Huu ni wakati wa kusimamia misingi ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
8,708
5,711
Taifa letu tangu limepata uhuru limekuwa likitawaliwa kwa misingi ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sheria za nchi yetu

Ndio maana hatuoni nchi hii ikiendeshwa kwa presidential decrees au ubabe na udikteta.

Tulishuhudia bunge la kumi jinsi lilivyoweza kuiadhibu serikali kwa kutokuwa na imani na Waziri Mkuu wakati huo. Na kila mtu alishangaa kwa namna serikali ilivyowajibika kama ibara ya 53A ya katiba ya Jamhuri ya Muungano Tanzania inavyosema.

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama Mbunge akifukuzwa uanachama, Mbunge huyo hupoteza uanachama wake. Hii ni kwa mujibu wa ibara ya 67(1)(b). Kwa hiyo Mbunge akifukuzwa uanachama wa chama chake basi hana shavu tena.

Kwa hiyo ili amani kwenye Taifa lolote ili amani itamalaki lazima Katiba ya Taifa hilo iheshimiwe na kusimamiwa.

Hivyo basi Spika wa Bunge letu aheshimu na kusimamia misingi ya katiba yetu. Kama kweli Halima Mdee na wenzake 18 wamefukuzwa uanachama CHADEMA basi sio wabunge halali tena. Watanzania tunaopenda utawala wa sheria tutashangaa spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwakingia kifua watu kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
CCM,NEC,BUNGE na MAHAKAMA vyote vipo macho kuwalinda COVID-19... kumbuka cuf walishafukuza wabunge wao lkn serikali hii ya kijinga iliendelea kuwalinda Kwa nguvu zote, sikuzote maccm ni maisha Yao kujitoa ufahamu
 
Hahahahahahahah 😂😂😂🤣🤣🤣
chagu wa malunde leo ccm wamekurudishia ubongo wako au account yako anatumia mtu mwingine?

Kwa kweli leo umeongea kama binadamu mwenye ubongo unaofanya kazi... Hongera sana
Kijana naomba tuheshimiane, lini Ccm walichukua ubongo wangu? Lini nimeongea pumba? Mimi ni mtu ninaejitambua.
 
Ukiona viongozi wameanza kusigina katiba waziwazi bila hofu yoyote ujue machafuko yanakaribia! Imebaki botton 1 tu ya 0 -tolerance. Siku ikibonyezwa taifa letu litaangamia!
Hatuwezi kufika huko ndio maana tunawakumbusha. Maana hatutaki kufikia huko.
 
Taifa letu tangu limepata uhuru limekuwa likitawaliwa kwa misingi ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sheria za nchi yetu

Ndio maana hatuoni nchi hii ikiendeshwa kwa presidential decrees au ubabe na udikteta.

Tulishuhudia bunge la kumi jinsi lilivyoweza kuiadhibu serikali kwa kutokuwa na imani na Waziri Mkuu wakati huo. Na kila mtu alishangaa kwa namna serikali ilivyowajibika kama ibara ya 53A ya katiba ya Jamhuri ya Muungano Tanzania inavyosema.

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama Mbunge akifukuzwa uanachama, Mbunge huyo hupoteza uanachama wake. Hii ni kwa mujibu wa ibara ya 67(1)(b). Kwa hiyo Mbunge akifukuzwa uanachama wa chama chake basi hana shavu tena.

Kwa hiyo ili amani kwenye Taifa lolote ili amani itamalaki lazima Katiba ya Taifa hilo iheshimiwe na kusimamiwa.

Hivyo basi Spika wa Bunge letu aheshimu na kusimamia misingi ya katiba yetu. Kama kweli Halima Mdee na wenzake 18 wamefukuzwa uanachama CHADEMA basi sio wabunge halali tena. Watanzania tunaopenda utawala wa sheria tutashangaa spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwakingia kifua watu kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mawazo yako ndio hali inavyotakiwa kuwa, lakini nani anafuata Katiba kwa sasa. Uliyemtag ameshasema atawalinda kina HALIMA kwa gharama yoyote. GHARAMA YOYOTE ni pamoja na kuvunja katiba.
 
Taifa letu tangu limepata uhuru limekuwa likitawaliwa kwa misingi ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sheria za nchi yetu

Ndio maana hatuoni nchi hii ikiendeshwa kwa presidential decrees au ubabe na udikteta.

Tulishuhudia bunge la kumi jinsi lilivyoweza kuiadhibu serikali kwa kutokuwa na imani na Waziri Mkuu wakati huo. Na kila mtu alishangaa kwa namna serikali ilivyowajibika kama ibara ya 53A ya katiba ya Jamhuri ya Muungano Tanzania inavyosema.

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama Mbunge akifukuzwa uanachama, Mbunge huyo hupoteza uanachama wake. Hii ni kwa mujibu wa ibara ya 67(1)(b). Kwa hiyo Mbunge akifukuzwa uanachama wa chama chake basi hana shavu tena.

Kwa hiyo ili amani kwenye Taifa lolote ili amani itamalaki lazima Katiba ya Taifa hilo iheshimiwe na kusimamiwa.

Hivyo basi Spika wa Bunge letu aheshimu na kusimamia misingi ya katiba yetu. Kama kweli Halima Mdee na wenzake 18 wamefukuzwa uanachama CHADEMA basi sio wabunge halali tena. Watanzania tunaopenda utawala wa sheria tutashangaa spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwakingia kifua watu kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Awamu hii ni vurugu match, ulimbukeni na usakubimbi +blaah blaah
 
Mawazo yako ndio hali inavyotakiwa kuwa, lakini nani anafuata Katiba kwa sasa. Uliyemtag ameshasema atawalinda kina HALIMA kwa gharama yoyote. GHARAMA YOYOTE ni pamoja na kuvunja katiba.
Kwani hajui madhara ya kuvunja misingi ya katiba?
 
Mirija ikikatwa utasikia mayowe kila kona , kunyimwa posho ya wiki 2 tu umerudi kwenye mstari kudadeki ! ama kweli njaa haina baunsa !

FB_IMG_1578677028602.jpg
 
Nani yupo juu ya sheria hapa Tanzania? Hujui kuwa bunge linamlaka ya kumvua urais kama atatumia madaraka yake vibaya?
Bunge lipi ilo mkuu? Au unasema like lililo chini yake.
Kuingiria haki ya vyama vya Siasa sini kinyume cha Katiba mkuu...
 
Back
Top Bottom