Huu ni wakati adhimu wa upinzani kuchukua nchi, CCM imechoka na imechokwa

Memento

JF-Expert Member
Jun 13, 2021
4,423
9,962
Upinzani kwenye serikali yoyote ile ni lazima uwepo ili kuharakisha Maendeleo, achana na yale maneno eti upinzani ulituchelewesha.

Miaka yote CCM wanatawala wao ila hakuna jipya zaidi ya kutubadilishia tu nyimbo.
Alianza JK na Kasi mpya, ari mpya ila mwisho wa siku hakuna lolote lile, ni umasikini mwanzo mwisho kwa watanzania.

Akaja Magufuli na kauli mbiu yake ya Tanzania ya viwanda ila nao hakuna lolote lile zaidi ya porojo tu.

Sasa hivi tupo na mama, yeye anakuambia kazi iendelee. Iendelee wapi? Maneno laini, matamu ila hakuna lolote lile ni yaleyale tu.

Ni wakati muafaka sasa wa CCM kukaa pembeni ,mpishe na wengine. CCM hamjazaliwa kutawala nyie tu Tanzania.

Kwani mkiachia upinzani nao tukapata hata miaka mitano shida ipo wapi? Hapa nazungumzia upinzani Chadema na sio wale wengine wasaka tonge na uteuzi. Chama Cha upinzani makini nchi hii ni chadema tu. Huo ndio ukweli.

Nawaomba wale wote ambao tunasupport upinzani kwa hali na mali tuungane na tushikamane zaidi kuangusha hawa CCM. Hii kazi sio rahisi ila Mimi ninaona ni muda muafaka na adhimu kuwaangusha sasa, tusichoke, tusikate tamaa, wataanguka tu inahitajika nguvu kidogo sana.

Tusitarajie lolote chini ya CCM hii na yoyote itayokuja.

Hebu fikiria chama kimejaza watu wanaowaza uteuzi tu, alafu ndio hawa wanataka kuendelea kutawala. HAPANA CCM juenj kuwa siku zenu si nyingi mtaanguka.
 
Upinzani upi wa kuchukua nchi Tanzania?
Hao wanaojiita wapinzani hata hawajitambui sasa wachukue nchi gani
 
Tusiwe na uchaguzi, twende nao hawahawa. Mbinu zote haramu wanazo. HAKUNA UCHAGUZI HUFANYIKA TZ, Hupita bila kupingwa
 
Changamoto kubwa iliyopo kwa tanzania ya sasa na baadae ni katiba mpya tu, Kama tuna taka hayo maendeleo tubayotarajia yasikae mbali na umma basi muda muafaka wa kudai katiba mpya vinginevyo CCM hakiwezi kuachia ngazi kwa sanduku la kura.

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Upinzani kwenye serikali yoyote ile ni lazima uwepo ili kuharakisha Maendeleo, achana na yale maneno eti upinzani ulituchelewesha.
Miaka yote CCM wanatawala wao ila hakuna jipya zaidi ya kutubadilishia tu nyimbo.
Alianza JK na Kasi mpya, ari mpya ila mwisho wa siku hakuna lolote lile, ni umasikini mwanzo mwisho kwa watanzania.
Akaja Magufuli na kauli mbiu yake ya Tanzania ya viwanda ila nao hakuna lolote lile zaidi ya porojo tu.
Sasa hivi tupo na mama, yeye anakuambia kazi iendelee. Iendelee wapi? Maneno laini, matamu ila hakuna lolote lile ni yaleyale tu.
Ni wakati muafaka sasa wa CCM kukaa pembeni ,mpishe na wengine. CCM hamjazaliwa kutawala nyie tu Tanzania.
Kwani mkiachia upinzani nao tukapata hata miaka mitano shida ipo wapi? Hapa nazungumzia upinzani Chadema na sio wale wengine wasaka tonge na uteuzi. Chama Cha upinzani makini nchi hii ni chadema tu. Huo ndio ukweli.
Nawaomba wale wote ambao tunasupport upinzani kwa hali na mali tuungane na tushikamane zaidi kuangusha hawa CCM. Hii kazi sio rahisi ila Mimi ninaona ni muda muafaka na adhimu kuwaangusha sasa, tusichoke, tusikate tamaa, wataanguka tu inahitajika nguvu kidogo sana.
Tusitarajie lolote chini ya CCM hii na yoyote itayokuja.
Hebu fikiria chama kimejaza watu wanaowaza uteuzi tu, alafu ndio hawa wanataka kuendelea kutawala. HAPANA
CCM juenj kuwa siku zenu si nyingi mtaanguka.

Kuelekea huko tujikite kupata katiba mpya kwanza.

Hapo yeyote atakeichukua nchi kwa mujibu wa katiba atakuwa mshindi. Sote tutakuwa washindi.
 
Upinzani upi wa kuchukua nchi Tanzania?
Hao wanaojiita wapinzani hata hawajitambui sasa wachukue nchi gani
Na hilo group lote la waliokuwa wapinzani ambao mmewachukua wawasaidie kwenye uongozi unadhani walitoka wapi? Almost wengi hapo ndio walewale watakaokuwa viongozi upinzani ukichukua nchi.

Kimsingi hamjajua tu kwamba bwawa mnaloogelea tayari kuna mamba Ila nyie endeleeni kudemka tu.
 
Na hilo group lote la waliokuwa wapinzani ambao mmewachukua wawasaidie kwenye uongozi unadhani walitoka wapi? Almost wengi hapo ndio walewale watakaokuwa viongozi upinzani ukichukua nchi.

Kimsingi hamjajua tu kwamba bwawa mnaloogelea tayari kuna mamba Ila nyie endeleeni kudemka tu.
Waganga njaa hawatishii lolote,, kuitoa CCM bado sana labda miaka 100 ijayo
 
Kwani mkiachia upinzani nao tukapata hata miaka mitano shida ipo wapi? Hapa nazungumzia upinzani Chadema na sio wale wengine wasaka tonge na uteuzi. Chama Cha upinzani makini nchi hii ni chadema tu. Huo ndio ukweli.
Hivi huu ujinga wa kudhani kwamba mtaachiwa kuongoza nchi bila kuonyesha chochote cha maana kinachoweza kuwafanya muaminike na kuchaguliwa utakwisha lini?

Tuonyesheni kitu tofauti na ccm ili tuwaone nyie ni option bora kuliko ccm ili tuwachague. Wananchi hatuoni chochote kutoka kwenu; hata ofisi tu ya makao makuu mmeshindwa kujenga, hata kiwanja cha kujenga kiofisi cha makao makuu hamna, mnataka tuwakabidhi kuongoza nchi, hivi mnatuona sisi ni hamnazo kama tundu lisu siyo?

Acheni porojo, jijengeni kama chama, fanyeni kazi, jihusisheni na mahitaji ya wananchi: utafika wakati tutawaamini na kuwachagua. Lakini kwa porojo hizi za sasa, na wagombea uchwara km kina lisu, msitegemee kupewa kuongoza nchi.
 
Vijana tafuteni kazi mpate vipato, fungueni biashara, limeni, chezeni ngoma nk

Msipoteze muda saaaana kuwaza kuchukua nchi

Nchi ipo tu na haiondoki, tena ndio inazidi kunawiri

But a good country inaletwa na wananchu, siyo wenye kutaka kuchukua nchi
 
Upinzani kwenye serikali yoyote ile ni lazima uwepo ili kuharakisha Maendeleo, achana na yale maneno eti upinzani ulituchelewesha.
Miaka yote CCM wanatawala wao ila hakuna jipya zaidi ya kutubadilishia tu nyimbo.
Alianza JK na Kasi mpya, ari mpya ila mwisho wa siku hakuna lolote lile, ni umasikini mwanzo mwisho kwa watanzania.
Akaja Magufuli na kauli mbiu yake ya Tanzania ya viwanda ila nao hakuna lolote lile zaidi ya porojo tu.
Sasa hivi tupo na mama, yeye anakuambia kazi iendelee. Iendelee wapi? Maneno laini, matamu ila hakuna lolote lile ni yaleyale tu.
Ni wakati muafaka sasa wa CCM kukaa pembeni ,mpishe na wengine. CCM hamjazaliwa kutawala nyie tu Tanzania.
Kwani mkiachia upinzani nao tukapata hata miaka mitano shida ipo wapi? Hapa nazungumzia upinzani Chadema na sio wale wengine wasaka tonge na uteuzi. Chama Cha upinzani makini nchi hii ni chadema tu. Huo ndio ukweli.
Nawaomba wale wote ambao tunasupport upinzani kwa hali na mali tuungane na tushikamane zaidi kuangusha hawa CCM. Hii kazi sio rahisi ila Mimi ninaona ni muda muafaka na adhimu kuwaangusha sasa, tusichoke, tusikate tamaa, wataanguka tu inahitajika nguvu kidogo sana.
Tusitarajie lolote chini ya CCM hii na yoyote itayokuja.
Hebu fikiria chama kimejaza watu wanaowaza uteuzi tu, alafu ndio hawa wanataka kuendelea kutawala. HAPANA
CCM juenj kuwa siku zenu si nyingi mtaanguka.
Hizi ndoto mnazoota baada ya kushinda mchana kutwa mnacheza karata muwe mnabakia nazo hukohukooo. Hivi kwa akili yako unaona kwa miaka 200 ijayo kuna kikundi chochote kinachoweza ata kuwaza tu kuiondoa CCM madalakani?
 
CCM imechoka na imechokwa, lakini ukweli mchungu bado hamna upinzani imara wa kuchukua nchi , sijui ni ccm wanapenyeza vibaraka wao sijui ni watu tu na tamaa zao za madaraka...

Wengi walio upinzani ndio dizaini za kina mdee na wengineo, safari bado ni ndefu.
 
CCM imechoka na imechokwa, lakini ukweli mchungu bado hamna upinzani imara wa kuchukua nchi , sijui ni ccm wanapenyeza vibara wao sijui ni watu tu na tamaa zao za madaraka...

Wengi walio upinzani ndio dizaini za kina mdee na wengineo, safari bado ni ndefu.
Njaa mbaya sana
 
Back
Top Bottom