Huwezi Kuua Maiti -Erick Shigongo

Duuh
SEHEMU YA 05...

Ghafla Meja Jenerali Lupilya akiwa amekata tamaa kabisa alisikika kitu kama mluzi ukipigwa pembeni yake
“Pswiiiiiiiiiiii!” Kufuatia mluzi huo Nzige wote wakasimamishwa zoezi lao la kula minofu yake! Mluzi mwingine tena ulifuata lakini katika mtindo tofauti kidogo! Kufuatia mluzi huo Nzige wote waliruka na kuondoka zao.

Meja jenerali Lupilya alipogeuza uso wake na kuangalia pembeni alikiona kibibi kizee kikitembea taratibu kuelekea mahali alipolala, Tembo wengi walikizunguka na mmoja wao alipomfikia alizungushia mkonga wake shingoni mwa Meja jenerali, alimnyanya na kuanza kumzungusha hewani, Lupilya alipiga kelele na kulia.

“Wiiiiii!” Bibi alitoa mlio mdomoni kwake na Tembo akamweka chini Lupilya, alikuwa akitoka jasho mwili mzima na mkojo ulimpenya! Tembo wote walikaa chini na kulaza vichwa vyao ardhini kama ishara ya kuonyesha heshima kubwa kwa bibi Nyanjige.

“I’m the queen of the forest who are you?”(Mimi ni malkia wa msitu wewe ni nani?)
“I’m ...ma...jor gene...ral Lupi...lya fro..m Tan..zania!”(Mimi ni Me...ja jene....rali Lupil....ya natoka Ta....nzania)
“Tanzania? From what tribe are you?”(Tanzania? Wewe ni kabila gani?)
“Su…ku..ma!” Alijibu Lupilya huku akilia na kutetemeka! Hakuamini kulikuwa na binadamu aliyekuwa na uamuzi mkubwa kiasi hicho mbele ya wanyama wa mwituni!

“Ule Nsukuma getegete?”(Wewe ni Msukuma kabisa?) Bibi Nyanjige alimuuliza meja kwa kabila ya Kisukuma, Lupilya alibaki mdomo wazi akishangaa.
“Ngh’ana gete mama! Nu bebe gashi uli wa Kukaya?”(Kweli kabisa bibi kumbe na wewe ni mtu na nyumbani!) Alijibu Lupilya huku akiendelea kulia machozi, mwili wake wote ulimuuma sababu ya kuliwa na Nzige, alipomwangalia mwenzake alikuwa kimya nyama zote hazikuwepo mwilini!Alibaki mifupa.

“Mnataka nini hasa nyinyi?” Bibi aliuliza kwa kiswahili.
“Nduhu mhayo mama! Nilekejage natalashogeja kabili!(Hakuna neno bibi nisamehe sitarudia tena) Meja Lupilya aliendelea kuongea kwa Kisukuma.
“Ongea kiswahili mpumbavu wewe! Unafikiri Kisukuma kitakusaidia HAPA?”
“Nisamehe bibi na mimi nilitumwa tu!” Lupilya alibadilisha lugha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom