Elections 2010 Huu ni wizi kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma

Ngalikivembu

JF-Expert Member
Oct 6, 2010
1,959
872
Kama kuna kero ambayo wananchi wa Mkoa wa Ruvuma wanaipata hasa kwa wamiliki wa magari ya abiria basi hili la kuchukua ushuru unaoitwa wa kuboreshwa kwa mji wa Songea.Kila barabara inayoingia mjin Songea kilomita 5 hadi 6 imewekewa kizuia(road block) kwa ajili ya kusimamisha magari yote yanayofanya biashara na kukusanya pesa ya maendeleo.lakini cha ajabu na kwa uchunguzi niliofanya kwa muda mrefu sasa imeonekana kuwa huu ni mradi wa baadhi ya watawala hapa mkoani.Kwani pesa inayokusanywa kila siku haioneshi kama inatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Bado barabara zetu ni chafu.Ukija stand kuu ya mabasi napo kuna kamba imewekwa pale ili kila gari linaloingia stendi na kutoka linapaswa kulipa pesa.Jamani sijapata ona stand ovyo kama hii ya Songea.Utadhani sio Manispaa.Ni bora isingepandishwa hadhi ya kuitwa manispaa.Tunajiuliza hivi hizi pesa zinazokusanywa zinakwenda wapi?Nimepata kuwauliza wale wakusanya ushuru,walitoa kauli ambazo zinathibitisha kuwa huu ni mradi wa wajanja.Nao kwa kutambua kuwa huu si mradi wa serikali iliyo makini huwa hawatoi risiti kwa madereva baada ya malipo.Sasa tunajiuliza ikiwa mtu anakusanya pesa bila kuwaonesha ushahidi wa makusanyo hayo,je kweli kuna uhalali hapo?Tuite ufisadi mdogo mdogo?Wako wapi viongozi wetu?Tupeni majibu kwanini stand hii ipo katika hali mbaya?
 
majibu: ujuha wa kuwaamini CCM miaka yote na yote, kwa CCM kama mnanyanyasika ndio maisha bora ali mradi wakubwa wanakula vizuri
 
CHAGUENI CHADEMA , yote hayo msingeyapata, sasa CCM wanarudisha gharama za uchaguzi mtakoma mpaka miaka mitano iishe hahahaaha mtakula MAJEKO (VIAZI JESHI) KWa MBULIKA(KUMBIKUMBI) mpaka mshangae hahahahah
 
Nao kwa kutambua kuwa huu si mradi wa serikali iliyo makini huwa hawatoi risiti kwa madereva baada ya malipo.Sasa tunajiuliza ikiwa mtu anakusanya pesa bila kuwaonesha ushahidi wa makusanyo hayo,je kweli kuna uhalali hapo?Tuite ufisadi mdogo mdogo?Wako wapi viongozi wetu?Tupeni majibu kwanini stand hii ipo katika hali mbaya?

Mkuu in-short, ni uzembe wa hali ya juu kulipa kodi yoyote inayosemekana ni yaserikali bila kupewa risiti. Kwani hao madreva wakikataa watafanywa nini.
 
Wana ruvuma mme jiatkia kwa kuichagua ccm,na badooooooooooooooooooooooooooooooooo,mtajuta kuikacha chadema.
 
Watu wa kusini ni wagumu sana kubadilika sijui wanamatatizo gani, na hasa ruvuma kw anchimbi.
 
sasa inabidi halmashauri zote yaliyo chini ya chadema kero kama hizi ziondolewe ili wengine wajifunze kutoka huko. naami 2015 nao watakubali kuachana na ccm.
 
wanaona mabadiliko hayawezekani hata wanawa Israel walikuwa wanamlalamikia na kumtuhumu Musa kwa kuwatoa misiri na kuwapeleka nchi ya kanani
 
Huu mfumo wetu Tanzania wa kukusanya mapato, kutoa malipo na kulipa kodi unaniweka hoi. Ijapokuwa malipo ni halali na unapewa risiti, kuna uwezekano kuwa risiti hizo ni feki (kuna watu wanarudufu risiti zao), na malipo hayo yakaishia matumboni mwa walafi.
Nimeona mfumo wa nchi moja, ambapo malipo yoyote rasmi, iwe katika sekta ya umma au binafsi, daima hupeleki pesa ofisini na kuwaachia watu kuchota na kuchachachua. Badala yake unapewa risiti kwenda kulipa benki (hata kama ni senti 5), ambako idara au shirika husika lina akaunti yake. Lakini petu, mtu unamlipa barabarani. Huu si wizi ni nini? Ama kweli sisi ni wadanganyika!
 
huko ruvuma si ndiko hawataki vyama vingine? wao na ccm tu> wanalialia nini?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom