Huo ni mtazamo wako; akili timamu za kuishabikia CCM tunazo lakini hatulazimiki kushabikia vitendo vyake ambavyo havipo kwa maslahi ya watanzania. Hatukatai kuna mambo mengi yamefanyika kinyume na matarajio ya wanaccm lakini je matendo hayo yanatulazimisha tuhame? Je iwapo tutahama na kwenda Chadema na hadithi ikijirudia tuhame tena? Ukweli CCM kama chama hakihubiri ubadhirifu wa mali za umma tatizo lilopo ni viongozi wetu ambao wamepewa dhamana ya kuendesha chama ndio wanaoleta matatizo. Tatizo siasa yetu imeingiliwa na watu wasio waadilifu hata huko Chadema wapo viongozi ambao tayari wameshajionesha ni si waadilifu wapo kwa maslahi binafsi; nafahamu fika mpo kwenye vugu vugu la kupenda huyaoni kama utahitaji nitakupa mifano hii.
Chama
Gongo la Mboto DSM
Chama
Gongo la Mboto DSM