Huu utaratibu mpya wa TANESCO wakulipa deni ni kiashiria tosha kuwa hawataki sisi wenye hali ya chini tutumie umeme

BOMBAY

JF-Expert Member
Apr 16, 2014
4,676
3,378
Habar wakuu,

Kwa masikitiko makubwa napenda niwaombe TANESCO waje watoe kila kilicho chao majumbani mwetu ili tujue moja.

Wameanzisha utaratibu wa ajabu kwa wateja wanaodaiwa madeni. Mwanzo walikuwa wanatukata madeni kupitia mfumo wa Luku, yaani tunanunua umeme tunapewa nusu ya pesa tulionunua umeme. Tukinunua umeme wa 10000 tunakatwa 5000 tunapewa umeme wa 5000

Chaajabu hivi sasa hawataki tena tulipe kwa mfumo huo! Yaani wanataka ulipe kiasi kikubwa cha pesa, mfano nyumbani wametuambia tunatakiwa kulipa Tsh. 85000 kila mwezi halafu ndo turuhusiwe kununua umeme! Tusipotoa hiyo hela hatupati umeme!


Hili haliwezekani hata kidogo, umeme tunaotumia kwa mwezi ni wa 10000. Je tutawezaje kumudu hiyo 85000 kila mwezi?


TANESCO Tuoneeni huruma jamanii vyuma vimekaza. Leo ni siku ya NNE tupo kizani.
 
Naona tangazo lao hapa, wanasema wametusogezea huduma karibu.
 
Habar wakuu,

Kwa masikitiko makubwa napenda niwaombe tanesco waje watoe kila kilicho chao majumbani mwetu ili tujue moja.

Wameanzisha utaratibu wa ajabu kwa wateja wanaodaiwa madeni,Mwanzo.walikuwa wanatukata madeni kupitia mfumo wa Luku,yaan tunanunua umeme tunapewa nusu ya pesa tulionunua umeme.
Tukinunua umeme wa 10000 tunakatwa 5000 tunapewa umeme wa 5000

Chaajabu hiv sasa hawataki tena tulipe kwa mfumo huo!!!!yan wanataka ulipe kias kikubwa cha pesa,mfano home wametuambia tunatakiwa kulipa 85000 kila mwezi halafu ndo turuhusiwe kununua umeme!!!Tusipotoa hiyo hela hatupati umeme!

Hili haliwezekan hata kidogo,umeme tunaotumia kwa mwezi ni wa 10000,je tutawezaje kumudu hiyo 85000 kila mwezi???


Tanesco Tuoneeni huruma jamanii vyuma vimekaza.Leo ni siku ya NNE tupo kizani.
Na wewe kwa nini ulitumia halafu hukulipa
 
Mwenye namba ya waziri wa nishati anipe tafadhali maana.hii haikubaliki
 
Habar wakuu,

Kwa masikitiko makubwa napenda niwaombe tanesco waje watoe kila kilicho chao majumbani mwetu ili tujue moja.

Wameanzisha utaratibu wa ajabu kwa wateja wanaodaiwa madeni,Mwanzo.walikuwa wanatukata madeni kupitia mfumo wa Luku,yaan tunanunua umeme tunapewa nusu ya pesa tulionunua umeme.
Tukinunua umeme wa 10000 tunakatwa 5000 tunapewa umeme wa 5000

Chaajabu hiv sasa hawataki tena tulipe kwa mfumo huo!!!!yan wanataka ulipe kias kikubwa cha pesa,mfano home wametuambia tunatakiwa kulipa 85000 kila mwezi halafu ndo turuhusiwe kununua umeme!!!Tusipotoa hiyo hela hatupati umeme!

Hili haliwezekan hata kidogo,umeme tunaotumia kwa mwezi ni wa 10000,je tutawezaje kumudu hiyo 85000 kila mwezi???


Tanesco Tuoneeni huruma jamanii vyuma vimekaza.Leo ni siku ya NNE tupo kizani.
Na ninyi kwa nini mlilimbikiza deni,Watanzania bwana shida tupu.Ni Tanzania tu ambapo mtu unaweza kupata utility on credit.Hivi na ninyi kwa nini msiwaonee huruma TANESCO.Lipeni hela hizo bwana miundo mbinu itengenezwe tupate umeme wa uhakika.Mtu unadaiwa, halafu unamuona anayedai mbaya.Noma sana.Yumkini wameona mfumo waliokuwa wanatumia zamani unawachelewesha.
Hakuna njia,dawa ya deni ni kulipa.Kwanza wamewahurumia,wangewapeleka mahakani mkalipie huko.
 
Na ninyi kwa nini mlilimbikiza deni,Watanzania bwana shida tupu.Ni Tanzania tu ambapo mtu unaweza kupata utility on credit.Hivi na ninyi kwa nini msiwaonee huruma TANESCO.Lipeni hela hizo bwana miundo mbinu itengenezwe tupate umeme wa uhakika.Mtu unadaiwa, halafu unamuona anayekudai mbaya.Noma sana.Wameona mfumo waliokuwa wanatumia zamani unawachelewesha.Hakuna njia,sawa ya deni ni kulipa.Kwanza wamewahurumia,wangewapeleka mahakani mkalipie huko.
Hujui kuwa Hawa tanesco ni majuha?pesa zetu zinaishia kuwalipa IPTL kila siku mil 400 bila sababu za msingi!!Qameshindwa kuboresha huduma kwa miongo kadhaa wajinga tu
Hivi videni vidogo wanavyotudai havitowasaidia chochote
 
Na ninyi kwa nini mlilimbikiza deni,Watanzania bwana shida tupu.Ni Tanzania tu ambapo mtu unaweza kupata utility on credit.Hivi na ninyi kwa nini msiwaonee huruma TANESCO.Lipeni hela hizo bwana miundo mbinu itengenezwe tupate umeme wa uhakika.Mtu unadaiwa, halafu unamuona anayekudai mbaya.Noma sana.Yumkini wameona mfumo waliokuwa wanatumia zamani unawachelewesha.Hakuna njia,dawa ya deni ni kulipa.Kwanza wamewahurumia,wangewapeleka mahakani mkalipie huko.
Wameshindwa kuwapeleka Dowans,Richmond na Iptl wezi wa fedha zetu.Acha kuwatetea Hawa wezi.
 
Na ninyi kwa nini mlilimbikiza deni,Watanzania bwana shida tupu.Ni Tanzania tu ambapo mtu unaweza kupata utility on credit.Hivi na ninyi kwa nini msiwaonee huruma TANESCO.Lipeni hela hizo bwana miundo mbinu itengenezwe tupate umeme wa uhakika.Mtu unadaiwa, halafu unamuona anayekudai mbaya.Noma sana.Yumkini wameona mfumo waliokuwa wanatumia zamani unawachelewesha.Hakuna njia,dawa ya deni ni kulipa.Kwanza wamewahurumia,wangewapeleka mahakani mkalipie huko.

ungekuwa unajua jinsi hayo madeni yalivyotokea kwa wateja wengi usingemlaumu mleta mada,zamani wakati mfumo wa mita za LUKU,haujawa kwa kila mteja kulikuwa na zile mita ambazo tanesco wanatakiwa waje kusoma kila mwezi ,wengi wao walikuwa hawaji kusoma mita bali wana kadilia tu matumizi yako ya kila mwezi na kukuletea bill,balaa lililowakumba wateja wengi walikuwa wanakadiliwa makadilio ya chini kuliko matumizi halisi,sasa hizo units zinazoachwa kila mwezi baada ya mwaka unazani itakuwaje??balaa lilianza pale walipoanza kuzibadilisha hizo conversion meter na kuweka luku,kwani lazima wasome actual readings,ndio unakuta mtu anadaiwa milioni kadhaa!!!na baadaye tanesco waliliona hilo kuwa kwa kiasi. Fulani walichangia ndio maana wakaweka utaratibu huo wa malipo kidogo kidogo!!kama wameutoa watu Mwafaaaa
 
Hujui kuwa Hawa tanesco ni majuha?pesa zetu zinaishia kuwalipa IPTL kila siku mil 400 bila sababu za msingi!!Qameshindwa kuboresha huduma kwa miongo kadhaa wajinga tu
Hivi videni vidogo wanavyotudai havitowasaidia chochote
Mkuu wanadai watu wengi,sio wewe tu.Wakikusanya madeni yote Tanzania nzima, ni hela nyingi.Nenda kalipe tu mkuu, ili wakuuzie umeme.The choice is yours.
 
ungekuwa unajua jinsi hayo madeni yalivyotokea kwa wateja wengi usingemlaumu mleta mada,zamani wakati mfumo wa mita za LUKU,haujawa kwa kila mteja kulikuwa na zile mita ambazo tanesco wanatakiwa waje kusoma kila mwezi ,wengi wao walikuwa hawaji kusoma mita bali wana kadilia tu matumizi yako ya kila mwezi na kukuletea bill,balaa lililowakumba wateja wengi walikuwa wanakadiliwa makadilio ya chini kuliko matumizi halisi,sasa hizo units zinazoachwa kila mwezi baada ya mwaka unazani itakuwaje??balaa lilianza pale walipoanza kuzibadilisha hizo conversion meter na kuweka luku,kwani lazima wasome actual readings,ndio unakuta mtu anadaiwa milioni kadhaa!!!na baadaye tanesco waliliona hilo kuwa kwa kiasi. Fulani walichangia ndio maana wakaweka utaratibu huo wa malipo kidogo kidogo!!kama wameutoa watu Mwafaaaa
Bado mpaka hapo kosa ni la mteja.Kama unaona bili imekuja kidogo au kubwa,nenda karipoti ili marekebisho yafanywe mapema,don't wait.Tatizo ni kwamba tukiona imekuja bili ndogo tunaminya tukidhani tumeula, kumbe tunalimbikiza matatizo. Najua hata wakati mwingine wateja wana-collude na wasoma metre ili waletewe bili ndogo!
Mkuu hakuna choice,inabidi tufanye TANESCO wanavyotaka au tukae gizani.Ila Watanzania ni lazima tujifunze logic,we are simply too illogical.
 
Wameshindwa kuwapeleka Dowans,Richmond na Iptl wezi wa fedha zetu.Acha kuwatetea Hawa wezi.
Kuwatetea katika hili,haina maana kwamba TANESCO hawana matatizo,lahasha,wanayo lukuki,ila kwa hili they are justified.I am just being rational mkuu.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom