Huu wimbo wa "Magufuli" ulioimbwa na Harmonize, je ni wimbo wa kampeni, kusifia au hamasa?

Mgeni wa Jiji

JF-Expert Member
Jul 27, 2017
7,913
13,373
Wasalamu .

Sina maongezi mengi sana juu ya hili kwa sababu maongezi yangu kwa upana wake yataitaji ufafanuzi mrefu ambao sipo tayari kuuweka kama sehemu ua uzi huu labda kama 'comment' ndogo ndogo.

Huu wimbo unatokana na wimbo wa 'Kwangaru' ulioimbwa na wasanii Diamond na Harmonize, kiukweli bado nawaza hatima ya taifa letu hasa kimaendeleo kama tunahamasishana kwa nyimbo kama kwangaru remix.

Sanaa ya nyimbo imefanya vizuri sana kwenye kuhamasisha hapa nchini ila ilipofikia sasa haihamasishi ujenzi wa taifa imara tena, badala yake tunachukulia kujenga taifa imara kama kitu cha mchezo mchezo.

Huu wimbo Kwangaru remix hauwezi fananisha na wimbo kama 'Alisema Mwalimu' ule orijino sio huu wa kijana Ney wa Mitego.

Hakuna taifa linatumia nyimbo za kucheza cheza katika kuhamasisha shughuli ka kujenga/kukomboa taifa, hili jambo ni Tz tu limeanza kushika kasi.

Pia bado sijajua huu wimbo nausikia hadi kwenye vituo vya redio, nayliza huu ni wimbo wa kampeni, kusifia au kuhamasisha?, je hatujaanza kampeni kabla ya muda?.

Sijaweza pangilia hoja yangu hii japo ni nzuri sababu kiukweli ninashangazwa na kushindwa kujua tunaelekea wapi kama taifa, ni wapi tunawapeleka vijana wetu.

Mimi ningekuwa ni raisi Magufuli huu wimbo ningekataza kupigwa na ningewatuma basata waufungie kabisa pengine ingesaidia kufanya watumishi na watendaji kuchapa kazi na si kunisifia sifia na kujipendekeza kiuongo uongo tu.

NB: mnivumilie sijapangilia hoja yangu

Shukrani.
 
Kama ambavyo msanii anaweza kuandika wimbo wa kumsifia demu wake mwanzo mwisho, basi nae Harmonize ameamua kuandika wimbo wa kumsifia raisi wake. Me sidhani kama kuna ubaya labda mtoa mada useme tu ukweli una chuki na aliyetajwa kwenye wimbo
 
watu wakanda ya ziwa bwana hata wakijamba wanapenda sifiwa
Wasalamu .
Sina maongezi mengi sana juu ya hili kwa sababu maongezi yangu kwa upana wake yataitaji ufafanuzi mrefu ambao sipo tayari kuuweka kama sehemu ua uzi huu labda kama 'comment' ndogo ndogo.
Huu wimbo unatokana na wimbo wa 'Kwangaru' ulioimbwa na wasanii Diamond na Harmonize, kiukweli bado nawaza hatima ya taifa letu hasa kimaendeleo kama tunahamasishana kwa nyimbo kama kwangaru remix.
Sanaa ya nyimbo imefanya vizuri sana kwenye kuhamasisha hapa nchini ila ilipofikia sasa haihamasishi ujenzi wa taifa imara tena, badala yake tunachukulia kujenga taifa imara kama kitu cha mchezo mchezo.
Huu wimbo Kwangaru remix hauwezi fananisha na wimbo kama 'Alisema Mwalimu' ule orijino sio huu wa kijana Ney wa Mitego.
Hakuna taifa linatumia nyimbo za kucheza cheza katika kuhamasisha shughuli ka kujenga/kukomboa taifa, hili jambo ni Tz tu limeanza kushika kasi.
Pia bado sijajua huu wimbo nausikia hadi kwenye vituo vya redio, nayliza huu ni wimbo wa kampeni, kusifia au kuhamasisha?, je hatujaanza kampeni kabla ya muda?.
Sijaweza pangilia hoja yangu hii japo ni nzuri sababu kiukweli ninashangazwa na kushindwa kujua tunaelekea wapi kama taifa, ni wapi tunawapeleka vijana wetu.
Mimi ningekuwa ni raisi Magufuli huu wimbo ningekataza kupigwa na ningewatuma basata waufungie kabisa pengine ingesaidia kufanya watumishi na watendaji kuchapa kazi na si kunisifia sifia na kujipendekeza kiuongo uongo tu.
NB: mnivumilie sijapangilia hoja yangu
Shukrani.
 
Wameshapokea maelekezo toka juu wafanye nini sasa na elimu yao ya darasa la 7 kama sio kutii maagizo bila nissan au noah nyeusi?
 
Ni wimbo wa kusifia na kuunga mkono juhudi za mheshimiwa mwenyekiti. Binafsi niliuelewa kwa kiasi fulani ule wa kwanza, ila sasa baada ya huu wa pili nao kutoka; imenibidi tu nyimbo zote nizipotezee.
 
Kama ambavyo msanii anaweza kuandika wimbo wa kumsifia demu wake mwanzo mwisho, basi nae Harmonize ameamua kuandika wimbo wa kumsifia raisi wake. Me sidhani kama kuna ubaya labda mtoa mada useme tu ukweli una chuki na aliyetajwa kwenye wimbo

Mbona sina chuki na kiongozi wetu?
 
wabongo bhana

mbona mondi aliwahi kutoa no 1 remix mule ndani anaimba kabisa "ccm ushindi ni lazima"??

na ulikuwa wimbo wa kampeni!..
na alizunguka kufanya show za kampeni mpaka zenji uko..

hapo vipi?
 
Back
Top Bottom