Huu upuuzi wa wazanzibari usisikilizwe kabisa

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,779
AFP waunga mkono Karume aongezewe muda

Nora Damian

CHAMA cha Alliance for Tanzania Farmers (AFP), kimetaka Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, aongezewe muda, ili awe katika nafasi mzuri ya kuunda serikali ya mseto.


Kauli hiyo imekuja huku kukiwa na hoja zinazokinzana, kuhusu kiongozi huyo ama kuongezewa au kutoongezewa muda wa kuongoza serikali ya Zanzibar.


Mapema wiki hii, Msaidizi wa Katibu Mkuu wa CUF, Ismail Jussa, alikaririwa na gazeti dada la The Citizen, akitaka Rais Karume, aongezewe muda wa kuwa madarakani, lakini baadaye Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahimu Lipumba, alisema huo si msimamo wa chama chake.


Pia Chama Cha Mapinduzi

(CCM), kilichomweka madarakani Rais huyo kimesema hakina mpango wa kumuongezea kwa sababu utaratibu hauruhusu.


Hoja ya kutaka Rais Karume aongezewe muda wa kuwa madarakani, imeibuka katika majuma ya hivi karibuni baada ya kiongozi huyo na Katibu Mkuu wa CUF, Seif Sharrif Hamad, kukutana na kukubaliana kuzika tofauti za kisiasa, jambo ambalo limewaletea sifa viongozi hao.


Akizungumzia hoja hiyo jana jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa AFP, Said Soud Said, alisema si dhambi Rais Karume,kuongezewa muda wa kuwa madarakani na kwamba dhambi ni kutoa wakimbizi wanaotokana na machafuko yanayoweza kutokea baada ya uchaguzi


Alisema Wanzanzibari, wanahitaji mno kuwepo kwa serikali ya mseto, ili hatimaye waweze kuishi kwa amani na utulivu huku wakiwa wamoja.


Sais alisema Zanzibar inaongozwa na katiba ya nchi na kwamba kwa kupitia katiba hiyo, Rais Karume ana uwezo wa kuunda serikali ya mseto akivishirikisha vyama vyote vya siasa, hatua ambayo alisema italeta utulivu katika visiwa hivyo.


"Kuundwa kwa serikali ya mseto visiwani Zanzibar, kutasaidia kuindoa nchi hiyo katika mitafaruku ya mara kwa mara ya kisasa inayotokana na msimamo wa viongozi walioko madarakani, kukataa serikali ya mseto," alisema Said.


Hivi karibuni, CCM kupitia Makamu Mwenyekiti wake (Bara), Pius Msekwa, ilisema haiwezi kumuongezea muda Rais Karume, muda wa kuwa madarakani kwa sababu ni kinyume cha katiba.


Msekwa alisema katiba ya chama hicho, inataka marais wa pande zote mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kushika nyadhifa hizo kwa mihula miwili ya miaka mitano, kwa kila muhula.


Katika hatua nyingine, chama cha AFP kimeiomba serikali kutoa msamaha wa kodi kwa vyama vya siasa ili waweze kuingiza nchini vifaa vya kampeni ambavyo alidai kuwa ni rahisi kuvinunua nje kuliko hapa nchini.


Chama hicho ambacho kimeanzisha operesheni ijulikanayo kama 'pomboo' kuhamasisha wananchi kujiunga nacho pia kimemtaka rais Jakaya Kikwete akutane na viongozi wakuu wa vyama vya upinzani kabla ya muda wake wa uongozi kumalizika ili waweze kumweleza mambo mbalimbali
 
Hivi vyama vinavyoanza kumchanganya rais karume vikome kabisa
wiki iliopita vilianza vyama vya wamama
mara vyama vya watoa mikopo
mara vyama vya wauza vifaa vya kilimo
hawa tena

ccm kwa hili tutakufa na nyie daima;msiruhu ujinga kama huu
 
Kwani yeye tu ndio anaejua kuunda serikali ya Mseto?
Hii kwa nini watu wengine wanapenda kujifanya wao ni Oxygen?
 
karume ataongezewa miaka miwili hawe pamoja na seif(mseto), uchaguzi zenjibar hakuna mwaka huu, habari ndiyo hiyo.
 
karume ataongezewa miaka miwili hawe pamoja na seif(mseto), uchaguzi zenjibar hakuna mwaka huu, habari ndiyo hiyo.

Kwa Katiba ipi Rais huyo ataendelea kuwa madarakani hata baada ya muda kwisha? Kwani huo ni mchezo wa soka mpaka kuwe na muda wa majeruhi ambaye anayeuongeza ni refa tu? Oh, use your brain, at least once please!
 
Kwa Katiba ipi Rais huyo ataendelea kuwa madarakani hata baada ya muda kwisha? Kwani huo ni mchezo wa soka mpaka kuwe na muda wa majeruhi ambaye anayeuongeza ni refa tu? Oh, use your brain, at least once please!

Kaka naona huyu jamaa leo unae tuu,akila kona una yeye with the same statement,"Use your brain atleast once please"
 
Kaka naona huyu jamaa leo unae tuu,akila kona una yeye with the same statement,"Use your brain atleast once please"

Ninapojibu mara nyingine huwa siangalii nimemjibu nani, ninachoangalia ni hoja yenyewe tu ndugu, sorry kama inaonekana namtarget mtu yule yule! Ni katika kuweka msisitizo wa jambo! Thanks for your observation!
 
...CCM 'inaogopa' nini kumpa KARUME muda wa nyongeza kuunda hiyo serikali ya mpito iwapo wapinzani wameridhia? Katiba sio msahafu au biblia kusema 'hauguswi'!

Hata kama CCM itang'ang'ania kuweka mgombea wake, nchi ya Zanzibar itakuja ongozwa na serikali ya Upinzani, kama sio 2010 basi 2015.

 
Kwa Katiba ipi Rais huyo ataendelea kuwa madarakani hata baada ya muda kwisha?
Kwa vile katiba siyo Msahafu, inabadilishika na itabadilishwa!.

CCM bara lazima wajifunze kusoma alama za nyakati, Karume keshafungua macho, hawaweza kumfanya zezeta kama walivyomfanza Jumbe. Yeye na Seif wameshakubaliana, uchaguzi mwaka huu, Zanzibar mikononi mwa Seif, hiyo CCM bara itatafuta pa kushikia na pa kushikia.
 
Hivi vyama vinavyoanza kumchanganya rais karume vikome kabisa
wiki iliopita vilianza vyama vya wamama
mara vyama vya watoa mikopo
mara vyama vya wauza vifaa vya kilimo
hawa tena

ccm kwa hili tutakufa na nyie daima;msiruhu ujinga kama huu

waachani wenye zanzibari yao waamue mambo yao wenyewe kwani nyie inawahusu nini?hata wakitaka karume awe rais wa milele si sawa tu
 
Kwa vile katiba siyo Msahafu, inabadilishika na itabadilishwa!.

CCM bara lazima wajifunze kusoma alama za nyakati, Karume keshafungua macho, hawaweza kumfanya zezeta kama walivyomfanza Jumbe. Yeye na Seif wameshakubaliana, uchaguzi mwaka huu, Zanzibar mikononi mwa Seif, hiyo CCM bara itatafuta pa kushikia na pa kushikia.
Mimi naamini hatima iko mikononi mwa Karume kwana Seif ameshatamka lakini Karume kwa sababu anazojua ameshatamka hadharani kuwa hataki sasa kama anayetakiwa ameshasema hapana nani tena atendeleza huo uchuro? Labda Seif ataomba apewe amalizie miaka miwili akidai ni kumalizia kipindi cha Karume.
waachani wenye zanzibari yao waamue mambo yao wenyewe kwani nyie inawahusu nini?hata wakitaka karume awe rais wa milele si sawa tu
Sisi kina tuhusu kwa sababu watakuja kutusumbua hawa. Huu ushirikiano wao ni wa wachawi hauwezi kudumu.
 
Back
Top Bottom