NANDERA
JF-Expert Member
- Mar 18, 2014
- 2,024
- 2,486
Aisee nimeshindwa kusoma, ila natumai kuna kitu tu kilichotokea kikasababisha mkafarakana, kwa kifupi unatakiwa kujifanya mjinga tu na kurudi chini na kumuomba msamaha kama mzazi, wanasema mzazi hakosei hata kama ndio mwenye makosa.
Rudi chini muendee mtake radhi na ukiri kuwa kweli uliyofanya yalikuwa ni makosa ila bado nafahamu kuwa wee ni mzazi wangu nahitaji kukuomba msamaha baada ya kugundua kuwa nilichokifanya ni makosa. Hata kama hataonyesha kukusamehe kwa muda ule lakini tayari kuna kitu deep inside his heart kitakuwa kimemuingia. Tafuta wazee wenye busara ikiwa ni marafiki zake au ndugu ikiwezekana uwaeleze wakusaidie kumueleza mzee wako kwa kuwa umemuomba msamaha lakini hajaupokea.
Mwsho ni kwamba, mzazi ni binadamu kuna leo kuna kesho, akitangulia mbele za haki kabla hujamuomba radhi mapema YOU WILL BE A LOSER usikubali kuwa hivyo aisee. Ila pia kumbuka NAZI HAISHINDANI NA JIWE.
Nakutakia kila la heri aisee.
Shkamoo Mzaramo na asante kwa kunifurahisha. Walau umeonyesha kujali.😄😄