Huu sasa ni mgogoro kati ya Watanzania na Chama chao tawala!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Mojawapo ya bajeti zitakazosababisha mzigo mkubwa kwa wananchi imepitishwa. KUpitishwa kwa bajeti hii nzima kunaashiria jambo moja kubwa CCM imefikia kikomo cha ubunifu wa kutatua matatizo ya wananchi iwe ni katika sera, sheria au utendaji. Kwa mwaka huu uliopita nimekuwa nikisisitiza sana watu kuelewa kuwa tatizo kubwa ambalo limechangia sana kuliingiza taifa kwenye matatizo mengi ni sera mbovu zilizoshindwa (japo hata wapinzani hawaamini sera za CCM ni mbovu).

Bajeti hii inadhihirisha msimamo wangu huo kwani bajeti hutoka kwenda kutekeleza sera mbalimbali. Sera hizi za CCM zimejaribiwa kwa miaka ishirini sasa na tayari zimeonesha kushindwa licha ya kupigwa 'tough' na mipango mbalimbali kama ya MKURABITA, MKUKUTA na Mpango wa maendeleo wa miaka mitano.

Kama hili ni kweli - na ninaamini ni kweli - basi kuna mgogoro kati ya Watanzania na chama chao tawala; mgogoro ambao hitimisho lake litaanzia 2014 (kwenye serikali za mitaa) na kwenye uchaguzi mkuu wa 2015. Mgogoro huu ni kamili na dhahiri. Ni mgogoro ambao hauwezi kuzimwa na ahadi, vitisho au kupuuzia. Ni mgogoro ambao hauwezi kutoweka hivi hivi isipokuwa kwa chama tawala kushindwa. Hata hivyo, tokeo hili litategemea moja kwa moja CDM itafanya nini to take advantage ya mgogoro huu. Hili ni swali ambalo muda utaamua.
 
Kabla huja ondoka mkuu, unaweza ukafafanua zaidi kwanini ume single out CHADEMA pekee km chama kinachoweza/takiwa ku capitalize katika hili ilhali tuna vyama vingi tu vya upinzani Tanzania?
 
Kabla huja ondoka mkuu, unaweza ukafafanua zaidi kwanini ume single out CHADEMA pekee km chama kinachoweza/takiwa ku capitalize katika hili ilhali tuna vyama vingi tu vya upinzani Tanzania?
Ngoja hapa nimsaidie Mwanakijiji. Ni kweli kuna vyama vingi vya siasa nchini Tanzania, lakini vingi hivyo ni vile ambavyo Kikwete ameviita vyama vya msimu. Chadema kimeonyesha kuwa si chama cha msimu na kama wasemavyo wazungu: it stands high above the rest.
 
CCM nafikiri ishawasoma watanzania wengi wakajua ni watu wa kupigwa porojo ndio maana wana ubavu wa kufanya wanachokitaka bila kuhofia chochote...
Kazi ya kutoa elimu kwa wananchi inatakiwa isiishie siku moja iwe ni zoezi la kdumu
 
Uzi una mantiki ingawa hukuweka steki sawasawa.

Sote twajua usanii huu wa ccm utaendelea mpaka mwakani, 2014 ishu yao kwisha! Lakini kabla ya hapo tunasubiri inevitable mpasuko utakaoongezwa na uchaguzi wa uongozi wa chama chao.

Kisha chaguzi za serikali za mitaa ccm wataona uhalisi wa mrejesho. Jinsi wasivyo relevant bajeti hii mbovu watatumia nguvu na gharama kubwa kuipigia debe.

Bado wanaamini sana ktk kutoa pipi kwa watanzania kwenye mambo muhimu. Bado ccm wataendelea kutumia rasilimali/akiba/nguvu kubwa kujaribu kufukia madhaifu ya serikali, sera na uwezo wao. CDM waendeleze elimu ya uraia, watoe sera zao na njia mbadala ya kuleta maendeleo hapa Tz.
 
Nimefurahishwa sana na kitendo cha kuita mbunge jina kila mmoja ili asema anaunga mkono hii bajeti au la. Kwa kufanya hivyo wananchi wanatakuwa na kumbukumbu sahihi kwa kila mbunge atakayetaka kuleta porojo 2015. Ni bajeti ya CCM 100%. Kwangu mimi mgogoro utaanza mapema kuliko 2014. By January 2013 tunaweza kuanza kuona mushikeli wa hii bajeti.

Dr Mgimwa ameongea kwa confidence sana na wabunge wa CCM wakaamini he's incharge!
 
hata wangesoma budget nzuri namna gani, bado uzoefu wa utekelezaji wake ni uleule miaka 50 iliyopita,
JK ni DHAIFU na CCM ni UPUUZI na wabunge ni WAJINGA.
 
kazi ipo ktk kukomboa nchi yetu,inahuzunisha sana kusikia watu wazima wanavyoshangilia kubitishwa kwa bajeti mzigo kwa wananchi.Inaama bajeti iliyopita niya chama?nn maana ya kuimba ccm ccm ccm baada ya kupitisha ujinga wao?ina maana bajeti imepitiswlhwa kwa maslai ya chama na si wananchi.WANAANDA KABURI LAO WENYEWE,NA TUTAWAZIKA TU.
 
Tutawapoteza kwa nguvu zote hawa wanafki wakubwa ccm{they know to talk our problems but they wil not implimate} kamwe hatutakubali porojo zao na propaganda zao. Vijana Daftari la wapiga kura likija nawaombeni MJIANDIKISHE WOTE ILI TUVUNJE NA KUUANGUSHA UTAWALA WA MKOLONI MWEUSI CCM.
 
Mbaya zaidi ni CCM kutumia kete ya uislam kuwahujumu wapinzani badala ya kutatua au hata kuangalia udhaifu wa sera na mipango yao. Leo nipo hapa Mtwara, kunamhadhara unaoendeshwa hapa uwanjani, mada ya mhadhara ni kuwasihi waislam waikatae CHADEMA eti ni chama cha wakristo na makafiri. Serikali na polisi CCM hawapo tayari hata kukemea tu uhuni huu kwa kuwa unakinufaisha chama twawala!
 
Nimesikitika zaidi nilipo ona wabunge wa ccm wanashangilia baada ya umeme kukatika.

Kweli ccm ni upuuzi.
Mimi nina mgogoro na ccm toka zamani.
 
Nasikia serikali ya wamagamba imeamua kuongeza kodi ya mishahara ya wafanyakazi ( PAYE) kama njia ya kutukomoa?
Kama kuna mfanyakazi ambaye bado anawapigia kura wamagamba ..**?##!!!@**.........
 
Siku zote nimekuwa nakerwa sana na kura za kiitikadi ya vyama bila kujali masilahi ya wananchi.

Kampeni ya kupiga kura za kiitikadi zilifikia kilele kwa mtazamo wangu pale naibu wa spika alipoanza kuwatisha wapinzani kwa kumtoa nje ya kikao Mheshimiwa Mnyika, jambo ambalo liliwajenga CCM kudhani wakiipitisha ile bajeti wanaikomoa kambi ya upinzani!

Wenye akili ya kupembua mambo wameona! Hongereni wote mlioikataa, jitihada zenu tumeziona na tunathamini. Ngoja tuone utekelezaji!
 
Suala lingine la msingi la kujiuliza hapa pia ni kwamba je taswira ya mgogoro huu unaouelezea wewe Mwanakijiji ni halisi? Je ni Watanzania wangapi wanaamini hivyo? Takwimu zinaonyesha asilimia karibu 80% ya Watanzania ni wakazi wa vijijini; ni wakulima na wengi ni maskini. Kwa mazingira haya ni wangapi wana habari kwamba bunge limeijadili bajeti inayogusa maisha yao na kama inawafaa au haiwafai ... kiasi cha kushawishika kuingia mgogoro na serikali yao.
 
Back
Top Bottom