Huu utulivu, furaha na shangwe Mhe. Rais ataukamilisha kwa katiba mpya?

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Kuna kautulivu flani unakaona kwenye nchi, kuna kauhuru flani unakaona kuanzia vijiweni,makazini,barabarani na kwenye mitandao ya kijamii watu wakijadiliana mambo kwa Uhuru bila kukamatwa na hakuna athari ya Usalama iliyoripotiwa.

Kuna upendo flani umeanza kuonekana baina ya viongozi wa kisiasa, Leo wanasiasa wanaweza kukaa wakabishana kwa mbaali bila kutuhumiana au vyama vyao kuwaona wasaliti.

Upo upendo wa kiimani umerudi ambapo hata akina Bagonza, Ni'mugizi na wengine wanaheshimika nakuonekana mashujaa wa kupigania haki tofauti na awali walipoonekana kama wasaliti na wasio Wazalendo.

Kuna Uhuru flani umeanza kuchomoza ambapo kesi zinafutwa na viongozi wetu wa dini wa Uamsho wanaanza kuona progress ya kesi zinazowakabili.

Kinachotokea ndani ya miezi miwili kimetoa nuru kwa wafanyabiashara na wananchi kuendelea kufanya kazi na kutoa mchango wao kwa Taifa.

Swali: Tunaanza kujadili kurejea kwa Uhuru,amani na utulivu kutokana na ukweli kwamba viongozi waliokuwepo walilivuruga Taifa, walishindwa kutambua kwamba maendeleo yanatokana na furaha ya watu. Lakini pia hawakufanya makusudi bali walifanya kwa sababu katiba na sheria zilizokuwepo na zilizopo zinatoa mwanya huo. Mhe. Rais ni lini utaamua kufungua mjadala wa Katiba mpya nakuusimamia ili tuwe na amani yakudumu? Ni lini utatuondoa kwenye dhana ya CCM ni ileile? Ni lini utakubali kwamba hakuna CcM bila Tanzania?
 
Japo kuna umuhimu mkubwa wa kupata Katiba mpya au hata kuendelea na mchakato wa kuipata ulipoishia lakini kwa maoni yangu ni mapema sana kumtwisha Rais SSH mzigo huo akiwa hata hajatimiza miezi mitatu akiwa kama Mkuu wa Nchi

Kuna kazi kubwa sana ya kurekebisha mifumo ya nchi katika kila nyanja na sekta kama vile mifumo ya kiutawala na uhusiano baina ya vyombo husika vya mihimili ya taifa, mifumo ya kiusalama, kibiashara kama fedha na kodi, mahusiano ya kimataifa n.k. Mifumo ambayo ilichezewa na kuharibiwa na mtangulizi wake.

Huu utulivu, uhuru na furaha kidogo tunavyo viona ni matokea ya nia ya SSH kuweka kila kitu na kila utaratibu mahali pake japo kuna mengine yatahitaji muda zaidi

Kusema aanze kushughulikia mchakato wa katiba mpya sasa kutachukua attention yake yote maana si jambo dogo

Kumbuka hadi sasa hakuna muafaka wa kitaifa kwamba ni katiba ipi iletwe kwa Watanzania. Je ni ile ya Warioba au iliyofanyiwa uhariri kwa baraka za Chama Tawala? Yeye mwenyewe alikua Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Katiba na anajua akisema alianzishe kwa sasa suala hilo kutakua na mivutano na miparuano kuanzia ndani ya chama chake mwenyewe hadi kwa wananchi kwa ujumla.

Tumpe muda angalau katika miaka miwili au mitatu ijayo kama sio muhula wake wa pili kama akifanikiwa kuendelea
 
Kuna kautulivu flani unakaona kwenye nchi, kuna kauhuru flani unakaona kuanzia vijiweni,makazini,barabarani na kwenye mitandao ya kijamii watu wakijadiliana mambo kwa Uhuru bila kukamatwa na hakuna athari ya Usalama iliyoripotiwa.

Kuna upendo flani umeanza kuonekana baina ya viongozi wa kisiasa, Leo wanasiasa wanaweza kukaa wakabishana kwa mbaali bila kutuhumiana au vyama vyao kuwaona wasaliti.

Upo upendo wa kiimani umerudi ambapo hata akina Bagonza, Ni'mugizi na wengine wanaheshimika nakuonekana mashujaa wa kupigania haki tofauti na awali walipoonekana kama wasaliti na wasio Wazalendo.

Kuna Uhuru flani umeanza kuchomoza ambapo kesi zinafutwa na viongozi wetu wa dini wa Uamsho wanaanza kuona progress ya kesi zinazowakabili.

Kinachotokea ndani ya miezi miwili kimetoa nuru kwa wafanyabiashara na wananchi kuendelea kufanya kazi na kutoa mchango wao kwa Taifa.

Swali: Tunaanza kujadili kurejea kwa Uhuru,amani na utulivu kutokana na ukweli kwamba viongozi waliokuwepo walilivuruga Taifa, walishindwa kutambua kwamba maendeleo yanatokana na furaha ya watu. Lakini pia hawakufanya makusudi bali walifanya kwa sababu katiba na sheria zilizokuwepo na zilizopo zinatoa mwanya huo. Mhe. Rais ni lini utaamua kufungua mjadala wa Katiba mpya nakuusimamia ili tuwe na amani yakudumu? Ni lini utatuondoa kwenye dhana ya CCM ni ileile? Ni lini utakubali kwamba hakuna CcM bila Tanzania?
tunatamani iwe hivyo
 
Japo kuna umuhimu mkubwa wa kupata Katiba mpya au hata kuendelea na mchakato wa kuipata ulipoishia lakini kwa maoni yangu ni mapema sana kumtwisha Rais SSH mzigo huo akiwa hata hajatimiza miezi mitatu akiwa kama Mkuu wa Nchi

Kuna kazi kubwa sana ya kurekebisha mifumo ya nchi katika kila nyanja na sekta kama vile mifumo ya kiutawala na uhusiano baina ya vyombo husika vya mihimili ya taifa, mifumo ya kiusalama, kibiashara kama fedha na kodi, mahusiano ya kimataifa n.k. Mifumo ambayo ilichezewa na kuharibiwa na mtangulizi wake.

Huu utulivu, uhuru na furaha kidogo tunavyo viona ni matokea ya nia ya SSH kuweka kila kitu na kila utaratibu mahali pake japo kuna mengine yatahitaji muda zaidi

Kusema aanze kushughulikia mchakato wa katiba mpya sasa kutachukua attention yake yote maana si jambo dogo

Kumbuka hadi sasa hakuna muafaka wa kitaifa kwamba ni katiba ipi iletwe kwa Watanzania. Je ni ile ya Warioba au iliyofanyiwa uhariri kwa baraka za Chama Tawala? Yeye mwenyewe alikua Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Katiba na anajua akisema alianzishe kwa sasa suala hilo kutakua na mivutano na miparuano kuanzia ndani ya chama chake mwenyewe hadi kwa wananchi kwa ujumla.

Tumpe muda angalau katika miaka miwili au mitatu ijayo kama sio muhula wake wa pili kama akifanikiwa kuendelea
uko sahihi mama anahitaji muda ili abadilishe mindset za wale wahuni waliomo ndani. vinginrvyo mchakato wa katiba mpya unaweza kuvulugwa tena. Ikumbukwe wahunu wengi wanadhani katiba mpya itawanyima ukaji wakati sio kweli. ni Imani potofu
 
Kuna kautulivu flani unakaona kwenye nchi, kuna kauhuru flani unakaona kuanzia vijiweni,makazini,barabarani na kwenye mitandao ya kijamii watu wakijadiliana mambo kwa Uhuru bila kukamatwa na hakuna athari ya Usalama iliyoripotiwa.

Kuna upendo flani umeanza kuonekana baina ya viongozi wa kisiasa, Leo wanasiasa wanaweza kukaa wakabishana kwa mbaali bila kutuhumiana au vyama vyao kuwaona wasaliti.

Upo upendo wa kiimani umerudi ambapo hata akina Bagonza, Ni'mugizi na wengine wanaheshimika nakuonekana mashujaa wa kupigania haki tofauti na awali walipoonekana kama wasaliti na wasio Wazalendo.

Kuna Uhuru flani umeanza kuchomoza ambapo kesi zinafutwa na viongozi wetu wa dini wa Uamsho wanaanza kuona progress ya kesi zinazowakabili.

Kinachotokea ndani ya miezi miwili kimetoa nuru kwa wafanyabiashara na wananchi kuendelea kufanya kazi na kutoa mchango wao kwa Taifa.

Swali: Tunaanza kujadili kurejea kwa Uhuru,amani na utulivu kutokana na ukweli kwamba viongozi waliokuwepo walilivuruga Taifa, walishindwa kutambua kwamba maendeleo yanatokana na furaha ya watu. Lakini pia hawakufanya makusudi bali walifanya kwa sababu katiba na sheria zilizokuwepo na zilizopo zinatoa mwanya huo. Mhe. Rais ni lini utaamua kufungua mjadala wa Katiba mpya nakuusimamia ili tuwe na amani yakudumu? Ni lini utatuondoa kwenye dhana ya CCM ni ileile? Ni lini utakubali kwamba hakuna CcM bila Tanzania?
Kariba mpya chini ya wahafidhina wa CCM ni ndoto... jiulizeni JK alipoanzisha huo mchakato ulivurugwa na kina nani? Je hao waliouvuruga hawakupewa vyeo vya hisani? Je hawapo tena au mapandikizi yao?
 
Siyo majambazi, mafisadi na wachezea mifumo ya serikali tu wanaomjaribu rais Samia hata Chadema wanamjaribu.

Leo wametangaza maandamano ya kudai katiba mpya na tume huru yani wanataka rais aache kufocus na kukamilisha SGR ,Bwawa la nyerere ,ajira, viwanda ambavyo ndiyo hitaji la wananchi akaanze kutenga mabilioni ya fedha kwa ajili ya katiba ambayo ni hitaji la wanasiasa tu?

Mbaya zaidi wanataka mchakato wa katiba uanze upyaaaaa na siyo pale ulipoishia zamani
 
Siyo majambazi, mafisadi na wachezea mifumo ya serikali tu wanaomjaribu rais Samia hata Chadema wanamjaribu.

Leo wametangaza maandamano ya kudai katiba mpya na tume huru yani wanataka rais aache kufocus na kukamilisha SGR ,Bwawa la nyerere ,ajira, viwanda ambavyo ndiyo hitaji la wananchi akaanze kutenga mabilioni ya fedha kwa ajili ya katiba ambayo ni hitaji la wanasiasa tu?

Mbaya zaidi wanataka mchakato wa katiba uanze upyaaaaa na siyo pale ulipoishia zamani
Siyo majambazi, mafisadi na wachezea mifumo ya serikali tu wanaomjaribu rais Samia hata Chadema wanamjaribu.

Leo wametangaza maandamano ya kudai katiba mpya na tume huru yani wanataka rais aache kufocus na kukamilisha SGR ,Bwawa la nyerere ,ajira, viwanda ambavyo ndiyo hitaji la wananchi akaanze kutenga mabilioni ya fedha kwa ajili ya katiba ambayo ni hitaji la wanasiasa tu?

Mbaya zaidi wanataka mchakato wa katiba uanze upyaaaaa na siyo pale ulipoishia zamani
Walivyo ona wamefanikiwa kufanya vikao vya ndani bila kuzuiwa,kweli kinacho fuata ni maandamano yayisiyo na kikomo.
ukicheka na nyani utavuna mabua.
 
Nimepokea barua ya kupanda cheo kazini,kwa nini nisimpende mama?
😁😁😁
Tulizoea haya mambo kwa wana CCM tu,na S'Gang.
Sisi tusio wanasiasa tulisota.
 
Back
Top Bottom