Huu Ubaguzi na Unyanyasaji wa Wachina kwa Waafrika Wenzetu huko Mji wa Guangzhou usinyamaziwe tafadhali

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,409
108,516
Wakati huku Afrika ( hasa nchini Tanzania ) Wachina pamoja na Serikali yao wakionekana ni Watu Wema na Marafiki wazuri kwa Sisi Waafrika tayari Wachina wameanza Kutuonyesha Waafrika ile Rangi yao halisi iliyomo Mioyoni mwao na pengine hili sasa litakuwa Fundisho kwa Mamlaka zetu.

Habari ikufikie hapo hapo ulipo kwamba kwa muda wa Siku Tatu nzima sasa Waafrika ( Watanzania wakiwemo ) waishio Mji wa Guangzhou ( Gwanzuu ) huko nchini China wameanza Kunyanyasika kwa Kubaguliwa na Wachina huku wakifukuzwa katika Nyumba zao wakidaiwa Kusambaza COVID-19.

Na taarifa ya muda si mrefu tu inaeleza kwamba Waafrika wengi hivi sasa wa huo Mji wanalazimika Kulala Mabarabarani huku wakiteseka na Baridi na wana Mazingira mabaya wakati wengine wakipigwa na Wachina na Kufukuzwa wakishutumiwa kuwa Wao ndiyo wanaeneza na wamepeleka huko Kirusi.

Tayari Serikali za Kenya na Afrika Kusini zimeanza Kulaani na Kuhoji hili hivyo basi nategemea haraka sana hata Serikali ya Tanzania nayo kwa kupitia Balozi wake huko watatoa Tamko na ikiwezekana hata Kulaani ila mkae mkijua ya kwamba hivi sasa Waafrika wenzetu Wananyanyasika huko China.

Watu tukiwa tunasema kuwa Wachina siyo Watu Wema na hawana Utu wala Huruma kwa Waafrika muwe mnatuelewa. Ila yawezekana hatutaeleweka katika hili kwakuwa tu hapa Kwetu Wachina wanaonekana ni Mungu wa Pili na Mshirika mwema wa Maendeleo na Misaada kwa Mamlaka.

Kwa Habari Kamili na za ndani kabisa juu ya Taarifa hii tembelea upesi Gazeti la Mtandaoni la The CITIZEN japo hata Radio One nao katika Taarifa yao ya Kutwa nzima ya Saa 4 Kamili hadi Saa 4 na Robo wameigusia pia katika Habari za Kimataifa. Tuwasaidieni Waafrika wenzetu huko Guangzhou.

Nawasilisha.
 
Watanzania tunapenda mno kulalamika...kule south afrika mweusi anambagua, kumnyanyasa na kumuuwa mweusi mwenzie, je hamlioni hilo?


Achilia mbali hilo, hapa juzi tu mchina kaambiwa na mtu mweusi mmetuletea corona hilo pia hamlioni?


Haya kwenye social media, mijitu mieusi inawasema vibaya wachina, macho madogo, wachafu, wametengeneza corona, virusi hivi ni vya wachina, mara sijui hawa wachina bora wafe wote siwapendi, juzi hapa kampuni ya Jack man na Ali baba wametusaidia vifaa vya kujikinga na hili janga, miafrika ikaanza uswahili oh wametuletea virusi ili watumalize kabisa....sipati picha wachina, wazungu, waarabu au wahindi wazungumzie haya maneno yakipumbavu kwenye social media sijui itakuwaje,

 
Wako sahihi kabisa! Kama hawako sahihi tunaweza kuwaprove kwa lipi kuwa wako wrong?
 
Wakati huku Afrika ( hasa nchini Tanzania ) Wachina pamoja na Serikali yao wakionekana ni Watu Wema na Marafiki wazuri kwa Sisi Waafrika tayari Wachina wameanza Kutuonyesha Waafrika ile Rangi yao halisi iliyomo Mioyoni mwao na pengine hili sasa litakuwa Fundisho kwa Mamlaka zetu.

Habari ikufikie hapo hapo ulipo kwamba kwa muda wa Siku Tatu nzima sasa Waafrika ( Watanzania wakiwemo ) waishio Mji wa Guangzhou ( Gwanzuu ) huko nchini China wameanza Kunyanyasika kwa Kubaguliwa na Wachina huku wakifukuzwa katika Nyumba zao wakidaiwa Kusambaza COVID-19.

Na taarifa ya muda si mrefu tu inaeleza kwamba Waafrika wengi hivi sasa wa huo Mji wanalazimika Kulala Mabarabarani huku wakiteseka na Baridi na wana Mazingira mabaya wakati wengine wakipigwa na Wachina na Kufukuzwa wakishutumiwa kuwa Wao ndiyo wanaeneza na wamepeleka huko Kirusi.

Tayari Serikali za Kenya na Afrika Kusini zimeanza Kulaani na Kuhoji hili hivyo basi nategemea haraka sana hata Serikali ya Tanzania nayo kwa kupitia Balozi wake huko watatoa Tamko na ikiwezekana hata Kulaani ila mkae mkijua ya kwamba hivi sasa Waafrika wenzetu Wananyanyasika huko China.

Watu tukiwa tunasema kuwa Wachina siyo Watu Wema na hawana Utu wala Huruma kwa Waafrika muwe mnatuelewa. Ila yawezekana hatutaeleweka katika hili kwakuwa tu hapa Kwetu Wachina wanaonekana ni Mungu wa Pili na Mshirika mwema wa Maendeleo na Misaada kwa Mamlaka.

Kwa Habari Kamili na za ndani kabisa juu ya Taarifa hii tembelea upesi Gazeti la Mtandaoni la The CITIZEN japo hata Radio One nao katika Taarifa yao ya Kutwa nzima ya Saa 4 Kamili hadi Saa 4 na Robo wameigusia pia katika Habari za Kimataifa. Tuwasaidieni Waafrika wenzetu huko Guangzhou.

Nawasilisha.
Na wakija huku wananyuka wenyeji viboko.
Hata MK254 anajua.
 
Njia sahihi ya kupambana na haya ni sisi WAAFRICA kuacha ujinga na kuzijenga nchi zetu za Africa ikiwa sambamba na kuboresha maisha ya watu wetu na kusiwe na nchi yeyote ya Africa inayoomba msaada au kutegemea Taifa lolote... Matatizo yote ya Africa tuyatatue wenyewe hapo kila mtu duniani atatuheshimu sisi WaAfrica..
 
Watanzania tunapenda mno kulalamika...kule south afrika mweusi anambagua, kumnyanyasa na kumuuwa mweusi mwenzie, je hamlioni hilo?


Achilia mbali hilo, hapa juzi tu mchina kaambiwa na mtu mweusi mmetuletea corona hilo pia hamlioni?


Haya kwenye social media, mijitu mieusi inawasema vibaya wachina, macho madogo, wachafu, wametengeneza corona, virusi hivi ni vya wachina, mara sijui hawa wachina bora wafe wote siwapendi, juzi hapa kampuni ya Jack man na Ali baba wametusaidia vifaa vya kujikinga na hili janga, miafrika ikaanza uswahili oh wametuletea virusi ili watumalize kabisa....sipati picha wachina, wazungu, waarabu au wahindi wazungumzie haya maneno yakipumbavu kwenye social media sijui itakuwaje,

Acheni ujinga kwakuwa mwafika wa SA anambagua mwafrika mwenZake ndio kusema mchina akibagua mwafrika watu wakae kimya! Haiwezekani wacha watu waseme, as long as ni ubaguzi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Njia sahihi ya kupambana na haya ni sisi WAAFRICA kuacha ujinga na kuzijenga nchi zetu za Africa ikiwa sambamba na kuboresha maisha ya watu wetu na kusiwe na nchi yeyote ya Africa inayoomba msaada au kutegemea Taifa lolote... Matatizo yote ya Africa tuyatatue wenyewe hapo kila mtu duniani atatuheshimu sisi WaAfrica..
Kwa kuanza, wewe anza kujenga uchumi wa familia yako, ndugu zako na wa jamii uliyotoka. Kila mmoja wetu akifanya hivyo nchi itakuwa huru kiuchumi.
 
ubaguzi ni asili ya mwadamu mwenye roho mbaya ilo chafu na ya kikatili,leo wachina watawabagua waafrika na kesho waafrika watawabagua wachina.
Waafrika watarudi Afrika na kuwabagua waafrika wenzao kwa sababu ya utaifa,dini,rangi na ukabila.
Ubaguzi wa hatari zaidi ni ule alonao muafrika kwa sababu anaweza kumbagua muafrika mwenzake
 
Acheni ujinga kwakuwa mwafika wa SA anambagua mwafrika mwenZake ndio kusema mchina akibagua mwafrika watu wakae kimya! Haiwezekani wacha watu waseme, as long as ni ubaguzi

Sent using Jamii Forums mobile app
Jumuia za kimataifa kama UN sijui zipo kwa leongo gani katika dunia hii,yani ni moja kati ya jumuia mbovu kabisa kuwahi kutokea dunia,leo walitakiwa wawe wamepiga kelele na kukemea ubaguzi huu lakini ndo kwanza sijui wapo mwezini saa hizi.
 
Hao Wachina wanaofanya hayo hawajui kuwa Daudi Albert Bashite ni RC wa Dar na anao uwezo wa kuwatenda lolote wakiwa huko kwenye ardhi yao?
Huu sasa ni utoto mkuu, mada hapa ni kuhusiana na ubaguzi wa rangi! Inashangaza kuona na hayo mengine pia.
 
Ubaguzi upo tu, unaanzia kwa mtu binafsi, familia, ukoo, serikali, jamii, rangi nk ni tabia za asili tunazo. Wageni wanatakiwa ku comply na sheria za wachina ili kuepusha kusambaa kwa ugonjwa. Mimi sipendezwi na wanachofanyiwa hawa ndgu zetu, lakini nilichokisikia ni kuwa wapo foreigners 5 walikuwa na covid 19, na serikali ikamua kuwapima waafrica wote kweny zile community na baada ya hapo wakawambia wajitenge kwa siku 14 hili linafanyika kwa watu wote wachina na wageni ikitokea kuna ugonjwa kweny makazi mfano community. Sasa wale ndugu walikiuka taratibu za quarantine wakatoka, ndipo taarifa zikaanza kusambaa kuwa wanasambaza ugonjwa (ingawa walipimwa wakakutwa hawana ugonjwa, walihitajika tu wajitenge ili baadaye wapimwe tena kabla ya kuwa huru). Sasa huku ukishakuwa mweusi ni mweusi tu, utaifa ni pembeni, wachina wakaanza kuwaepuka, kuhamasishana wasiwakaribishe kweny maeneo yao maana wamekiuka masharti ya wataalam, wengi wa wale watu ni Wanigeria na wengi inasemekana wanaishi bila kuwa na vibali ndio maana wanakuwa wakali hasa kuruhusu serikali ifanye kazi yake. Binafsi sijapata ubaguzi wa kiasi hiko na hata marafiki zangu weusi ninaowajua hakuna aliyepata shida kweny mji huu ninaoishi. Nimeenda mbali zaidi, nimekuwa na girlfriend wa kichina tangu mwanzoni 2018 mpk leo, na huwa tunasafiri kwend miji mbalimbali wkt mwingine kuna hotel wanakataa kupokea foreigners ila ukienda hotel za viwango wala hakuna shida kabisa. Msisahau kwamba wachina bado ni washamba sana na hawako informed sana
 
Bado tukifanya ivyo wanatuwekea vizingiti mfano ni Gadaffi na Mugabe
Njia sahihi ya kupambana na haya ni sisi WAAFRICA kuacha ujinga na kuzijenga nchi zetu za Africa ikiwa sambamba na kuboresha maisha ya watu wetu na kusiwe na nchi yeyote ya Africa inayoomba msaada au kutegemea Taifa lolote... Matatizo yote ya Africa tuyatatue wenyewe hapo kila mtu duniani atatuheshimu sisi WaAfrica..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ut
Wakati huku Afrika ( hasa nchini Tanzania ) Wachina pamoja na Serikali yao wakionekana ni Watu Wema na Marafiki wazuri kwa Sisi Waafrika tayari Wachina wameanza Kutuonyesha Waafrika ile Rangi yao halisi iliyomo Mioyoni mwao na pengine hili sasa litakuwa Fundisho kwa Mamlaka zetu.

Habari ikufikie hapo hapo ulipo kwamba kwa muda wa Siku Tatu nzima sasa Waafrika ( Watanzania wakiwemo ) waishio Mji wa Guangzhou ( Gwanzuu ) huko nchini China wameanza Kunyanyasika kwa Kubaguliwa na Wachina huku wakifukuzwa katika Nyumba zao wakidaiwa Kusambaza COVID-19.

Na taarifa ya muda si mrefu tu inaeleza kwamba Waafrika wengi hivi sasa wa huo Mji wanalazimika Kulala Mabarabarani huku wakiteseka na Baridi na wana Mazingira mabaya wakati wengine wakipigwa na Wachina na Kufukuzwa wakishutumiwa kuwa Wao ndiyo wanaeneza na wamepeleka huko Kirusi.

Tayari Serikali za Kenya na Afrika Kusini zimeanza Kulaani na Kuhoji hili hivyo basi nategemea haraka sana hata Serikali ya Tanzania nayo kwa kupitia Balozi wake huko watatoa Tamko na ikiwezekana hata Kulaani ila mkae mkijua ya kwamba hivi sasa Waafrika wenzetu Wananyanyasika huko China.

Watu tukiwa tunasema kuwa Wachina siyo Watu Wema na hawana Utu wala Huruma kwa Waafrika muwe mnatuelewa. Ila yawezekana hatutaeleweka katika hili kwakuwa tu hapa Kwetu Wachina wanaonekana ni Mungu wa Pili na Mshirika mwema wa Maendeleo na Misaada kwa Mamlaka.

Kwa Habari Kamili na za ndani kabisa juu ya Taarifa hii tembelea upesi Gazeti la Mtandaoni la The CITIZEN japo hata Radio One nao katika Taarifa yao ya Kutwa nzima ya Saa 4 Kamili hadi Saa 4 na Robo wameigusia pia katika Habari za Kimataifa. Tuwasaidieni Waafrika wenzetu huko Guangzhou.

Nawasilisha.
utanyamaziwa tu sisi shida yetu Mzungu akimnyanyasa mwafrika mweusi ndiyo tutapiga kelele weeeeee! Mwarabu na Mchina hata awatese vipi waafrika huwa tunakaa kimya! Hata waafrika kwa waafrika wakitesana tunakaa kimya
 
Back
Top Bottom