Huu sasa si ufisadi na tamaa ya pesa bali ni pepo kabisa!

buyegiboseba

JF-Expert Member
Jun 3, 2011
535
145
Kitendo wa wataalamu wa wanyama,afisa afya na watendaji wa majinchio ya vingunguti kuruhusu kuletwa utumbo na nyama iliyooza na kuuzwa kwa wananchi,kimevuka hata mipaka ya ubinadamu
Ni kweli nchi inanuka rushwa na ufisadi lakini kwa kiwango cha namna hii,si kawaida ni pepo ndani ya watu!
Kwa hali ya kawaida,haihitaji kuwa msomi sana kubaini kuwa bidhaa ya kuoza kama ile italeta madhara madhara makubwa sana kwa watu na pengine hata ndugu wa karibu wa wahusika(kwani hakuna namna utafuatilia nani kanunua ili wewe usijikute unakula pia)
Niliangalia habari ile kwa masikitiko makubwa sana,nikafananisha na ya ekelege wa TBS kuruhusu bidhaa feki.
Tunahitaji ukombozi wa kiroho pia sio tu wa kupaka siagi wakati mkate ni ule ule uliokwisha muda wake

I sadly submit!
Source.ITV habari saa 2 usiku,6/5/2012.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom