Joan S
JF-Expert Member
- Oct 26, 2021
- 2,382
- 9,503
Huu ukatili Kwa watoto ni maumivu makali Sana, nashindwa kuelewa Dunia inaelekea wapi. Nimetulia zangu napewa taarifa ya kusikitisha mno,,,, Baba unapata wapi ujasiri wa kumlawiti mtoto wako wa kumzaa wewe mwenyewe?,,, tena Kwa kushirikiana na rafiki yako. Sijajua ni ushirikina ama ni tamaa za mwili. Mtoto wa miaka 3 unampa jeraha la moyo na historia ya maumivu katika maisha yake.
Hii ikapelekea mtoto baada ya kupimwa amekutwa na maambukizi ya virusi, ambayo ameambukizwa na rafiki wa baba yake. Kiukweli inasikitisha sana. Ata adhabu ya kifungo Cha maisha haiwastahili kabisa.
Sijakaa sawa, napokea tena taarifa mtoto amelawitiwa na Mjomba wake, kaka wa mama yake, mwenye mke na mtoto. Mtoto ana umri wa miaka 5, mpaka Sasa hospitali ndogo wameshindwa, wamempa transfer ya kuelekea hospitali kubwa ya serikali.... Hali yake ni mbaya... Inasikitisha sana.
Jamii nzima tuwe wa kwanza kuzuia hili jambo kutokea Kwa watoto wetu, tunawapa watoto jeraha la maisha, chuki ya maisha, majuto ya maisha. Wababa wamekuwa wakatili Kwa watoto zao.
Siku hizi hata kumuacha mwanao sijui Kwa bibi, sijui Mjomba, shangazi ,baba mkubwa, mtu unatakiwa kuwa makini haswaa, maana Kwa hivi vitendo vya Sasa ni masikitiko kupitiliza, huruma imetoweka. Wanawake wote waliojaa, kwenda kumteketeza mtoto Mdogo asiye na Kosa jamani.
Wamama hakikisheni unaposafiri, safiri na mtoto wako, hii ya kusema sijui namuacha na baba yake, namuacha na kaka yake,namuacha na jirani,. hujui usalama wake upoje pindi ambapo wewe haupo. Hii amekuja Mjomba ngoja alale na mtoto wangu, aisee utakuja kulia kilio kikuu siku ukigundua mwanao ameshaharibika.
Dunia inatia majonzi, watoto wanahitajika umakini Sana, hakuna kumuamini mtu. Na ni bora kumkagua mtoto wako mara Kwa mara, hii labda itasaidia kugundua mapema Hali sintofahamu Kwa mtoto wako.. na kumpa mtoto ujasiri wa kuzungumza na wewe, pindi anapoona anatendewa kitu kisichofaa1.
Haya matukio niliyoshughudia yameniumiza mnooo. Ngoja tusubiri Hali ya huyo mtoto itaendeleaje
Hii ikapelekea mtoto baada ya kupimwa amekutwa na maambukizi ya virusi, ambayo ameambukizwa na rafiki wa baba yake. Kiukweli inasikitisha sana. Ata adhabu ya kifungo Cha maisha haiwastahili kabisa.
Sijakaa sawa, napokea tena taarifa mtoto amelawitiwa na Mjomba wake, kaka wa mama yake, mwenye mke na mtoto. Mtoto ana umri wa miaka 5, mpaka Sasa hospitali ndogo wameshindwa, wamempa transfer ya kuelekea hospitali kubwa ya serikali.... Hali yake ni mbaya... Inasikitisha sana.
Jamii nzima tuwe wa kwanza kuzuia hili jambo kutokea Kwa watoto wetu, tunawapa watoto jeraha la maisha, chuki ya maisha, majuto ya maisha. Wababa wamekuwa wakatili Kwa watoto zao.
Siku hizi hata kumuacha mwanao sijui Kwa bibi, sijui Mjomba, shangazi ,baba mkubwa, mtu unatakiwa kuwa makini haswaa, maana Kwa hivi vitendo vya Sasa ni masikitiko kupitiliza, huruma imetoweka. Wanawake wote waliojaa, kwenda kumteketeza mtoto Mdogo asiye na Kosa jamani.
Wamama hakikisheni unaposafiri, safiri na mtoto wako, hii ya kusema sijui namuacha na baba yake, namuacha na kaka yake,namuacha na jirani,. hujui usalama wake upoje pindi ambapo wewe haupo. Hii amekuja Mjomba ngoja alale na mtoto wangu, aisee utakuja kulia kilio kikuu siku ukigundua mwanao ameshaharibika.
Dunia inatia majonzi, watoto wanahitajika umakini Sana, hakuna kumuamini mtu. Na ni bora kumkagua mtoto wako mara Kwa mara, hii labda itasaidia kugundua mapema Hali sintofahamu Kwa mtoto wako.. na kumpa mtoto ujasiri wa kuzungumza na wewe, pindi anapoona anatendewa kitu kisichofaa1.
Haya matukio niliyoshughudia yameniumiza mnooo. Ngoja tusubiri Hali ya huyo mtoto itaendeleaje