneno mengi ya Kiarabu yaliyomo kwenye Kiswahili.

Itakuwa ni rahisi sana kwa mwanafunzi kuwa na ufasaha wa hali ya juu na au Mwalimu atakuwa na kina cha kufundisha ikiwa tu atakielewa Kiswahili kwa herufi za Kiarabu kuliko yule ambae atabaki na kukielewa kwa herufi za Kilatini tu.

Leo hii utashangaa mtu anakuja na jina la kiajabu ajabu la kutunga hata halina kina wala halina uhusiano wowote na ubaridi wala historia eti "jokofu", wakati neno hilohilo kwa Kiswahili fasaha lipo "barada", ambalo lina historia, lina kina na lina uhusiano na ubaridi.

Nnawashauri Waalimu wa Kiswahili, wa kuanzia shule za msingi mpaka juu kabisa huko, waanze kujifundisha herufi za Kiarabu na waone wakisha zijuwa kuandika na kuzisoma herufi hizo watavyoona raha kufundisha Kiswahili kwa ufasaha na kina zaidi.

Fikiri.
 
FaizaFoxy, miongoni mwa maprofesa nguli wa Kiswahili wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, pengine ni wawili tu ninaowafahamu ambao wanafahamu Kiarabu cha kubabia: M. Mulokozi na Abduli Hamisi Mtajuka... Wengine wote wamesoma tu mahusiano kati ya lugha hizi mbili.

Ziada ni kuwa, zipo lahaja za Kiswahili ambazo hazina maingiliano kabisa na Kiarabu, kama vile Kimakunduchi na Kingwana kinachosemwa Kongo Mashariki.

Uhusiano wa kulazimisha kati ya Kiarabu na Kibantu unapingwa kwa kuwa sio Waarabu wote wanaweza kusikia walau msamiati mdogo wa Kiswahili, na kinyume chake vivyo hivyo.

NB: Kiswahili ni Kibantu hasaa!

"Nnadiriki" au Ninadiriki" ndio kiswahili fasaha?

Hapo UDSM zamani alikuwepo nguli wa kiswahili aliyemaster kiarabu, kingereza na kiswahili chenyewe; sasa hivi ni marehemu akiitwa Mzee Pera!!!
 
Wewe mama unajaribu kujipendekeza kwa waarabu ili iweje?......

1.Kiswahili sio Kiarabu na haitotokea kua kiarabu kamwe ..pia kiarabu sio kiswahili.


Tuanze na hilo namba moja.

Ni wapi uliona nimeandika kuwa Kiswahili ni Kiarabu au Kiarabu ni Kiswahili?

Kasome post namba moja para ya kwanza uone nilichokiandika uje na majibu ya hilo na si kupindisha maneno na kutaka kunilisha maneno ambayo si yangu.

Kabla hatujaenda la pili kwanza tuhakikishe hili umelielewa na limekuingia.
 
Maalim FaizaFoxy weye mchokonozi sana!

Kila lugha ina ustaarabu wake, halikadhalika kwa kiswahili pia! Japokuwa ustaarabu wa kiswahili una mahusiano sana na lugha ya kiarabu. Kuna baadhi ya pahala, ni muhali kueleza jambo kiufasaha na kupata maana ya kile kikusudiwacho ikiwa msomaji si mahiri na mjuvi wa lugha ya kiarabu.

Kwa hiyo nakubaliana na wewe kwa kiasi FULANI japo pia ujuzi wa lugha nyinginezo ni silaha nzuri ya kumfanya mtu akiongee kiswahili na kueleza maana ya mambo mengi kwa kiswahili vizuri zaidi kuliko asie mjuzi.
 
Last edited by a moderator:
Kwangu mimi lugha ni kwaajili ya mawasiliano ili kuelewana. Kama nakuelewa na unanielewa basi huo ufasaha utabaki kwa wanaofundisha tu.
Ukitaka kuamini ufasaha hauna tija angalia bubu anavyowasiliana na bubu mwenzie au asiye bubu, pia angalia kiziwi anavyo wasiliana na watu wa aina mbalimbali. Hapo ndio utajua umuhimu wa lugha ni kuwasiliana na masuala ya ufasaha yapo kwaajili ya kuongeza ajira tu.

Ha haaa haaaa! Mkuu SaaMbovu umenikumbusha shuleni .... lugha ni sauti za nasibu zenye kubeba maana mawasiliano ... Duh! Kitambo sana hiyo.
 
Last edited by a moderator:
mwisho wa siku conclusion ni kwamba Kiswahili ni Kiswahili hakijawahi kuwa Kiarabu wala Hakijawahi kuwa Kibantu, ili ujuwe kiswahili fasaha unaitaji kujifunza kiswahili fasaha, si kiarabu kama mtoa maada anataka kukuaminisha, na kwanini kiarabu na si kibantu? mwisho wa siku kiswahili kitabaki kuwa kiswahili haijalishi kimetokana na Lugha ipi. na kiswahili fasaha kinapatikana katika kamusi ya kiswahili tu.
 
Dah, umeshindwa kutofautisha kiswahili fasaha na kiswahili sanifu? kiswahili fasaha ni kile ambacho watu wakizungumza wanaelewana na kiswahili sanifu kinafata sheria zote kuanzia matamshi, sentensi, maneno na nk, watanzania wengi wanaongea kiswahili fasaha
 
ukishaweza kuonge au kuandika kiswahili fasaha halafu inatokea nini ?

Hahaha,Itakurahisishia kupata kazi katika nchi kubwa za dunia ya kwanza kama France,Britain,USA,Italy,Japan etc. Ambapo kiswahili kinazungumzwa sana kama the leading language.
 
Niliposema mtu anahitaji kusoma kitabu sikutaraji mtu atatumia mantiki ya ajabu kama nilyoiona hapa. Vitabu vilivyorejelewa havitoi mwanga hata kidogo juu ya ushahidi wa nasaba ya Kiswahili. Ilikuwa kama vile mtu ametuletea marejeleo juu ya kuunda ndege iwe kama mwongozo wetu juu ya utengenezaji wa pikipiki.
Baada ya hapo nikaona pia mtu mmoja aitwaye Ntaganzwa ambaye ameandika kifupi tu kwa ushahidi wa msamiati tu. Hawezi hata kurejelea mjadala huu ambao wataalamu wengi tayari wameufanya. Hiki alichokiandika Ntaganzwa hakistahili hata kupata heshima ya kurejelewa kwenye mjadala ulio makini. Natilia mashaka na mtu ambaye anatumia hii kama ndiyo msingi au ushahidi wa hoja. Naweza hata kumsaidia Ntaganzwa kwamba kuna orodha ndefu sana ya msamiati uliotokana na Kiarabu ambao Bwana Bosha amechapisha kwenye tasnifu yake hapo UDSM.
Barbarosa kaeleza mambo mengi kwa ufasaha. Na kama unafuatilia hoja zake na uwazi wa fikra, hapana shaka yoyote utaona mshiko wa hoja zake. Baada ya hapo niseme tena kwamba kigezo cha nasaba ya lugha si idadi ya msamiati uliotoka katika lugha nyingine. Ingelikuwa hivyo, tungelisema kwamba Kiingereza kimetokana na Kifaransa au Kilatini.
Kigezo kikuu cha nasaba ya lugha ni muundo wake. Napenda kutoa mfano mmoja wa ngeli za Kibantu. Mfumo wa ngeli ni kitu cha kipekee katika lugha za Kibantu. Ni mfumo unaokipambanua Kiswahili kama lugha ya Kibantu. Kusema kwamba asili ya Kiswahili ni Kiarabu, ni kusema pia kwamba Kiswahili kimekopa mfumo wa ngeli. Kwa lugha yoyote ambayo si ya Kibantu, haiyumkiniki kwamba itaweza kukopa mfumo mzima huo na upatanisho wake wa kisarufi. Kitu hicho hakijapata kudhihirika katika isimu.
Magwiji wengi wa lugha za Kibantu, mathalani Guthrie (1967-71), Meinhof (1939) Massamba (2012-I believe) wanatumia Kiswahili kama mfano wa muundo wa Kibantu. Lugha hazikopi hivyo. km. M-toto m-dogo m-moja a-meanguka. Ki-kombe ki-moja ki-dogo ki-mevunjika. nyumba-ni p-angu p-amechafuka.
Kuna mifano mingine mingi ya kimuundo. Inahusu pia viambishi vingi vinavyofanya kama mtungo wa mofimu vya kitenzi. km. a-li-ye-tu-gong-an-ish-i-a. Uchangamano huu wa mofolojia ni tofauti kabisa na wa Kiarabu na hauwezi kuwa matokeo ya kukopa bali ni sehemu ya nasaba yake.
Muundo wa maneno ya Kiarabu unafuata mfumo wa mizizi ya konsonanti tatu: ktb, drs, hml, nk. Unayanyambulisha kwa kuchomekea viambishi na si mchangamano wa kimtungo kama wa Kibantu. Hatuuoni kabisa muundo wa Kiarabu katika Kiswahili. Ajabu iliyoje kama Kiswahili kimetokana na Kiarabu kisioneshe ushahidi wa muundo wa Kiarabu.
Utaona kwamba sina hofu yoyote ya kutumia maneno ambayo ninajua yanatokana na Kiarabu. Lugha zote hupeana maneno. Sijui Kiarabu ingawa nimepata kupitia makala na maandishi mbalimbali yahusuyo sarufi na isimu ya Kiarabu. Tena, lugha nyingi zinakuwa na majina wanayopewa na watu wengine. Na huo si ushahidi kwamba hiyo ndiyo asili ya lugha hivyo. Asili ya Afrikaans ni Kidachi na sio kwa vile kina jina hilo basi asili yake hasa ni Afrika.
 
Nikuchote akili kwani wewe ni msukule.

Unabwabwaja na kuhororja lakini bado hujaja na cha maana na inaonesha hata mada hukuielewa.

Ngoja nikuanzie taratiiiiib, maana unakuja na utumbo mreeefu lakini mada unaipiga chenga:


Hii ni sentensi ya kwanza kwenye mwanzo wa hii mada, nieleze unachokipinga hapa ni nini?

Kiswahili ni lugha ambayo imetokana na Kiarabu na Kibantu na maneno mengine machache yaliongezeka kidogo kidogo kutoka lugha zingine za Afrika, Uropa na Asia.
uko sahihi (kiasi kidogo sana) illa kwa mawazo yangu sentensi hii ilitakiwa isomeke hivi
kiswahili ni lugha ya kibantu yenye maneno toka lugha ya kiarabu na maneno toka lugha nyingine za afrika, europa na asia.
maana utafiti unaonesha 60% ni lugha za kibantu, 30%kiarabu na nyingnezo 10%

nimeshangaa sentensi yako kuanza na lugha yenye 30%, ukaipa daraja sawa na lugha yenye 60%.
kiswahili ni kibantu, waarabu waliwahi kufika pwani mapema sana na ndio sababu wameiathiri sana lugha ya kiswahili
 
uko sahihi (kiasi kidogo sana) illa kwa mawazo yangu sentensi hii ilitakiwa isomeke hivi
kiswahili ni lugha ya kibantu yenye maneno toka lugha ya kiarabu na maneno toka lugha nyingine za afrika, europa na asia.
maana utafiti unaonesha 60% ni lugha za kibantu, 30%kiarabu na nyingnezo 10%

nimeshangaa sentensi yako kuanza na lugha yenye 30%, ukaipa daraja sawa na lugha yenye 60%.
kiswahili ni kibantu, waarabu waliwahi kufika pwani mapema sana na ndio sababu wameiathiri sana lugha ya kiswahili

Kwanini hukuanzisha mada yako na kuyasema hayo?

Huo utafiti ulifanywa na nani na lini?

Eti umeweza kuweka asilimia za utafiti wako ukashindwa kuweka asilimia za "upo sahihi".

Nikiwa sahihi ni either 100% nipo sahihi au 100% sipo sahihi.

Unajuwa maana ya sahihi? unajuwa kuwa hilo neno ni la Kiarabu?

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
 
Kwanini hukuanzisha mada yako na kuyasema hayo?

Huo utafiti ulifanywa na nani na lini?

Eti umeweza kuweka asilimia za utafiti wako ukashindwa kuweka asilimia za "upo sahihi".

Nikiwa sahihi ni either 100% nipo sahihi au 100% sipo sahihi.

Unajuwa maana ya sahihi? unajuwa kuwa hilo neno ni la Kiarabu?

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
haupo sahihi 100% uko sahihi 5% kwa kuhusisha kiswahili na kiarabu
ila kiswahili ni kibantu chenye maneno toka lugha ya kiarabu
 
haupo sahihi 100% uko sahihi 5% kwa kuhusisha kiswahili na kiarabu
ila kiswahili ni kibantu chenye maneno toka lugha ya kiarabu

Hilo neno "Kiswahili" linatokana lugha ipi?

Hilo neno "Bantu" linatokana na lugha ipi?

Shule uliyosoma ina matatizo, amma nipo sahihi 100% amma sipo sahihi 100%.

Its either black or white, no gray shades.
 
Jamani msitumie nguvu nyingi kubinya vitufe vya "keyboard" zenu ili kukidhi matakwa ya huyu jamaa mleta Uzi, hasa zaidi akiwa anataka mkubaliane naye. Muacheni aamini anachokiamini maana ndio chimbuko lake ana ameleleka huko. Ana ugonjwa moja ambao na yeye binafsi haja ujua kama anao unaitwa "OMANI"
 
FaizaFoxy;

Nafikiri wewe ndiyo unachanganya mambo na hili jambo ni rahisi sana!
Kiswahili SIYO Kiarabu (linguistically) na hakikutokana na Kiarabu na sababu ni hii, Kiarabu kiko kwenye Familia ya semetic/Afro languages na Kiswahili siyo Semitic languages na hakina uhusiano wowote ule na Semitic languages bali kiko kwenye familia ya lugha zijulikanazo kama bantu languages ambazo asili yake ni Afrika Magharibi Niger-Kongo!
Sasa kama ungesema Kisomali au Amharic (kiithiopia) ni Kiarabu hapo ningekuelewa kwa maana zote ni familia moja ya Hemitic langauages!

Sasa kama Kiswahili siyo sehemu ya semitic languages sijui hata hoja yako imebase wapi labda kama tunabishana kienyeji tu lkn siyo kitaalamu! Kwa maana Lugha zote Duniani zimepangwa kwenye makundi, na lugha zenye uhusiano mmoja ziko kundi moja sasa kama Kiswahili kingetokana na Kiarabu basi aidha Kiswahili kingekuwa ni semitic au kiarabu kingekuwa Kibantu ni rahisi kihivyo tu!

Hilo neno unalirudia sana, ni wapi niliandika Kiswahili ni Kiarabu?

Hebu nisome post namba moja.

Ukaleta habari zako sijuwi kuwa "Waarabu" walikuja wakakuta Wabantu, nikakuuliza i wapi hiyo historia inayoonesha Wabantu walikuja kwanza kabla ya Waarabu Afrika ya Mashariki? mpaka sasa umeshindwa kuonesha, sasa mimi nnakuuliza wewe? Jee unajuwa kuwa Wabantu wamekuja Afrika ya Masshariki? na unajuwa historia inatwambia wamekuja lini? ukipata majibu ya hayo, sasa niambie walimkuta nani ni Mwenyeji wa pwani ya Afrika Mashariki? kama haujuwi sema nikusaidie.

Hayo makundi uyasemayo si tatizo, hizo ni "classification" tu za utambulisho lakini si "static"" zipo "dynamic", nikikupeleka huko unapotaka kuelekea kwa haraka haraka ntakuchanganya zaidi na ndiyo maana kila ulipogusia hilo nimelipuuzia kwa kuwa huko mimi niko deep sana na ntakufikisha taratiibu tu, usiwe na haraka. Nnakupeleka huko huko lakini kwa namna zake ili somo lieleweke.

Mara kadahaa nimekwambia kuwa tatizo lako kubwa ni kuwa huijuwi historia na nnauhakika kuwa huna uelewa wa kianthropolojia, hususan kwenye mada inayoitwa "cross cultural studies", laiti ungalikuwa na uelewa japo kiduchu usingekuja na hizo "classification".

Ili somo likuingie vizuri, soma hapo nilipo "bold" halafu jaribu kujibu hayo maswali ili twende sambamba na uelewe kuwa Waarabu wapo kabla ya Wabantu hii pwani ya Afrika ya Mashariki.
 

Anaejiita hukumundo amechanganya sana majibu kwa watu tofauti mpaka tanabahi ya msimamo wake siielewi. Sijuwi hata hicho kitabu anachosema alimwambia nani akisome. Nimeshindwa kumjibu unless awe specific na majibu yake.

Kwa ufupi, dhanna ya kuazima/kukopa maneno nimeitolea ufafanuzi hapa awali na laiti angeipitia hii nyuzi kwa utaratibu angeliona hilo.
 
Last edited by a moderator:
kiswahili kimetokana na kiarabu na kibantu? kibantu ndio lugha gani? hakuna bantu language, kuna bantu speaking people, nikimaanisha kuwa kuna lugha ambazo zina muingiliano fulani na ambazo utakuta baadhi ya maneno yanaelekeana ingwawa yaweza kuwa machache sana kiasi kwamba uwezekano wa kuelewana kati ya makabila mawili yaliyo kwenye mkusanyiko wa bantu speaking people.

Kiarabu kama ilivyo kwa lugha nyingine kimechangia kiasi katika maneno ya kiswahili lakini haina claim kwenye kiswahili maana kuazima maneno kutoka kwenye lugha moja kwenda lugha nyingine ni kitu cha kawaida mno duniani

na kwa kuwa kiarabu sio oldest language under the sun then nacho kitakuwa kimeundwa na maneno kutoka katika lugha nyingine kwa hiyo hizo lugha inawezekana ndo zimechangia kwenye kiswahili kwa kupitia mkondo wa kiarabu.

ustaarabu kwa tafsiri ni "civilization" sasa nao hauwezi kuwa confined kwa watu au tabaka fulani..kitu kinachoitwa ustaarabu kwa mmanyema sio lazima kichukuliwe hivyo na m-Danish..bali kila jamii ya watu ina kipimo chao cha ustaarabu...kwa baadi ya watu cannibalism inachukuliw kama kipimo kikubwa cha ustaarabu wakati kwa wtu wengine watajudge kuwa ni barbaric deed!!!
 
Back
Top Bottom