Huu ni zaidi ya uchawi kwenye hii biashara ya huyu Ustadhi

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,689
36,048
Twende kwenye mada direct!

Kuna Ustadhi ana duka la samaki wabichi mtaa mmoja huku Dar. Kaweka vijana 2 wanauza. Sijui ni ndugu zake au ni wafanyakazi tu.

Hili duka la samaki bei ni ya kawaida tu kama maduka mengine. Samaki wake na maduka mengine wapo pia. Cha ajabu anapanga foleni ya wateja kuanzia saa moja asubuhi mpaka jioni na giza. Siku moja nilimwambia wife twende kwenye lile duka ukajionee maajabu.

Tulifika dukani alasiri tukakuta duka limefungwa, majirani wakasema kuwa vijana wako msikitini basi tukavuta benchi kusubiri. Dk. kama 4 hivi wakarudi, ile kumaliza kufungua milango tu wateja wamejaa mpaka sisi wa kwanza kufika tukawa wa 4 kuhudumiwa.

Tulipoondoka nyuma watu wamepanga foleni wengi. Nimeona foleni kwenye biashara ila hii ni too much. Jirani yake ameshafungasha na kukimbia mtaa. Huyo jirani yake nilijua hana samaki aina nyingi au bei zake ni kubwa kumbe bei ni sawa tu na jamaa very humble kwa wateja ila anaishia kuharibikiwa na samaki huku mwenzake akitajirika. Bongo nyoso!

Anayetaka kuthibitisha aje Chanika sokoni nimpeleke ajionee maajabu.
 
c224567f-e1a5-44fe-af27-19574812906d.jpg
 
Hii ndo bongo ukikosa wateja "HUNA NYOTA YA BIASHARA" Mara UMEROGWA ukipata wateja ni MWANGA unatumia MAJINI mara UCHAWI yaaani hawanaga positive mind unakuta uyo Ustadh anaSafirisha Samaki kutoka Mwanza Sato,Furu jumlisha Kambale,Kamongo sasa kwanini BIASHARA ISISHAMIRI WATEJA MKUU??Tujitahidi kuwa positive
 
Twende kwenye mada direct!

Kuna Ustadhi ana duka la samaki wabichi mtaa mmoja huku Dar. Kaweka vijana 2 wanauza. Sijui ni ndugu zake au ni wafanyakazi tu.

Hili duka la samaki bei ni ya kawaida tu kama maduka mengine. Samaki wake na maduka mengine wapo pia. Cha ajabu anapanga foleni ya wateja kuanzia saa moja asubuhi mpaka jioni na giza. Siku moja nilimwambia wife twende kwenye lile duka ukajionee maajabu.

Tulifika dukani alasiri tukakuta duka limefungwa, majirani wakasema kuwa vijana wako msikitini basi tukavuta benchi kusubiri. Dk. kama 4 hivi wakarudi, ile kumaliza kufungua milango tu wateja wamejaa mpaka sisi wa kwanza kufika tukawa wa 4 kuhudumiwa.

Tulipoondoka nyuma watu wamepanga foleni wengi. Nimeona foleni kwenye biashara ila hii ni too much. Jirani yake ameshafungasha na kukimbia mtaa. Huyo jirani yake nilijua hana samaki aina nyingi au bei zake ni kubwa kumbe bei ni sawa tu na jamaa very humble kwa wateja ila anaishia kuharibikiwa na samaki huku mwenzake akitajirika. Bongo nyoso!

Anayetaka kuthibitisha aje Chanika sokoni nimpeleke ajionee maajabu.
Chanika na temeke yote mpak uwe unajua kupuliza ,
 
Ssa na wew kwanin hukuenda kwa huyo mwengine pia umeenda kwake!?!!

Hii nayo ni taarifa ya habari
Kuna mahali nimesema kuwa jamaa ni humble kwa wateja ina maana huwa nakwenda siku moja moja. Hiyo siku niliyokuwa na wife nilikwenda kumwonyesha jambo ambalo mara nyingi nilikuwa namsimulia
 
Hakuna kitu ambacho hakina sababu, wala usiwaze ushirikina

Pia kuna kitu kinaitwa herd mentality watu wakiona wengine wanakwenda sehemu fulani na pengine hawaendi wote wanakimbilia huko wakijua ndio penyewe....

Ndio maana wewe unaweza kuuza wanyama wako kadhaa wanaokupa maziwa na nyama na mbolea na kununua kijiwe cha kuvaa shingoni sababu watu / majority ndio wana-percieve kwamba hicho kijiwe kina thamani zaidi..., na wewe hapo utajiona mjanja na kwamba upo cool (ila kumbe mjanja ni yule gwiji wa kufanya marketing) Katambuga za mmasai leo ukiziwekea nembo ya nike au Adidas huenda watu watanunua kwa bei maradufu....
 
Mwenzio anasali wengine wanakomaa na hela hawawezi kupata baraka
Kusali Imani, Kuroga Imani zote zinakupa confidence na haukati tamaa ila mwisho wa siku hakuna devine intervation ukifuata kanuni za pesa au kucheza faulo wengine hawachezi lazima utawazidi kwenye game....

Ingekuwa do -gooders ndio wanafanikiwa kuliko wacheza faulo dunia ingekuwa haina wanyonyaji since beginning of time...., Watumwa walikuwa wanasali na bakora walipigwa na waliendelea kupigwa kama sasa hivi the power that be wanavyolamba asali wakati kina nyie mnapigwa bakora la Tozo
 
Back
Top Bottom