Huu Utitiri Wa Gesti Mjini Songea Unaashiria Nini?!!

chakii

JF-Expert Member
Sep 15, 2013
19,680
22,685
Habari Wana-Jf!!

Kwa uwepo wangu hapa mjini Songea nimebaini mambo mengi likiwemo hili la utitiri wa Gesti katika mji huu wa Songea,.

Wakuu hii hali siyo ya kawaida kama wengine wanavyoweza kuwaza kwani huu mji hauna wageni kiasi cha kupelekea Gesti kuwepo kila kona,.

Mji huu una wakazi wachache ukilinganisha na Mikoa mingine iliyopo hapa Tanzania,.

Sasa tujiulize Gesti za nini kiasi hiki au wenyeji wenyewe wanazitumia kwa starehe zao ilhali wamejenga au wanazo nyumba zao,..

Kuna habari za chinichini ambazo bado sijazipatia majibu ya Uhakika Kwamba wakazi wengi wa mkoa huu wa Ruvuma ukiwemo mji huu wa Songea wanapenda sana starehe kuliko kazi hivyo wanatumia sana Gesti hizi!!

Wakuu sijahukumu bali nimeleta hili jambo kwenu ili tupatiane majibu ya Uhakiki Juu ya hii Hali,.

Nawasilisha,..
 
Inawezekana zinaandaliwa kwa ajili ya wageni wawekezaji wanaotaka kuja kuwekeza ukoo huko...
 
...kwamba songea ni mbali,huwezi kwenda na kurudi. Pia usafiri na barabara za kwenda mikoa/wilayani ni mbaya...
 
sidhani mkuu kwani wageni wengi wanaochukua vyumba kwenye hizi gesti hawalali,.

Wanavitumia kwa masaa machache tu kisha wanaondoka!!

Hahahahaaaa..... endelea na uchunguzi utujuze uhalisia wa hali ilivyo hapo.
 
...kwamba songea ni mbali,huwezi kwenda na kurudi. Pia usafiri na barabara za kwenda mikoa/wilayani ni mbaya...

mkuu una wazo, labda kuna sababu nyingine zaidi ya hii!!
 
Back
Top Bottom