Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Last week end nilikuwa maeneo ya mwenge pale nikiwa na mwandani wangu. Kimsingi aliniomba nimsindikize akatengeneze kucha zake. Tukatia timu, mwenyewe anadai kuna kijana ambaye humtengeneza hizo kucha mara kwa mara. Tukafika mwenge na yule jamaa tukamkuta, kwa kuwa alikuwa na mteja mwingine tukalazimika kusubiri. Then ikafata zamu ya honey wangu. Mamaaa akavua viatu akaweka miguu kwenye mapaja ya kale kajamaa, kakaanza kumnyoosha vidole vya miguu kama masaji fulani hivi. Nikimuangalia demu wangu sikuamini, amejiachiaaaa katuliaa jamaa anabonyeza vidole then ndio akaanza kumsafisha hizo kucha na baadae kumpaka rangi kwa mtindo aliotaka....Alipomaliza tukiwa kwenye gari tunarudi nyumbani nikamwambia next time akitaka kusafisha kucha na kupaka rangi hilo zoezi nitalifanya mimi tukiwa chumbani kwetu kwani sikupenda jinsi jamaa alivyokuwa anamchezea miguu ni wazi alikuwa anamtekenya kimtindo.....Huwezi kuamini alinigomea kwa nguvu zote...Hivi wana nini wale jamaa pale mwenge???