Huwa Rais anafikiria nini katika uteuzi wake?

Mimi mkuu wakti nipo Tanzania niliwahi kufanya kazi na kwa karibu sana katika level ya Mkoa na wanajeshi hawa Col Nsa Kaisi, Brig Mwakanjuki na vile vile nilipokuwa wizarani nilifanya kazi kwa karibu na Maj Gen Lupogo.

nakubali kabisa ukifanyakazi na hawa hakuna lele mama. maaagizo au maazimio yote yanawekwa katika time frame nao wanafatilia.

Sasa nikirudi kwenye ngazi ya wilaya. Nilikuwa nikiwa Mkoani unaona kabisa hao wanajeshi wa ngazi za wilaya wanafanya kazi zao kwa maelekezo toka juu.

Niliwapenda sana capt Nkoswe na wengine.

Mkuu nadhani hizo time frame hata utakapokuwa nazo kwenye mafile 1,000 kama utendaji wako ni mbovu huwezi kwenda kokote. Kazi za mezani kwa kalamu ni wengi wanaziweza hata wewe au hata mama yangu mzazi kule kijijini anaweza hizo.

Wakuu wa Mikoa na Wilaya wanajeshi walio wengi hawajishughulishi zaidi ya kushughulikia maagizo wanayopata kutoka Serikalini. Hilo kubali au kataa lakini lipo wazi.

Kipindi ulipokuwa Tanzania ni tofauti na jana, Kama ulikaa na hawa waheshimiwa basi una bahati sana, Na huenda hata kutumia Bunduki unaweza.

Unaweza kuwa mkali sana kwa mwanao wakike lakini kama ukali ule hauna tija yoyote waweza shangaa mwanao huyo akapata ujauzito na akajifungulia nyumbani kwako...

Unapo kuwa Kiongozi usisubiri tu kupangiwa au kupewa maelekezo kutoka juu, Bali jaribu kubuni jinsi ya kuwaongoza wale walio chini yako kutokana na hali ya mazingira ya uongozi uliyopangiwa..Unapo boronga anaye laumiwa si boss wako bali ni wewe..!
 
na perfomance nayo tuiweke wapi?
Mkuu, performance inategemea na commitment, uzoefu na nidhamu ya kazi.

Naamini kuwa wanajeshi wengi huwa na ujasiri kuliko raia wa kawaida, wanakuwa na nidhamu kutokana na mafunzo na mazoea ya muda mrefu (hivyo kuwa tabia yao) na pia huweza kusikiliza na kufuata maazimio/maagizo na taratibu za kazi zao kwa uwezo mkubwa zaidi. Hivyo, nadhani ni rahisi kwa kiongozi mwenye nia ya kufikia matokeo mazuri na kwa haraka kuamua kumteua mwanajeshi kushika madaraka katika nafasi ambayo kwa kiongozi huyo ni muhimu utekelezaji wake ukawa wa kiwango cha juu.

Vinginevyo pia, sidhani kuwa mwananchi wa kawaida ndie pekee anaeweza kuwa na performance ya juu na mwanajeshi kuwa kinyume chake. Pamoja na kuwa, kuna wananchi wengi wenye nidhamu na uwezo mkubwa wa kufanya kazi kama inavyotakiwa. Hivyo kuwafanya watu hawa wawili kutokuwa na tofauti kubwa kati yao.

Ieleweke pia kuwa sio wanajeshi wote wenye nidhamu, jitihada na uzoefu mkubwa. Ila kwa muundo wa taasisi yao, ni rahisi kuwajua wenye uwezo na wasio na uwezo kuliko kuchambua kutoka kwenye jamii ya wananchi wa kawaida.
 
ukweli ushaonyesha kuwa hawajui kitu inaitwa management an leadership especialy kwa civil activities,alizoea kupokea amri leo hii atakuwaje self starter? that means atapokea from above na kuimplement tuu basi!!
Sometimes, that is all that is needed to achieve best results.

Vile vile, ifahamike kuwa jeshini kuna uongozi na utawala ambao viongozi wake wamepata mafunzo mazuri sana. Na sia ajabu wakawa wamefuzu kuliko wengine wengi nje ya jeshi.

Inawezekana kwa kutokujua kwetu, tukadhani kuwa wanajeshi huwa hawapati mafunzo ya utawala/uongozi
.
 
NNali hakuwa mwanajeshi. Fuatilia vyombo vya habari huko Bongo.

Unamaanisha chombo hichi cha Habari?

JWTZ yamkana DC aliyewachapa walimu

2009-02-18 10:47:38
Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), limemkana aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Vijijini mkoani Kagera, Albert Mnali ambaye aliwachapa viboko walimu kuwa hajawahi kupitia mafunzo yoyote ya kijeshi.

Taarifa iliyotolewa na Idara ya Habari na Uhusiano Makao Makuu ya JWTZ jana ilisema, Mnali hajawahi kuwa afisa wa jeshi hilo wala kuwa na cheo chochote kama ilivyotangazwa na baadhi ya vyombo vya habari (siyo Nipashe).

Baadhi ya vyombo hivyo vya habari, viliripoti kuwa, Mnali alikuwa ni Kanali mstaafu wa JWTZ.

``JWTZ haijawahi kuwa na afisa mwenye jina na cheo hicho,`` taarifa hiyo fupi ilieleza.

Wakati huo huo, Ahmed Makongo kutoka Bunda anaripoti kuwa, Jeshi la Polisi wilayani humo, limezuia maandamano ya walimu yaliyolenga kupinga unyanyasaji wanaodaiwa kufanyiwa wenzao wa Wilaya ya Bukoba Vijijini na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo.

Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Wilaya ya Bunda, Francis Ruhumbika alisema maandamano hayo yaliyokuwa yafanyike juzi kuanzia asubuhi, yalishindikana kwa ajili ya kulaani kitendo kilichofanywa na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya huyo kuwachapa viboko wenzao wa shule za msingi.

Mnali alichukua hatua hiyo akidai kuwa ni watoro na shule zao zimekuwa zikifanya vibaya kitaaluma.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Kaimu Katibu wa CWT, wilayani Bunda, alisema maandamano hayo yaliyokuwa yafanyike juzi kuanzia saa 2:00 asubuhi, yalizuiwa na polisi baada ya kukatiwa kibali cha kuwaruhusu ili waweze kuandamana.

Ruhumbika alisema polisi wamemwandikia barua ya kuzuia maandamano hayo kwa maelezo kuwa, Rais Jakaya Kikwete, amelifanyia ka.zi suala hilokwa kumfukuza kazi.

Kwa barua hii ombi lako la kutaka kuandamana kama ilivyojieleza barua yako husika limekataliwa,`` ilisema sehemu ya barua hiyo iliyosainiwa na Afisa Upelelezi wa Wilaya kwa niaba ya Mkuu wa Polisi Wilaya ya Bunda.

Hata hivyo, Ruhumbika aliwaambia waandishi wa habari kuwa, hajatendewa haki ya kuzuia maandamano hayo kwa kuwa Katiba ya nchi inawaruhusu na kwamba yalikuwa siyo ya kufanya vurugu ni ya amani.


Naye Ofisa Elimu wa Wilaya ya Bunda, Yesse Kanyuma, alisema maandamano hayo hayana msingi wowote kwa kuwa Rais tayari amechukua hatua na kwamba kama walimu wangeandamana wangepoteza bure vipindi vya wanafunzi wanaowafundisha.
 
Mkuu nadhani hizo time frame hata utakapokuwa nazo kwenye mafile 1,000 kama utendaji wako ni mbovu huwezi kwenda kokote. Kazi za mezani kwa kalamu ni wengi wanaziweza hata wewe au hata mama yangu mzazi kule kijijini anaweza hizo.

Wakuu wa Mikoa na Wilaya wanajeshi walio wengi hawajishughulishi zaidi ya kushughulikia maagizo wanayopata kutoka Serikalini. Hilo kubali au kataa lakini lipo wazi.

Kipindi ulipokuwa Tanzania ni tofauti na jana, Kama ulikaa na hawa waheshimiwa basi una bahati sana, Na huenda hata kutumia Bunduki unaweza.

Unaweza kuwa mkali sana kwa mwanao wakike lakini kama ukali ule hauna tija yoyote waweza shangaa mwanao huyo akapata ujauzito na akajifungulia nyumbani kwako...

Unapo kuwa Kiongozi usisubiri tu kupangiwa au kupewa maelekezo kutoka juu, Bali jaribu kubuni jinsi ya kuwaongoza wale walio chini yako kutokana na hali ya mazingira ya uongozi uliyopangiwa..Unapo boronga anaye laumiwa si boss wako bali ni wewe..!

Mkuu labda nikukumbushe tu. Enzi zetu wakati ukimalza form six ilikua lazima upite JKT mwaka mmoja ka mujibu wa sheria.

Mimi nilipata bahati kubwa ya kupita JKT kambi ya Ruvu, enzi hizo chini ya Mkuu wa kikosi Col Meena, OC wangu alikuwa Capt Chota, RSM aliitwa Mwarobaini na , Sir meja alikua Ssgt Kitomali.

Ndani ya JKT pamoja na kujifunza ukakamavu vile vile tulifundishwa field craft (ujanja wa porini) na vile vile kutumia silaha, SRA, SMG na LMG. Hivyo nipo FIT kenye masuala ya silaha na mbinu za kijeshi.
 
I wish u had cofirmation maana linafana sana na ukweli!! nadhani ni bora wangetafutiwa ulaji mwingine kuliko huu maana sasa wanatupa shida sisi wananchi wanaotuongoza kwa kuboronga wanapogaiwa hizo nyadhifa muhimu za kuongoza mikoa na wilaya.
Ukiangalia wanajeshi hawajawahi kuongoza watu walio huru. Wamezoe kuongoza watu kwa AMRI siyo KUSHAWISHI. Wakija uraiani wanatumia amri watu wanagoma, sheria hamna ya kumfukuza mtu nchini kama wanavyofanya jeshini hakuna.wanabaki kukasirika na kuamua kutoshugulika.Yaani ni mzigo mkubwa kwenye almashauri hawa mabwana. wanajeshi wafundishwe fani mbali mbali wakistaafu waingie kwenye fani zao. Hivi ilivyo sasa hatuendelei. Wangeachia basi watu wenye elimu wawashauri basi lakini ni ving'ang'anizi
 
Mkuu nadhani hizo time frame hata utakapokuwa nazo kwenye mafile 1,000 kama utendaji wako ni mbovu huwezi kwenda kokote. Kazi za mezani kwa kalamu ni wengi wanaziweza hata wewe au hata mama yangu mzazi kule kijijini anaweza hizo.

Wakuu wa Mikoa na Wilaya wanajeshi walio wengi hawajishughulishi zaidi ya kushughulikia maagizo wanayopata kutoka Serikalini. Hilo kubali au kataa lakini lipo wazi.

Kipindi ulipokuwa Tanzania ni tofauti na jana, Kama ulikaa na hawa waheshimiwa basi una bahati sana, Na huenda hata kutumia Bunduki unaweza.

Unaweza kuwa mkali sana kwa mwanao wakike lakini kama ukali ule hauna tija yoyote waweza shangaa mwanao huyo akapata ujauzito na akajifungulia nyumbani kwako...

Unapo kuwa Kiongozi usisubiri tu kupangiwa au kupewa maelekezo kutoka juu, Bali jaribu kubuni jinsi ya kuwaongoza wale walio chini yako kutokana na hali ya mazingira ya uongozi uliyopangiwa..Unapo boronga anaye laumiwa si boss wako bali ni wewe..!

Hakika ungefanya kazi Serikalini ungeyajua haa. Kwa kukudokolea kidogo . Kila wilaya inajipangia malengo yake na kuwakilisha mkoani. Mkoa unaweka malengo na kupeleka Serikalini. kazi ya serikali ni kuainisha na kutoa malengo kwa kila mkoa. Mkoa ukipata maelekezo toka Serikalini basi ndipo mnapoyapangia mikakati kimkoa kwa kushirikisha wilaya.

Lazima ujue Mkuu wa wilaya kazi yake kubwa ni kusimamia maagizo yote ya Serikali yanayoletwa wilayani kwake. Kazi hii haitaki ubunifu wala nini ewe ni kutekeleza mipango ya Serikali kuu tu kwa wilaya yako.

Sasa sijui kama kuna shule yoyote inayohitajika hapo zaidi ya kupata amri na kuzitekeleza amri hizo. Sasa wanajeshi ndio wenyewe katika kutekeleza amri hizo.

katika Ngazi ya wilaya na mkoa kazi inayohitaji taaluma ni Mkurugenzi mtendaji.
 
Mimi nadhani hakuna tatizo lolote kwa Rais kuteua wanajeshi kushika madaraka yoyote katika nchi isipokuwa kama kufanya hivyo anakuwa amevunja sheria.

Wanajeshi (kama wananchi wengine wowote) wanayo haki ya kushiriki katika shughuli zozote ambazo wanaonekana kuweza kushiriki. Uwezo wao, nidhamu yao na hata mapenzi tu ya Rais yanatosha kuwa sababu ya kutosha kuhalalisha uteuzi wao.

Sioni sababu kwa kweli ya kufikiri wanajeshi hawana haki ya kuteuliwa kushika nafasi wanazoteuliwa kuzishika. Kwani kwa kuwabagua kwa namna hiyo, tunaweza kuanzisha matabaka ya wenye haki na wasio na haki ya kushika madaraka mbalimbali katika nchi.

Nadhani swali la muhimu ni kwanini wasiteuliwe kushika madaraka hayo, wakati wengine huteuliwa kwenye nafasi hizo?
Uwezo wao ndo ni mtoahoja kahoji iweje mikoa au wilaya zinazongozwa na hawa mabwana maendeleo ni duni.Nafikiri hilo ndo ungejibu.akusema raisi kavunja katiba.ata akichagua mwananchi yeyetu hajavunja katiba vile vile
 
Mkuu labda nikukumbushe tu. Enzi zetu wakati ukimalza form six ilikua lazima upite JKT mwaka mmoja ka mujibu wa sheria.

Mimi nilipata bahati kubwa ya kupita JKT kambi ya Ruvu, enzi hizo chini ya Mkuu wa kikosi Col Meena, OC wangu alikuwa Capt Chota, RSM aliitwa Mwarobaini na , Sir meja alikua Ssgt Kitomali.

Ndani ya JKT pamoja na kujifunza ukakamavu vile vile tulifundishwa field craft (ujanja wa porini) na vile vile kutumia silaha, SRA, SMG na LMG. Hivyo nipo FIT kenye masuala ya silaha na mbinu za kijeshi.

Sasa mkuu unaona je ukienda ku volunteer kule Afghanistan , Maana jamaa wanawapelekesha speed sana majeshi ya UN.Hahaaaaa!! Nimekupata mkuu hakuna shida ila bado hali ni mbaya kwa hawa wa heshimiwa, Nadhani wanafuata mtiririko kutoka juu kabisa. Utakuwa umenielewa.!!
 
na perfomance nayo tuiweke wapi?
Good hiki ndo kigezo.Mapenzi ni kwa Tanzania siyo rais.Na isitoshe alichaguliwa na watu wengi wenyemapenzi naye siyo hao makamanda. Rais tunamweshimu na kupokea order na kutekeleza kwa kufuata sheria zetu basi.
 
Sasa mkuu unaona je ukienda ku volunteer kule Afghanistan , Maana jamaa wanawapelekesha speed sana majeshi ya UN.Hahaaaaa!! Nimekupata mkuu hakuna shida ila bado hali ni mbaya kwa hawa wa heshimiwa, Nadhani wanafuata mtiririko kutoka juu kabisa. Utakuwa umenielewa.!!
Ku volunteer siwezi ila kama kuna pesa BISMILLAH nipo tayari.......joke
Hakika kwa sie tuliepata bahati ya kupitia JKT kuna mengi tumejifunza lakini kubwa zaidi ni uvumilivu,ujasiri na ukakamavu.

Shukrani sana nimekupata.
 
Mhh vigumu kujua yaani inatisha, hata hiyo "power of reasoning" ya hao wateule, inatia huzuni na mashaka!!
 
pia nahisi sababu nyingine kubwa ni kuhofia mapinduzi ya kijeshi kwani hawa watu wakiwa mtaani bila kazi na kama unavyojua mafao yao kuwa ni kidogo sana hivyo kuwa rahisi kushawishika na hatma yao huo nio kuchukua nchi kaka
 
Mkuu labda kwa kuongezea (mimi sina data), hawa wanajeshi wanaopewa hivi vyeo ni wale kama JK au kuna waliostaafu jeshini then wakapewa position hizi. Maana isije kuwa wanavyeo juu lakini ni wale waliojiondoa kipindi ilipopitishwa sheria.

Vyovyote iwavyo hakuna jipya kwao zaidi ya kuleta kasheshe. Lakini pia kuna ile ya kuwa wanapenda kuwaweka kwenye mikoa ya pembezoni ili kukabiliana na uharifu sijui kama ina ukweli au la. Maana huo uharifu umejaa tele. Mara, Kagera (wamemtoa huyu kawekwa kikampeni zaidi), Kigoma,Mtwara kwa baadhi mikoa niifahamuyo.
 
pia nahisi sababu nyingine kubwa ni kuhofia mapinduzi ya kijeshi kwani hawa watu wakiwa mtaani bila kazi na kama unavyojua mafao yao kuwa ni kidogo sana hivyo kuwa rahisi kushawishika na hatma yao huo nio kuchukua nchi kaka

Kwahiyo kwa kuwa teuwa kama Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa ni njia moja wapo ya kuzuia ushawishi wa kuchukua nchi na si wapo kule kiutenda je sio ?
 
pia nahisi sababu nyingine kubwa ni kuhofia mapinduzi ya kijeshi kwani hawa watu wakiwa mtaani bila kazi na kama unavyojua mafao yao kuwa ni kidogo sana hivyo kuwa rahisi kushawishika na hatma yao huo nio kuchukua nchi kaka

kwa hiyo ukionekana utakuwa na madhara kweny emaslahi ya wenye nchi unapozwa kiaina ahaaaa!!!....on our expense...poor wananchi wa newala!!!

Hii njii kumbe ni zaidi ya ninavoijua...the hard i try to understand my dear country the more complicated it becomes!!
 
Nafikiri ni kulindana tu kwa sababu kama ingekuwa tunaogopa rebels basi hatujafanikiwa wala haijatusaidia kwa miaka yote, nchi zote zinazofanya mapinduzi ziko juu yetu na hakuna upumbavu kama hapa kwetu!!
 
Back
Top Bottom