Kenya 2022 Huu uwazi wa uchaguzi wa Kenya ni mageuzi makubwa sana! Kila mtu duniani anaweza kudownload matokeo na kujijumlishia

Kenya 2022 General Election

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Feb 17, 2015
13,661
18,035
Pale kituoni kura zikihesabiwa na kujazwa kwenye form (34A), kila wakala anaipiga pcha na kuwarushia watu wake, anapata hard copy kisha hiyo form inakuwa uploaded kwenye mfumo wa tume ya uchaguzi. Kila mtu anaweza kudownload na kujijumlishia ili kuona mwenendo wa mgombea yeyote, kisichotakiwa ni kutangaza tu kuwa nani ni mshindi maana hilo ni jukumu la Tume ya uchaguzi. Huku kwetu waliojaribu kuweka kituo cha kujijumlishia pale mliman city walikiona cha moto!!. Kwa wenzetu ruhusa kujumlisha lakini haramu kumtangaza yeyote kuwa ni mshindi!!

Kila chombo cha habari kimejijumlishia na kuweka wazi matokeo bila kutamka nani ni mshindi. Gazeti la The Daily Nation (online) la kenya limeweka tayari majumuisho zaidi nya asilimia 94% za kura zilizopigwa, na imeyaanika kama ifuatavvyo:

William Ruto​

UDA

49.92%
6,702,438 Votes

Raila Odinga​

AZIMIO

49.41%
6,634,135 Votes

George Wajackoyah​

RPK

0.44%
59,449 Votes

David Waihiga​

AGANO

0.23%
31,265 Votes

Kwa mujibu wa kura zilizojumulishwa la The Daily Nation: Jumla ya kura zilizojumilishwa ni 13,427,287.
Jumla ya kura zilizopigwa ni 14,164,561 sawa na asilimia 65.4% ya watu waliojiandikisha.

Kwa hiyo kwa mujibu yaliyooneshwa (siyo yaliyotangazwa), kura ambazo bado hazijajumlishwa ni 737,274 (zikiwemo zile zilizoharibika), Kwa hiyo kuna kila dalili kuwa uchaguzi utarudiwa kwa kuwa hakuna anayeelekea kupata asilimia 50 + 1. (Ruto ana 49.92% na Raila Odinga ana 49.41%).

Kama nia ipo, na sisi tunaweza kujifunza kitu kutoka kwa majirani zetu, ikizingatiwa kuwa Rais wetu mstaafu Kikwete yuko huko kama kiongozi wa timu ya waangalizi wa uchaguzi ya Afrika ya mashariki!!

Ukizingatia walivyokaribiana vikali kati ya Ruto na Odinga, bila UWAZI katika mwenendo wa kuhesabu na kujumlisha kura hakuna ambaye angeridhika kuwa katendewa haki kama akishindwa!
 

2022 General Election voter turnout is 65.4pc, Chebukati says.​

The voter turnout in the 2022 General Election stands at 65.4 percent, Independent Boundaries and Elections Commission (IEBC) chair, Wafula Chebukati has announced.
Mr Chebukati clarified the figure which represents 14,164,561 voters, will go up once they include those who voted through the manual register.
 
sasa uwazi uko wapi? huko vituoni zilipotoka hizi kura unajua yaliyotendeka.

Figisu zote zinafanyika huko mapolini na hapo kwenye Billboard ya IEBC ni kukamilisha fitna tu.

Huku NEC nao mbona wanaweza tu kufanya hivyo lakini umafia wote ukaishia kasuli huko.

Njia pekee ni kuwa na electonic system ambayo mpiga kura akipiga inahesabu hapo hapo na liscreen likuuubwa la Tume ya uchaguzi linahesabu na kutoa current results. Muda wa kupiga kura ukiisha na lenyewe linastop kucount na matokeo hapohapo kila mtu anayaona.

Hakuna haki kwenye kitu kinaitwa uchaguzi.
 
Sa
Subiri hadi mwisho
Sawa, lakini dalili njema huonekana asubuhi. Hatusemi kuwa hakutakuwa na matatizo kabisa ila tumeiona ile "political will"/utashi wa kisiasa wa kufanya uchaguzi ulio huru na wa haki!! Mfumo unaotumika unaruhusu uwazi!! Halafu matokeo yoyote yakiwemo ya urais inaruhusiwa kuyapinga mahakamani. Hapa kwetu matokeo ya Rais hayapingwi mahakamani!!.
 
The winner of presidential elections needs 50% + 1 of the valid votes cast and at least 25% votes in more than 24 counties.
 
Pale kituoni kura zikihesabiwa na kujazwa kwenye form (34A), kila wakala anaipiga pcha na kuwarushia watu wake, anapata hard copy kisha hiyo form inakuwa uploaded kwenye mfumo wa tume ya uchaguzi. Kila mtu anaweza kudownload na kujijumlishia ili kuona mwenendo wa mgombea yeyote, kisichotakiwa ni kutangaza tu kuwa nani ni mshindi maana hilo ni jukumu la Tume ya uchaguzi. Huku kwetu waliojaribu kuweka kituo cha kujijumlishia pale mliman city walikiona cha moto!!. Kwa wenzetu ruhusa kujumlisha lakini haramu kumtangaza yeyote kuwa ni mshindi!!

Kila chombo cha habari kimejijumlishia na kuweka wazi matokeo bila kutamka nani ni mshindi. Gazeti la The Daily Nation (online) la kenya limeweka tayari majumuisho zaidi nya asilimia 94% za kura zilizopigwa, na imeyaanika kama ifuatavvyo:

William Ruto​

UDA

49.92%
6,702,438 Votes

Raila Odinga​

AZIMIO

49.41%
6,634,135 Votes

George Wajackoyah​

RPK

0.44%
59,449 Votes

David Waihiga​

AGANO

0.23%
31,265 Votes

Kwa mujibu wa kura zilizojumulishwa la The Daily Nation: Jumla ya kura zilizojumilishwa ni 13,427,287.
Jumla ya kura zilizopigwa ni 14,164,561 sawa na asilimia 65.4% ya watu waliojiandikisha.

Kwa hiyo kwa mujibu yaliyooneshwa (siyo yaliyotangazwa), kura ambazo bado hazijajumlishwa ni 737,274 (zikiwemo zile zilizoharibika), Kwa hiyo kuna kila dalili kuwa uchaguzi utarudiwa kwa kuwa hakuna anayeelekea kupata asilimia 50 + 1. (Ruto ana 49.92% na Raila Odinga ana 49.41%).

Kama nia ipo, na sisi tunaweza kujifunza kitu kutoka kwa majirani zetu, ikizingatiwa kuwa Rais wetu mstaafu Kikwete yuko huko kama kiongozi wa timu ya waangalizi wa uchaguzi ya Afrika ya mashariki!!

Ukizingatia walivyokaribiana vikali kati ya Ruto na Odinga, bila UWAZI katika mwenendo wa kuhesabu na kujumlisha kura hakuna ambaye angeridhika kuwa katendewa haki kama akishindwa!

UCHAGUZI KENYA: Maafisa wa Tume wameitisha Kikao cha Dharura baada ya sintofahamu kutokea katika Ukumbi wa kuhakiki kura za Urais, baada ya Kompyuta kuingizwa ukumbini kinyume na Taratibu

Mchakato wa uhakiki umeahirishwa

Soma LIVE - Yanayojiri Uchaguzi Mkuu wa Kenya: Ruto na Odinga wanaendelea kuchuana vikali katika matokeo ya awali

#KenyaDecides2022
 
sasa uwazi uko wapi? huko vituoni zilipotoka hizi kura unajua yaliyotendeka.

Figisu zote zinafanyika huko mapolini na hapo kwenye Billboard ya IEBC ni kukamilisha fitna tu.

Huku NEC nao mbona wanaweza tu kufanya hivyo lakini umafia wote ukaishia kasuli huko.

Njia pekee ni kuwa na electonic system ambayo mpiga kura akipiga inahesabu hapo hapo na liscreen likuuubwa la Tume ya uchaguzi linahesabu na kutoa current results. Muda wa kupiga kura ukiisha na lenyewe linastop kucount na matokeo hapohapo kila mtu anayaona.

Hakuna haki kwenye kitu kinaitwa uchaguzi.
Hiyo ya electronic inaweza kuwa prone to hacking ndio maana manual inaenda sambamba na electronic Ili majibu ya makaratasi yaendane na yale ya electronic.
 
Huo uwazi, matokeo kila mtu anayaona, yakienda yofauti, maana sio ya Tume ni ya vyanzo vingine ,tujiandae kwa machafuko
 
Huo uwazi, matokeo kila mtu anayaona, yakienda yofauti, maana sio ya Tume ni ya vyanzo vingine ,tujiandae kwa machafuko
Wala hakuna machafuko, Kenya ya zamani muda huu tayari Kibra walishaandamana..... Ila mwaka huu karibu Kila aliyeanguka anakubali matokeo hasa ubunge na u governor so naamini hata Urais kama uwazi utaendelea hakuna machafuko ila kuna uwezekani uchaguzi ukamalizwa mahakamani.
 
Back
Top Bottom