Kiboko ya Jiwe
JF-Expert Member
- Apr 7, 2020
- 12,689
- 36,048
Twende kwenye mada direct!
Kuna Ustadhi ana duka la samaki wabichi mtaa mmoja huku Dar. Kaweka vijana 2 wanauza. Sijui ni ndugu zake au ni wafanyakazi tu.
Hili duka la samaki bei ni ya kawaida tu kama maduka mengine. Samaki wake na maduka mengine wapo pia. Cha ajabu anapanga foleni ya wateja kuanzia saa moja asubuhi mpaka jioni na giza. Siku moja nilimwambia wife twende kwenye lile duka ukajionee maajabu.
Tulifika dukani alasiri tukakuta duka limefungwa, majirani wakasema kuwa vijana wako msikitini basi tukavuta benchi kusubiri. Dk. kama 4 hivi wakarudi, ile kumaliza kufungua milango tu wateja wamejaa mpaka sisi wa kwanza kufika tukawa wa 4 kuhudumiwa.
Tulipoondoka nyuma watu wamepanga foleni wengi. Nimeona foleni kwenye biashara ila hii ni too much. Jirani yake ameshafungasha na kukimbia mtaa. Huyo jirani yake nilijua hana samaki aina nyingi au bei zake ni kubwa kumbe bei ni sawa tu na jamaa very humble kwa wateja ila anaishia kuharibikiwa na samaki huku mwenzake akitajirika. Bongo nyoso!
Anayetaka kuthibitisha aje Chanika sokoni nimpeleke ajionee maajabu.
Kuna Ustadhi ana duka la samaki wabichi mtaa mmoja huku Dar. Kaweka vijana 2 wanauza. Sijui ni ndugu zake au ni wafanyakazi tu.
Hili duka la samaki bei ni ya kawaida tu kama maduka mengine. Samaki wake na maduka mengine wapo pia. Cha ajabu anapanga foleni ya wateja kuanzia saa moja asubuhi mpaka jioni na giza. Siku moja nilimwambia wife twende kwenye lile duka ukajionee maajabu.
Tulifika dukani alasiri tukakuta duka limefungwa, majirani wakasema kuwa vijana wako msikitini basi tukavuta benchi kusubiri. Dk. kama 4 hivi wakarudi, ile kumaliza kufungua milango tu wateja wamejaa mpaka sisi wa kwanza kufika tukawa wa 4 kuhudumiwa.
Tulipoondoka nyuma watu wamepanga foleni wengi. Nimeona foleni kwenye biashara ila hii ni too much. Jirani yake ameshafungasha na kukimbia mtaa. Huyo jirani yake nilijua hana samaki aina nyingi au bei zake ni kubwa kumbe bei ni sawa tu na jamaa very humble kwa wateja ila anaishia kuharibikiwa na samaki huku mwenzake akitajirika. Bongo nyoso!
Anayetaka kuthibitisha aje Chanika sokoni nimpeleke ajionee maajabu.