Kazi Ndiyo Kipimo Cha Utu
JF-Expert Member
- Mar 8, 2006
- 1,211
- 230
Unstoppable;
Ninanukuu Kauli ya Dr Ulimboka baada ya Kurudi Nchini amesema "apewe muda awe na familia yake na ukweli ya yote aliyofanyiwa ni yeye tu ndiye anayeujua"Mwisho wa Nukuu.
Kwa kauli hiyo inatia shaka kidogo kwamba bado Dr Ulimboka anasimamia yale aliyoyasema siku ya kwanza baada ya shambulio,Kama angekuwa anayasimamia hayo jibu lilikuwa rahisi sana kama unavyosema kwamba angethibitisha tu kwa kusema nilishaeleza yaliyonikuta na wote mnayajua na isingekuwepo hoja ya kwamba ni yeye tu ndiye anayejua kilichomtokea,Hii inafanya wengine tuamini alichoeleza baada ya kipigo kile yeye mwenyewe hakiamini na siyo ukweli na ndiyo maana ukweli ni yeye tu anayeujua.Na hili linawezekana hasa kutoka na athari za kipigo au amesema hivyo kama mbinu ya kujipanga na kujiridhisha kabla hajachukua hatua ya kuthibitisha yale aliyoyasema ndiyo hayo hayo.
Tafadhali naomba apewe muda ajipange na kama alivyoahidi nafikiri atatimiza ahadi,shauku yetu yakutaka kujua zaidi yasitufanye tusahau kuna maswala mengi kwake ya kuzingatia hasa baada ya yaliyomkuta na kuyapatia majibu likiwemo la ulinzi na usalama wake.
Ninanukuu Kauli ya Dr Ulimboka baada ya Kurudi Nchini amesema "apewe muda awe na familia yake na ukweli ya yote aliyofanyiwa ni yeye tu ndiye anayeujua"Mwisho wa Nukuu.
Kwa kauli hiyo inatia shaka kidogo kwamba bado Dr Ulimboka anasimamia yale aliyoyasema siku ya kwanza baada ya shambulio,Kama angekuwa anayasimamia hayo jibu lilikuwa rahisi sana kama unavyosema kwamba angethibitisha tu kwa kusema nilishaeleza yaliyonikuta na wote mnayajua na isingekuwepo hoja ya kwamba ni yeye tu ndiye anayejua kilichomtokea,Hii inafanya wengine tuamini alichoeleza baada ya kipigo kile yeye mwenyewe hakiamini na siyo ukweli na ndiyo maana ukweli ni yeye tu anayeujua.Na hili linawezekana hasa kutoka na athari za kipigo au amesema hivyo kama mbinu ya kujipanga na kujiridhisha kabla hajachukua hatua ya kuthibitisha yale aliyoyasema ndiyo hayo hayo.
Tafadhali naomba apewe muda ajipange na kama alivyoahidi nafikiri atatimiza ahadi,shauku yetu yakutaka kujua zaidi yasitufanye tusahau kuna maswala mengi kwake ya kuzingatia hasa baada ya yaliyomkuta na kuyapatia majibu likiwemo la ulinzi na usalama wake.
Last edited by a moderator: