GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,548
- 108,858
Ni tukio ambalo nimekuwa nikikutana nalo sana mara kwa mara tena sehemu nyingi ambapo utamwona Mwanaume ameongozana na ama Mpenzi au Mke wake mwenye mkoba wake ( Handbag ) kisha ukiwaona wako sehemu zisizo na Watu wengi utaona Mwanaume amebeba ule mkoba bila wasiwasi, hofu wala aibu tena kuna wengine hadi huwa wanayavaa mabegani na wengine wanayabeba Vichwani mwao wakiwa na nyuso za furaha lakini wakifika tu maeneo ya Watu wengi wenye mikoba yao hurudishiwa haraka haraka na Yule Mwanaume ' Kujikausha ' kama vile hajabeba ule mkoba.
Enyi Wanaume huu ' Unafiki ' kwa hao Wapenzi wenu / Wake zenu huwa mnaufanya kwa faida ya nani hasa? Kwani kama kweli umempenda Demu / Mke wako na labda unaongozana nae kutoka Tegeta hadi Mbagala kwanini tu usiwe unambebea huo mkoba wake muda wote ili kuonyesha upendo wako Kwake kuliko ' Kujitutumua ' kuwabebea sehemu za ' mafichoni ' na ' vichochoroni ' tu kuogopa aibu au kuchoreshwa?
Halafu na Wanawake nao walivyo ' Oya Oya ' wakiowaona Wapenzi wao / Waume zao wanapenda kuwabebea hiyo mikoba hudhani ndiyo wamependwa kweli kweli wakati ukweli ni kwamba hapo huwa ' wanasanifiwa ' kunakotukuka.
Nawasilisha.
Enyi Wanaume huu ' Unafiki ' kwa hao Wapenzi wenu / Wake zenu huwa mnaufanya kwa faida ya nani hasa? Kwani kama kweli umempenda Demu / Mke wako na labda unaongozana nae kutoka Tegeta hadi Mbagala kwanini tu usiwe unambebea huo mkoba wake muda wote ili kuonyesha upendo wako Kwake kuliko ' Kujitutumua ' kuwabebea sehemu za ' mafichoni ' na ' vichochoroni ' tu kuogopa aibu au kuchoreshwa?
Halafu na Wanawake nao walivyo ' Oya Oya ' wakiowaona Wapenzi wao / Waume zao wanapenda kuwabebea hiyo mikoba hudhani ndiyo wamependwa kweli kweli wakati ukweli ni kwamba hapo huwa ' wanasanifiwa ' kunakotukuka.
Nawasilisha.